Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy

Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy The Chama Cha Mapinduzi CCM


( Revolution Party) is the dominant ruling party in Tanzania CCM CHAMA MAKINI KINACHOFANYA MAAMUZI KWA VIKAO RASMI

WASIRA: HAKUNA MTU 'ALIYESHUGHULIKIWA' KWA KUWASEMEA WATANZANIANa MWANDISHI WETUMAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi...
08/09/2026

WASIRA: HAKUNA MTU 'ALIYESHUGHULIKIWA' KWA KUWASEMEA WATANZANIA

Na MWANDISHI WETU

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM - Bara), Stephen Wasira, amesema hakuna mtu anayeshughulikiwa kwa sababu ya kuwasemea wananchi, akisisitiza kuwa kauli yoyote ya kukosoa inapaswa kuungwa mkono na utafiti na ushahidi.

Wasira amesema kauli kwamba mtu anaweza kushughulikiwa kwa sababu amezungumza kwa niaba ya wananchi si sahihi, akimtaka kila anayetoa madai hayo kufanya utafiti kabla ya kuzungumza.

Amesema hayo leo Septemba 8, 2026 katika mkutano wa wadau wa kitaifa wa kitafakari kutafakari hali ya siasa nchini, jijini Dar es Salaam.

Amesema wasomi wana wajibu mkubwa wa kufanya utafiti, kwa kuwa utafiti ni sehemu muhimu ya usomi na humsaidia mtu kutoa taarifa na hoja zenye msingi.

“Usipotafiti utasema chochote tu, utakuwa k**a mitandao ya kijamii ambayo haina control, (udhibiti)” amesema Wasira.

Kwa mujibu wa Wasira, hakuna aliyesema kwa niaba ya wananchi kisha akaondolewa au kushughulikiwa kwa sababu hiyo, amesisitiza kuwa viongozi na wananchi wote ni sehemu ya jamii moja.

Amesema kauli kwamba mtu fulani anazungumza kwa niaba ya wananchi inapaswa kuangaliwa kwa kuzingatia ushahidi wa wananchi hao ni akina nani na walitoa wapi mamlaka ya kuwakilishwa.

Wasira ametoa mfano wa suala la Katiba Mpya, akisema CCM iliahidi katika Ilani yake ya Uchaguzi kuhusu suala hilo, huku akieleza kuwa utekelezaji wake unahitaji kuangalia mazingira na changamoto zilizopo.

Amesema hata Katiba ya mwaka 1984 ilitokana na Katiba ya mwaka 1977, akieleza kuwa mabadiliko ya katiba yamekuwa yakitokana na mahitaji na changamoto zilizojitokeza katika vipindi tofauti.

Ameongeza kuwa wakati wa kuandaa mipango ya utekelezaji, baadhi ya matukio hayawezi kutabirika mapema, hivyo muda na mazingira vinaweza kulazimisha kufanya marekebisho ya hatua zilizopangwa.

Wasira amesema suala la Katiba Mpya halijaachwa, bali mchakato wake unapaswa kuendelea kwa kuzingatia uamuzi na mipango iliyowekwa.

Amesema mtu anapowataka wananchi “wapambane,” ni muhimu pia kujiuliza wanapambana na nani, kwa kuwa wakati mwingine changamoto zinazozungumziwa zinahitaji juhudi za pamoja badala ya kuonekana kana kwamba kun

TAARIFA KWA UMMA
08/09/2026

TAARIFA KWA UMMA

SALAMU ZA RAMBIRAMBI  🙏
07/09/2026

SALAMU ZA RAMBIRAMBI
🙏

05/09/2026

CCM NDICHO CHAMA KINACHOWASIKILIZA ZAIDI WANANCHI NCHINI - KIHONGOSI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama kinachowasikiliza zaidi wananchi nchini, kikieleza kuwa maandalizi yake pamoja na ushirikiano mzuri na wananchi katika mikutano ya kampeni ni miongoni mwa viashiria vya kukubalika kwake kwa umma.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi akihojiwa na kituo cha televisheni cha Star TV Septemba 05, 2026 kuhusu matukio ya ghasia, uharibifu wa mali na vifo vilivyotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 29.

Akijibu hoja ya iwapo matukio hayo yalitokana na CCM kuwa na kiburi na kushindwa kuwasikiliza wananchi, Kihongosi amesisitiza kuwa chama hicho ndicho kinachowasikiliza wananchi zaidi, akitaja namna kilivyojiandaa na ushirikiano uliokuwepo katika mikutano yake ya kampeni.

Kuhusu chanzo cha ghasia hizo, Kihongosi amesema hazikutokana na CCM, bali zilihamasishwa na makundi ya kisiasa au taasisi zilizotoa kauli za kuvuruga na kuzuia uchaguzi baada ya kuona kuwa zisingeweza kushinda.

Amesema vyombo vya ulinzi na usalama vina wajibu wa kulinda wananchi pamoja na mali zao, huku akieleza kuwa Rais aliunda tume za uchunguzi, zikiwemo Tume ya Jaji Chande na Jaji Lila, kwa ajili ya kuchunguza kwa kina matukio hayo na kubaini wahusika.

