Babati Town Council

Babati Town Council P. O BOX 383 BABATI

"Tunawajibu wa kutafsiri matarajio ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo"....
04/09/2026

"Tunawajibu wa kutafsiri matarajio ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo".RC Shigela

Ameyasema hayo leo Septemba 4,2026 Mkoani Manyara baada ya kupokea Hati ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkoa wa Manyara kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Sendiga ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Aidha amewataka Viongozi wa ngazi zote kujipanga kukabiliana na mabadiliko ya tabia Nchi kufuatia tahadhari iliyotolewa na mamlaka ya Hali ya hewa Tanzani (TMA) kuhusu uwepo wa mvua za Elnino Oktoba 2026.

Kwa upande wake Mhe.Queen Sendiga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ameeleza kuwa Mkoa wa Manyara ni salama,pia amewataka Watumishi na Watendaji wa Mkoa wa Manyara kutoa ushirikiano kwa kiongozi huyo ili aweze kutimiza majukumu yake kikamilifu.

"Mkoa wa manyara umekuwa Chuo kwangu umenifundisha vitu vingi, nawakaribisha sana Morogoro",nimefurahi kukabidhi Mkoa wa Manyara kwa Mhe. Martine Shigela nakutakia majukumu mema". ameeleza

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Manyara Rs Shaaban Mpendu Msemaji Mkuu wa Serikali Maelezo News Ikulu Tanzania

"Tuna wajibu wa kutafsiri matarajio ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo"...
04/09/2026

"Tuna wajibu wa kutafsiri matarajio ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo".RC Shigela

Ameyasema hayo leo Septemba 4,2026 Mkoani Manyara baada ya kupokea Hati ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkoa wa Manyara kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Sendiga ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Aidha amewataka Viongozi wa ngazi zote kujipanga kukabiliana na mabadiliko ya tabia Nchi kufuatia tahadhari iliyotolewa na mamlaka ya Hali ya hewa Tanzani (TMA) kuhusu uwepo wa mvua za Elnino Oktoba 2026.

Kwa upande wake Mhe.Queen Sendiga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ameeleza kuwa Mkoa wa Manyara ni salama,pia amewataka Watumishi na Watendaji wa Mkoa wa Manyara kutoa ushirikiano kwa kiongozi huyo ili aweze kutimiza majukumu yake kikamilifu.

"Mkoa wa manyara umekuwa Chuo kwangu umenifundisha vitu vingi, nawakaribisha sana Morogoro",nimefurahi kukabidhi Mkoa wa Manyara kwa Mhe. Martine Shigela nakutakia majukumu mema". ameeleza

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI Manyara Rs OFISI YA WAZIRI MKUU Shaaban Mpendu Maelezo News@msemajimkuuwaserikali Ikulu Tanzania

Habari Picha:  Watumishi wa Halmashauri ya Mji Babati wakipewa mafunzo juu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Bw...
04/09/2026

Habari Picha: Watumishi wa Halmashauri ya Mji Babati wakipewa mafunzo juu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Bw.Tumaini Mgala
Afisa mfuko wa fidia kwa Wafanyakazi katika Ukumbi wa Halmashauri.

OFISI YA WAZIRI MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI Manyara Rs Shaaban Mpendu Msemaji Mkuu wa Serikali Maelezo News Workers Compensation Fund (WCF)

Wamiliki wa Asasi za Kiraia wametakiwa kushirikisha Serikali Mipango ya miradi kabla ya utekelezaji.Rai hiyo imetolewa n...
02/09/2026

Wamiliki wa Asasi za Kiraia wametakiwa kushirikisha Serikali Mipango ya miradi kabla ya utekelezaji.

Rai hiyo imetolewa na Mhe.Remidius Mwema Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Babati katika Jukwaa la mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Wilayani Babati lililofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

Mhe. Mwema amesema kuwa ni muhimu Asasi za Kiraia kuwasilisha mapema mipango ya utekelezaji wa miradi kwa Serikali ili kupunguza utekelezaji wa Miradi inayofanana katika jamii lakini pia Jamii iweze kutambua thamani ya Miradi hiyo.

"Serikali ipo tayari kufanya kazi na kutoa ushirikiano kwa Mashirika yanayofanya kazi vizuri,Mashirika yanayofanya kazi vizuri yapongezwe jambo hilo liwe endelevu,"ameeleza.

Aidha ametoa wito kwa waandaaji wa Jukwaa hilo Kuandaa jukwaa maalumu litakalo kutanisha Asasi zote za kiraia kwa ajili ya kuwasilisha na kuonesha utekelezaji wa Shughuli za miradi yao katika jamii.

"Wasilisheni taarifa za utekelezaji wa miradi kwa Viongozi, Fedha zilizopokelewa na gharama zilizotumika katika utekelezaji wa miradi kwa uwazi, Ameongeza.

