24/05/2026
MICHEZO NI CHACHU YA MSHIKAMANO NA AFYA KWA WATUMISHI BUKOBA RRH
Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba wametakiwa kuendeleza utamaduni wa kushiriki michezo k**a njia ya kuimarisha afya, kuimarisha mshik**ano kazini na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi.
Wito huo umetolewa na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Museleta Nyakiroto, wakati akifungua rasmi michezo mbalimbali iliyojulikana k**a “BUKOBA RRH GET TOGETHER BONANZA”, yenye lengo la kuwakutanisha watumishi wa kada tofauti katika mazingira ya urafiki na burudani.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Nyakiroto alisema michezo ni chachu muhimu ya mshik**ano, kwani huwapa watumishi fursa ya kujenga mahusiano mazuri nje ya majukumu ya kazi, kupunguza msongo wa mawazo na kuchochea afya njema ya mwili na akili. Aliongeza kuwa mshik**ano kazini huongeza ushirikiano, mawasiliano bora na hatimaye kuboresha huduma kwa wagonjwa.
“Mazingira ya kazi yenye afya yanahitaji watumishi wenye afya ya mwili na akili. Michezo hutuwezesha kufurahia kazi, kuimarisha umoja na kuongeza ari ya kuwahudumia wananchi,” alisema Dkt. Nyakiroto.
Michezo iliyoshirikiwa katika bonanza hilo ilijumuisha kukimbiza kuku, kuvuta kamba, utambuzi wa rangi, utambuzi wa ladha ya vinywaji pamoja na mechi ya mpira wa miguu kati ya mashabiki wa klabu za Yanga na Simba, ambapo shangwe na burudani vilitawala uwanja.