06/05/2026
๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Tanga- Mei 6, 2026
Mkataba wa umaliziaji wa awamu ya kwanza ya jujenzi wa jengo la Kampasi ya Tanga umesainiwa leo jijini Tanga, kati ya mkandarasi M/s Intergo Company Limited na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kwa gharama ya TZS 3.778 bilioni.
Mkataba umesainiwa kwa niaba ya TPSC na Mkurugenzi wa Kampasi ya Tanga, Bi. Zawadi Rashidi, na kwa niaba ya mkandarasi na Mkurugenzi wa Intergo Company Limited, Bw. Gulam Abdul. Kwa upande wa mshauri elekezi, M/s Wakala wa Majengo (TBA), mkataba ulisainiwa na Kaimu Meneja wa TBA mkoa wa Tanga, Bw. Justo Lyatuu.
Utiaji saini umefanyika mbele ya Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho.
Akizungumza baada ya kusaini mkataba, Dkt. Ernest Mabonesho amesema kuwa ukaguzi wa mara kwa mara kuhakikisha mkataba unatekelezwa kikamilifu na kwa ubora.
"Mkandarasi anatakiwa kuzingatia ubora wa kazi k**a ilivyoainishwa kwenye mkataba na kuhakikisha kukamilisha kazi ndani ya wakati uliokubaliwa" amesisitiza Dkt. Mabonesho
Utekelezaji wa mkataba unatarajiwa kuchukua mwaka mmoja (siku 365) na ukamilishaji wake unatarajiwa kufanyika kwa wakati ili jengo lianze kutumika.
Mradi unalenga kukamilisha jengo lenye madarasa 26 zitakazohudumia zaidi ya wanafunzi 2,500 kwa awamu moja, ofisi 24 za watumishi, kumbi mbili za mikutano na vyoo vya kisasa 18.