17/10/2024
Ashuwei ni mji unaopatikana katika eneo la kiunga katika wilaya ya lamu. Inakadiriwa kuwa maeneo haya yote wakaazi wao ni takriban 8000, kulingana na utafiti katika miaka ya tisaini(90s).Upande wa mashariki wa mji wa ashuwei kunapatikana bahari iliyo na takriban kilomita mia kaskazini kuna patikana mpaka wa somalia, magharibi na k**ini kunapatika inchi kavu(bara) iliyo na msitu wa pori, hivo wakaazi wa sehemu hizo walifaidika kwa wanyama wa mwituni k**a nyati, paa na wengine.Wakaazi wa sehemu hii wanatambulika kuwa ni watu wa waliyokuwa na mazingira ya ukulima wa hali ya juu, na uvuvi wa samaki.Ukulima ulikuwa ukifanywa kwenye nyakati za siku za k**i, na uvuvi ulikuwa unafanyika sanaa baadabya jua la masika.Sehemu ya ashuwei inapatikana mvu nyingi sana kutoka mwezi wa nne hadi wa tano na mvua katika kipindi cha mwezi wa kumi hafi mwanzo wa mwezi wakumi na mbili.Neema hii imekuwa kwa takriban miaka mingi na watu walikuwa hawana uhaba wa chakula pia. Inasemekana yoyote alokuwa ameajiriwa na mtu ashuwei wakati wa kuenda kwao alikuwa akipewa mazao yabtakriban mwaka mzima.Inasemekana sehemu hii hakujawahi kukosekana maji, hii ni kutokana na mvua ilokuwa ikinyesha kwa uzuri sana na pia maji yalokuwa kwenye visima yalisawazika kuwa k**a maji ya mvua.Kwa kizungu walijulikana k**a 'militant raiders of somali origin'. Kutokana na uvamizi wa kila mara iliwabidi wakaazi wa mjii huu kuhamia sehemu za miji iliyo karibiana.Baadhi ya ukulima wazee walokuwa wakilima na kuvunwa yalikuwa uguta, mtama, tikitiki, mahindi, peas, maharagwe, malenge. Katika hii mimea ufuta ulikuwa ukivunwa kwa wingi sana.Maisha ya wa kaazi wa ashuwei yaliingia katika babaiko la kutokuwa na usalama kutokana na uvamizi uliokiwa ikifanywa na waasi wa kisomale wanaojulikana k**a 'shifta'. Kuna wanao sema watu walikimbilia sehemu inayojulikana k**a "uso wa tavau" hapo kuna mila. Walikaa kwa mda nakuelekea sehemu za visiwani.Visiwa k**a ndau, rasini, mbwajumwali, mtangawanda na wengine walihamia malindi,Mombasa na wengine kukimbilia inchi za ng'ambo.Kutokana na usalama na utulivu walioupata katika miji waluohamia wakaazi wa ashuwei walikuja na fikra za kutaka kurudi katika ardh zao za jadi ili zumilikibsehemu za wazazi wao.Fikra iliundwa katika mwakanwa 1998 na wazee wakiwemo mzee mjahid suo, mzee suo,Ali shemaka na shemaka sizi, mohamed sizi, bahero adi, mwalimu shamu, bahero omar(Almaghufur biidhin llah). Fikra hii pia alikuwa ndugu sizi shemaka(Almaghufur biidhin llah).Vikao vya fikra hii vilikuwa vikifanywa kwa mwalimu shamu akiwa ndie kiongozi wao.Safari ilipangwa wakati huo na wazee wakaenda sehemu zao mzuri wakia na azma ya kuzirudisha kwenye umiliki wa watu wa ashuwei.Wazee waliopoenda walikuwa na azma moja, ardhi ya ashuwei iwe ni community land kwa kila mtu ambae ana asli ya ashuwei aweze kufaidika na ardhi hii iliyojaa neema.Mashallahnwazee walipambana na vizuizi vingi katika safarii hii lakini fikra yao haikuwa mwisho, baadhi ya wavamizi kutoka familia zenye nguvu waliwahai kuziregesha ardhi na title zao kuwa revoked yaani kubatilishwa.Wazee wengingi walienda mbele ya mungu ikiwa walobakia wameishiwa na nguvu.. Leo fikra hii iko mikononi sote vijana... Na tukaamua tuendeleze ukombozi wa ardhi yetu...
Send a message to learn more