Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake Pemba

Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake Pemba Karibu katika ukurasa rasmi wa Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake.

Ukurasa huu unatoa taarifa kuhusu maendeleo ya michezo, mashindano, vipaji, matukio na shughuli mbalimbali za michezo zinazofanyika Wilayani Chake Chake

πŸ“ TABLE TENNIS DEVELOPMENT PROGRAM – WETE DISTRICT πŸ†Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake kwa kushirikiana na Zanzibar ...
17/08/2026

πŸ“ TABLE TENNIS DEVELOPMENT PROGRAM – WETE DISTRICT πŸ†

Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake kwa kushirikiana na Zanzibar Table Tennis Association (ZTTA) inaendelea na juhudi za kuendeleza na kuutangaza mchezo wa mpira wa meza (Table Tennis) katika Wilaya ya Wete.

Katika kuendeleza mpango huu, Semina ya Table Tennis Development Program inatarajiwa kufanyika:

πŸ“… Jumamosi, 22 Agosti 2026
⏰ Saa 2:00 asubuhi (8:00 AM)
πŸ“ Chasasa Secondary School – Wete

🎯 Malengo ya programu ni pamoja na:
βœ… Kuendeleza ujuzi wa mchezo wa Table Tennis
βœ… Kubaini na kukuza vipaji vya vijana
βœ… Kuimarisha utimamu wa mwili
βœ… Kujenga nidhamu na ushirikiano miongoni mwa vijana
βœ… Kuwapa vijana fursa ya mashindano na uzoefu wa kiushindani

πŸ‘¦πŸ½πŸ‘§πŸ½ Wavulana na wasichana kutoka shule teula watapatiwa mafunzo juu ya mchezo wa mpira wa meza.

🀝 Tushirikiane kuijenga kesho ya Table Tennis katika Wilaya ya Wete!

BUILDING SKILLS. BUILDING CHARACTER. BUILDING CHAMPIONS. πŸ“πŸ†

FINALI YA VOLLEYBALL PEMBA KUCHEZWA LEO!!!Afisi ya michezo wilaya ya chake chake Pemba ikishirikiana na Shirikisho la Mp...
16/08/2026

FINALI YA VOLLEYBALL PEMBA KUCHEZWA LEO!!!

Afisi ya michezo wilaya ya chake chake Pemba ikishirikiana na Shirikisho la Mpira wa Wavu Zanzibar (ZVF) wameandaa mchezo wa finali ya Pemba, utakaizikutanisha Team mbili kubwa kutoka hapa visiwani Pemba.

muda: saa 10 jioni
sehemu: uwanja wa Tennis Chake chake

Wananchi wote mnaalikwa kushuhudia mtanange huo.

Karibuni sana.

MICHEZO KWA MAENDELEO YA TAIFA

🏐πŸ”₯ **FINALI YA VOLLEYBALL YA PEMBA – NI JUMAPILI HII!** πŸ”₯🏐Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake kwa kushirikiana na Zan...
11/08/2026

🏐πŸ”₯ **FINALI YA VOLLEYBALL YA PEMBA – NI JUMAPILI HII!** πŸ”₯🏐

Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake kwa kushirikiana na Zanzibar Volleyball Federation (ZVF) inawakaribisha wananchi, wapenzi wa michezo na wadau wote wa michezo kushuhudia mchezo mkubwa wa fainali ya Volleyball ya Pemba.

πŸ† MADUNGU WARRIORS πŸ†š WETE STARS πŸ†

Mchezo huu ni sehemu ya kuimarisha mashirikiano, umoja na maendeleo ya mchezo wa Volleyball, pamoja na kuendelea kujenga mazingira bora ya michezo kwa vijana na jamii kwa ujumla.

πŸ“… Jumapili, 16/08/2026
⏰ Saa 10:00 za Jioni
πŸ“ Uwanja wa Tennis Chake Chake

Karibu tushuhudie burudani, ushindani na vipaji vya hali ya juu.
🀝 Michezo kwa Afya, Maendeleo na Umoja.