Katika hatua nyingine, Kihongosi amesisitiza kuwa CCM k**a chama hakikuhusika na matumizi ya silaha wala kuwadhuru wananchi, akiwataka wananchi kusubiri ripoti rasmi za tume zilizoundwa kisheria ambazo, kwa mujibu wake, zitatoa majibu kuhusu matukio hayo.

WASIRA ATETA NA WABUNGE WA CCM.MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM - Bara), Stephen Wasira, amekutana na kuzun...
02/09/2026

WASIRA ATETA NA WABUNGE WA CCM.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM - Bara), Stephen Wasira, amekutana na kuzungumza na Kamati ya Wabunge wa CCM, leo tarehe 2, Septemba 2026, katika Ukumbi wa White House Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma.

Katika kikao hicho Wasira aliambatana na ujumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ukiongozwa na Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro.

Kwa niaba ya Wanachama wa CCM  Tawi la  Chama Cha Mapinduzi  Napoli Italy. Tunapenda kumpongeza Makamu wa Rais kwa uapis...
29/08/2026

Kwa niaba ya Wanachama wa CCM Tawi la Chama Cha Mapinduzi Napoli Italy. Tunapenda kumpongeza Makamu wa Rais kwa uapisho rasmi Kwa nafasi hiyo kubwa ya kumsaidia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutekekeza Ilani ya Chama chetu na kuliongoza taifa letu. Tunampongeza mwenyekiti wa Chama Dkt. Samia Suluhu Hassan,wajumbe wote wa Kamati kuu ya CCM na Halmashauri kuu kwa maamuzi yote yaliyofanyika na kufikia kupendekeza jina la Mhe. Deogratius John Ndejembi .

UAPISHO WA MAKAMU WA RAIS
29/08/2026

UAPISHO WA MAKAMU WA RAIS

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakiogozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndg. Stephen Wasira wakati wa hafla ya Uapisho wa Ma...
29/08/2026

Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakiogozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndg. Stephen Wasira wakati wa hafla ya Uapisho wa Makamu wa Rais Mteule wa Tanzania Mhe. Deogratius John Ndejembi Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo Agosti 29,2026.

27/08/2026

MWIGULU AMPONGEZA NDEJEMBI, AMSIFU RAIS SAMIA KWA KUMCHAGUA MTU MAHIRI NA MCHAPAKAZI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amempongeza Mhe. Deogratius John Ndejembi kwa kuaminiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu ya CCM na kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dkt. Mwigulu ameitumia nafasi hiyo pia kumpongeza Rais Samia kwa kile alichokiita uwezo wa kumuona Ndejembi na kutambua sifa zake za uongozi, akieleza kuwa kiongozi huyo anazo sifa zinazomfanya astahili kupewa dhamana hiyo kubwa ya kitaifa.

Akizungumza leo Alhamisi, Agosti 27, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu amesema Ndejembi ni kiongozi mahiri, makini na mchapakazi anayefanya kazi bila kuchoka kwa ajili ya kuhakikisha Watanzania wanapata manufaa.

"Mhe. Spika, Deogratius Ndejembi k**a kiongozi ni kiongozi mahiri sana, ni kiongozi makini, kiongozi mchapakazi anayefanya kazi bila kuchoka ili Watanzania waweze kupata manufaa." Amesema Dkt. Mwigulu.

Waziri Mkuu amesema pamoja na uwezo wa kufanya kazi, Ndejembi pia ana sifa za unyenyekevu na upole, akimtaja kuwa mtu rahimu na asiye na hiana ndani yake.

Kwa upande mwingine, Dkt. Mwigulu amemhakikishia Ndejembi kuwa yeye pamoja na mawaziri wenzake wako tayari kushirikiana naye katika kutekeleza majukumu yake mapya, ikiwa ni pamoja na kupokea na kutekeleza maelekezo yatakayosaidia kufanikisha maagizo ya Rais Samia katika kuijenga Tanzania.

Kauli hiyo ya Waziri Mkuu inaweka wazi kuwa uteuzi wa Ndejembi haukuangalia nafasi pekee, bali ulizingatia pia sifa za kiuongozi ambazo amekuwa akizionesha katika utekelezaji wa majukumu yake.

CCM DIASPORA TAWI LA CHAMA CHA MAPINDUZI ITALY PONGEZI ZA UTEUZI WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA T...
27/08/2026

CCM DIASPORA
TAWI LA CHAMA CHA MAPINDUZI ITALY PONGEZI ZA UTEUZI WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Indirizzo

Casalnuovo Di Napoli

Notifiche

Lasciando la tua email puoi essere il primo a sapere quando Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy pubblica notizie e promozioni. Il tuo indirizzo email non verrà utilizzato per nessun altro scopo e potrai annullare l'iscrizione in qualsiasi momento.

Scelte rapide

Condividi