02/06/2026
Millioni 57 za wawezesha kikundi cha Vijana Sokoni kujiajiri.
Halmashauri ya Mji Babati kupitia mikopo ya 10% isiyo na riba ya Vijana, Wanawake na wenye Ulemavu inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri imewezesha kikundi cha Vijana sokoni kununua pikipiki za magurudumu matatu (Bajaji) tano na kujiajiri kupitia shughuli za usafirishaji.
Naye Bw.Samweli Paulo Mwenyekiti wa kikundi hicho ameeleza kuwa wamenufaika k**a kikundi lakini pia mtu mmoja mmoja kwa kujipatia kipato na kukidhi mahitaji yao ya kila siku.
Aidha ameongeza kuwa hali ya maisha imekuwa bora ukilinganisha na kipindi cha awali.
Halmashauri ya Mji Babati imeendelea kutenga 10% ya mapato yake ya ndani ili kuwezesha makundi hayo kiuchumi na kufikia adhma ya Serikali ya kuwezesha Vijana kujiajiri.