πŸ“ ELIMU BILA YA MALIPO KUELEKEA TAIFA 2026 πŸ“Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kwa kushirikiana na Afisi ya Michezo Wi...
06/08/2026

πŸ“ ELIMU BILA YA MALIPO KUELEKEA TAIFA 2026 πŸ“

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kwa kushirikiana na Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake – Pemba na Chama cha Mpira wa Meza Zanzibar (ZTTA), inawakaribisha wananchi, wadau wa michezo na wapenda elimu kushuhudia mashindano ELIMU BILA YA MALIPO 2026, yatakayotumika k**a mchujo wa kupata wawakilishi wa Pemba kuelekea mashindano ya kitaifa.

Mashindano haya yanalenga kuibua, kuendeleza na kukuza vipaji vya wanafunzi katika mchezo wa mpira wa meza, sambamba na kuhamasisha ushiriki wa michezo shuleni k**a sehemu ya malezi, afya na maendeleo ya vijana.

πŸ“… Tarehe: Jumamosi, 08 Agosti 2026
πŸ•’ Muda: Saa 2:30 Asubuhi
πŸ“ Mahali: Michakaini Primary School, Pemba

Mgeni Rasmi atakuwa Rajab A. Mkumbaru, Meneja wa TAWI PBZ Bank – Pemba.

Kauli mbiu: "Mpira wa Meza ni Fursa."

Tunawakaribisha wazazi, walimu, wanafunzi na wadau wote wa michezo kuja kuwaunga mkono vijana wetu katika safari ya kutafuta mabingwa watakaoiwakilisha Pemba kwenye mashindano ya kitaifa.

πŸ† AFISA WA MICHEZO WILAYA YA CHAKE CHAKE AHUDHURIA MCHUJO WA ELIMU BILA MALIPO NGAZI YA TAIFALeo nimepata fursa, nikiwa ...
01/08/2026

πŸ† AFISA WA MICHEZO WILAYA YA CHAKE CHAKE AHUDHURIA MCHUJO WA ELIMU BILA MALIPO NGAZI YA TAIFA

Leo nimepata fursa, nikiwa katika nafasi yangu k**a Afisa Michezo wa Wilaya ya Chake Chake, kuhudhuria mashindano ya Mchujo wa Elimu Bila ya Malipo Ngazi ya Taifa, yaliyowakutanisha jumla ya timu 8 kutoka ngazi ya Shule za Msingi na Sekondari.

Mashindano haya yameonesha kiwango kizuri cha vipaji, ushindani na nidhamu miongoni mwa wanafunzi, jambo linalodhihirisha umuhimu wa michezo katika kujenga afya, kuibua vipaji na kukuza maendeleo ya vijana wetu.

Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake itaendelea kushirikiana kwa karibu na Idara ya Michezo na Utamaduni WEMA pamoja na wadau wengine kuhakikisha michezo inaendelea kupewa kipaumbele katika shule na jamii kwa ujumla. Ushirikiano huu ni sehemu ya jitihada za kukuza na kuendeleza michezo, kuibua vipaji na kuwajengea vijana fursa za kufikia mafanikio kupitia michezo.

Tunawatakia kila la heri washiriki wote na tunatoa pongezi kwa waandaaji kwa maandalizi mazuri ya mashindano haya.

πŸ… Michezo ni afya, nidhamu na msingi wa maendeleo ya taifa.

🀝 KUIMARISHA MASHIRIKIANO KWA AJILI YA MAENDELEO YA MICHEZO WILAYA YA CHAKE CHAKELeo nilipata fursa ya kukutana na uongo...
27/07/2026

🀝 KUIMARISHA MASHIRIKIANO KWA AJILI YA MAENDELEO YA MICHEZO WILAYA YA CHAKE CHAKE

Leo nilipata fursa ya kukutana na uongozi wa Kitengo cha Kuzuia na Kudhibiti Maambukizi ya Kichocho Pemba, kinachotekeleza shughuli zake kwa ushirikiano na China Aid, kwa lengo la kufanya mazungumzo ya kujenga ushirikiano wa kikazi kati ya kitengo hicho na Afisi ya Afisa Michezo Wilaya ya Chake Chake.

