18/07/2026
π MAFUNZO YA KUENDELEZA MCHEZO WA TABLE TENNIS β MITIULAYA SECONDARY SCHOOL
Kwa lengo la kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya mchezo wa Table Tennis kwa vijana, Chama cha Mchezo wa Table Tennis Zanzibar (ZTTA) kilishirikiana na Afisi ya michezo wilaya ya chake chake, leo kimeendesha mafunzo ya utangulizi katika Shule ya Sekondari Mitiulaya.
Jumla ya wanafunzi 19 walipata fursa ya kushiriki mafunzo hayo, wakiwemo wasichana 6 na wavulana 13. Washiriki walipata elimu ya msingi kuhusu mchezo wa Table Tennis pamoja na umuhimu wake katika kujenga afya, nidhamu, kujiamini na kuibua vipaji vya michezo.
Aidha, kabla ya kuanza kwa mafunzo haya, mazungumzo ya awali yalifanyika katika Shule ya Sekondari Chasasa na Shule ya Sekondari Utaani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupeleka programu hii ya maendeleo ya mchezo wa Table Tennis katika shule hizo.
Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa shule, walimu, wanafunzi na wadau wote walioshiriki kufanikisha programu hii. Kwa pamoja tunaendelea kujenga msingi imara wa kuibua vipaji vipya na kuendeleza mchezo wa Table Tennis Zanzibar.
π Leo tunafundisha mchezo, kesho tunazalisha mabingwa!