Jukwaa la mwaka la mashirika yasiyo ya Kiserikali 2026 lenye Kauli mbiu "Fikra mpya kuhusu uendelevu wa Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali:Ubunifu,Ubia na upatikanaji wa Rasilimali Fedha kupitia Vyanzo vya ndani(Re imaging NGO'S Sustainability Innovation Pertnership And Home Growth Financing Solutions ni muhimu kwa kuwa limewakutanisha Wadau wa Maendeleo kujadili utekelezaji na namna ya kutatua changamoto.

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI Manyara Rs Shaaban Mpendu Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali Remidius Mwema Ikulu Tanzania

HONGERA SANA MHE.DEOGRATIUS JOHN NDEJEMBI .OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Shaaban Mpendu Manyara Rs ...
30/08/2026

HONGERA SANA MHE.DEOGRATIUS JOHN NDEJEMBI .

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Shaaban Mpendu Manyara Rs Msemaji Mkuu wa Serikali Maelezo News Ikulu Tanzania

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.AMINA.🙏APUMZIKE KWA AMANI.OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI Manyara R...
30/08/2026

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.AMINA.🙏

APUMZIKE KWA AMANI.

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI Manyara Rs Shaaban Mpendu Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Tanzania Maelezo News

MWISHO NI LEO HAKIKISHA MTOTO MWENYE UMRI CHINI YA MIAKA 10 ANAPATA CHANJO YA POLIO YA MATONE."MPE CHANJO,ZUIA POLIO".OF...
30/08/2026

MWISHO NI LEO HAKIKISHA MTOTO MWENYE UMRI CHINI YA MIAKA 10 ANAPATA CHANJO YA POLIO YA MATONE.

"MPE CHANJO,ZUIA POLIO".

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI
OFISI YA WAZIRI MKUU
Manyara Rs Shaaban Mpendu Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Tanzania Manyara Rrh Wizara Ya Afya

KAMPENI YA CHANJO YA POLIO YA MATONE INAENDELEA WALENGWA NI WATOTO WOTE WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 10.CHANJO YA POLIO YA ...
29/08/2026

KAMPENI YA CHANJO YA POLIO YA MATONE INAENDELEA WALENGWA NI WATOTO WOTE WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 10.

CHANJO YA POLIO YA MATONE INATOLEWA KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA,SOKONI,SHULENI,NYUMBA KWA NYUMBA NA MAENEO YENYE MIKUSANYIKO YA WATU.

EWE MZAZI/MLEZI HAKIKISHA MTOTO WAKO ANAPATA CHANJO YA POLIO YA MATONE ILI KUMKINGA MTOTO NA UGONJWA WA POLIO.

"MPE CHANJO,ZUIA POLIO"

"TUNZA MAZINGIRA YAKUTUNZE".OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Shaaban Mpendu Manyara Rs Ikulu Tanzania ...
28/08/2026

"TUNZA MAZINGIRA YAKUTUNZE".

OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Shaaban Mpendu Manyara Rs Ikulu Tanzania Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali

DC MWEMA AZINDUA RASMI KAMPENI YA CHANJO YA POLIO YA MATONE NGAZI YA WILAYA BABATI MJI.Mhe.Remidius Mwema Emmanuel Kaimu...
28/08/2026

DC MWEMA AZINDUA RASMI KAMPENI YA CHANJO YA POLIO YA MATONE NGAZI YA WILAYA BABATI MJI.

Mhe.Remidius Mwema Emmanuel Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Babati amezindua rasmi zoezi la utoaji Chanjo ya Polio ya Matone kwa Watoto walio na umri chini ya miaka 10 katika Shule ya Msingi Maisaka.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mhe.Mwema amewataka Viongozi wa Dini na Serikali ngazi zote kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha Watoto wote walengwa wanapatiwa Chanjo hiyo ya Polio ya Matone ili kuweza kuwalinda na Ugonjwa wa Polio.

Aidha ameongeza kuwa Wazazi/Walezi wanatakiwa kuhakikisha wanawapeleka Watoto kupata Chanjo hiyo ili waweze kufikia malengo yao wakiwa na Afya Njema.

Vilevile amesema kuwa ushirikiano wa Viongozi,Wataalam wa Afya,Wazazi na Walezi ni muhimu ili kuhakikisha hakuna mtoto yeyote atakayekosa Chanjo ya Polio ya Matone haswa kwa wale Wageni wanokuja na kutoka sehemu nyingine.

Dkt.Nassib Msuya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Babati amesema zoezi la utoaji wa Chanjo ya Polio ya Matone linaendelea katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa Babati,ikiwa na lengo la kuwafikia Watoto 38,249.
OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI OFISI YA WAZIRI MKUU Manyara Rs Shaaban Mpendu Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Tanzania Wizara Ya Afya Manyara Rrh

Address

Town Director's Office, Babati Town Council, 1 Council Street, Bagara Manyara
Babati
27103

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Babati Town Council posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Babati Town Council:

Shortcuts

Share