Mazungumzo yetu yalijikita katika kutafuta fursa za ushirikiano zitakazochangia kuimarisha afya ya jamii kupitia michezo, pamoja na kukuza na kuendeleza sekta ya michezo katika Wilaya ya Chake Chake.

Ninashukuru kwa mapokezi mazuri na mazungumzo yenye mafanikio yaliyofanyika. Tuna imani kuwa ushirikiano huu utazaa matokeo chanya na kufungua fursa mbalimbali zitakazonufaisha vijana, wanamichezo na jamii kwa ujumla.

Afisi ya Afisa Michezo Wilaya ya Chake Chake itaendelea kujenga ushirikiano na taasisi mbalimbali kwa lengo la kuendeleza michezo, kuimarisha afya ya jamii na kuleta maendeleo endelevu katika wilaya yetu.

22/07/2026

πŸ“ UFUNGUZI WA PROGRAMU YA MAENDELEO YA MPIRA WA MEZA πŸ“

Tarehe 5 July 2026, tulifanikiwa kuzindua rasmi Programu ya Maendeleo ya Mpira wa Meza katika FIDEL CASTRO SECONDARY SCHOOL, ikiwa ni hatua muhimu ya kuendeleza vipaji vya wanafunzi na kuwajengea msingi wa afya, nidhamu na ushindani.

Programu hii imeandaliwa kwa ushirikiano wa Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake na Zanzibar Table Tennis Association, kwa lengo la kuibua vipaji na kutoa fursa kwa vijana kushiriki katika mashindano ya kitaifa na kimataifa.

Tunawashukuru walimu, wanafunzi, viongozi na wadau wote waliojitokeza kuunga mkono uzinduzi huu.

πŸ“ Kauli Mbiu: "Mpira wa Meza ni Fursa."

πŸ“ž Mawasiliano: +255 623 973 635
πŸ“§ Email: [[email protected]]

πŸ€ KILA LA KHERI TEAM PEMBA! πŸ€Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake, leo Afisi ya Afisa Michezo Wilaya ya Chake Chak...
21/07/2026

πŸ€ KILA LA KHERI TEAM PEMBA! πŸ€

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake, leo Afisi ya Afisa Michezo Wilaya ya Chake Chake imeiaga rasmi Timu ya Mpira wa Kikapu ya Pemba (Team Pemba) inayokwenda kuiwakilisha Pemba katika mashindano ya CRDB Bank Taifa Cup 2026, yatakayofanyika jijini Dodoma kuanzia tarehe 21 Julai hadi 1 Agosti 2026.

Jumla ya wachezaji 12 wa kiume pamoja na viongozi 5, wamesafiri mchana wa leo kulekea Dodoma kwa ajili ya kushiriki mashindano hayo huku wakiwa na matumaini makubwa ya kufanya vizuri.

Tunaondoka na matumaini makubwa kwamba vijana wetu wataonesha nidhamu, mshik**ano, uzalendo na kiwango cha juu cha mchezo, wakiipeperusha vyema bendera ya Pemba katika mashindano hayo ya kitaifa.

Tunatoa pongezi kwa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi wa timu pamoja na wadau wote waliochangia maandalizi ya safari hii. Jitihada zenu ni sehemu muhimu ya maendeleo ya mchezo wa mpira wa kikapu na michezo kwa ujumla visiwani Pemba.

Team Pemba, nendeni mkaiwakilishe Pemba kwa heshima na ari kubwa. Piganeni kwa moyo mmoja, chezeni kwa nidhamu, na mrudi na ushindi.

Afisi ya Afisa Michezo Wilaya ya Chake Chake inawatakia safari njema, afya njema na mafanikio makubwa katika mashindano yote.

πŸ† Kila la Kheri Team Pemba!
πŸ€ Pemba Kwanza, Ushindi Kwanza!**
πŸ’š Dodoma tunakuja!
**

πŸ“ MAFUNZO YA KUENDELEZA MCHEZO WA TABLE TENNIS – MITIULAYA SECONDARY SCHOOLKwa lengo la kuibua, kukuza na kuendeleza vip...
18/07/2026

πŸ“ MAFUNZO YA KUENDELEZA MCHEZO WA TABLE TENNIS – MITIULAYA SECONDARY SCHOOL

Kwa lengo la kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya mchezo wa Table Tennis kwa vijana, Chama cha Mchezo wa Table Tennis Zanzibar (ZTTA) kilishirikiana na Afisi ya michezo wilaya ya chake chake, leo kimeendesha mafunzo ya utangulizi katika Shule ya Sekondari Mitiulaya.

Jumla ya wanafunzi 19 walipata fursa ya kushiriki mafunzo hayo, wakiwemo wasichana 6 na wavulana 13. Washiriki walipata elimu ya msingi kuhusu mchezo wa Table Tennis pamoja na umuhimu wake katika kujenga afya, nidhamu, kujiamini na kuibua vipaji vya michezo.

Aidha, kabla ya kuanza kwa mafunzo haya, mazungumzo ya awali yalifanyika katika Shule ya Sekondari Chasasa na Shule ya Sekondari Utaani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupeleka programu hii ya maendeleo ya mchezo wa Table Tennis katika shule hizo.

Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa shule, walimu, wanafunzi na wadau wote walioshiriki kufanikisha programu hii. Kwa pamoja tunaendelea kujenga msingi imara wa kuibua vipaji vipya na kuendeleza mchezo wa Table Tennis Zanzibar.

πŸ“ Leo tunafundisha mchezo, kesho tunazalisha mabingwa!

MADUNGU SECONDARY SCHOOL TABLE TENNIS DEVELOPMENT PROGRAM KUZINDULIWA RASMI!Leo Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake i...
13/07/2026

MADUNGU SECONDARY SCHOOL TABLE TENNIS DEVELOPMENT PROGRAM KUZINDULIWA RASMI!

Leo Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake imezindua rasmi Programu ya Maendeleo ya Mpira wa Meza (Table Tennis Development Program) katika Skuli ya Madungu Secondary ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendeleza michezo shuleni na kuibua vipaji vipya vya vijana.
Programu hii inalenga kuwahamasisha wanafunzi kushiriki katika mchezo wa mpira wa meza, kuwajengea nidhamu, kuimarisha afya zao, pamoja na kuwapa mafunzo ya msingi na ya kitaalamu yatakayowawezesha kufikia viwango vya juu vya ushindani.
Zaidi ya wanafunzi 40 wanatarajiwa kunufaika na awamu ya kwanza ya mafunzo haya. Aidha, programu hii itapanuliwa katika shule nyingine teule za Wilaya ya Chake Chake ili kuwafikia vijana wengi zaidi wenye vipaji na hamasa ya mchezo wa mpira wa meza.
Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake inaendelea kuamini kuwa uwekezaji katika michezo ya vijana ni uwekezaji katika afya, nidhamu na mustakabali wa jamii yetu.

Tunawashukuru uongozi wa Madungu Secondary School, walimu na wanafunzi wote kwa ushirikiano wao katika kufanikisha uzinduzi wa programu hii.
"Kujenga Vipaji vya Leo, Mabingwa wa Kesho." πŸ“πŸ’ͺ

Address

MKUU WA WILAYA OFFICE
Chake Chake
7100

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afisi ya Michezo Wilaya ya Chake Chake Pemba posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share