Baraza la Michezo la Taifa

Baraza la Michezo la Taifa Baraza la Michezo la Taifa (BMT)
"Michezo ni Afya, Michezo ni Ajira"

12/06/2026

Makonda: Kombe la Dunia 2026 kutupa Dira ya Kuandaa na Kusimamia AFCON 2027

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema anatarajia kujifunza namna mashindano makubwa duniani yanavyoandaliwa na kusimamiwa kupitia ushiriki wake kwenye mechi za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Mexico.

Amesema hayo Juni 11, 2026, wakati akizungumza kwa njia ya simu akiwa Mexico kushuhudia michuano hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino, na kubainisha kuwa, ushiriki wake ni fursa ya kujionea kwa karibu namna mashindano makubwa ya kimataifa yanavyoandaliwa na kusimamiwa.

Mwaka 2027 Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano makubwa ya AFCON, hivyo uzoefu kutoka Kombe la Dunia 2026 utatumika kuboresha mashindano hayo na sekta ya michezo hapa nchini.

RUKWA, DODOMA NA IRINGA ZANG'ARA GOALBALL UMITASHUMTA 2026Mashindano ya Goalball katika UMITASHUMTA 2026 yameendelea kus...
10/06/2026

RUKWA, DODOMA NA IRINGA ZANG'ARA GOALBALL UMITASHUMTA 2026

Mashindano ya Goalball katika UMITASHUMTA 2026 yameendelea kushika kasi mkoani Iringa huku timu za Rukwa, Dodoma na wenyeji Iringa zikionyesha ubabe katika michezo ya hatua za makundi iliyochezwa leo Juni 10, 2026.

Katika mchezo uliovutia mashabiki wengi, Rukwa iliibuka na ushindi wa mabao 7-3 dhidi ya Lindi kwenye mchezo wa wavulana uliochezwa katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Lugalo, Manispaa ya Iringa. Kabla ya mchezo huo, Simiyu na Ruvuma zilitoshana nguvu kwa kutoka sare ya mabao 6-6.

Matokeo mengine ya wavulana yalishuhudia Dodoma ikiichapa Morogoro mabao 13-5, Rukwa ikiifunga Tanga mabao 10-5, huku Iringa ikiwafurahisha mashabiki wake kwa ushindi mnono wa mabao 11-1 dhidi ya Dar es Salaam.

Kwa upande wa wasichana, Kigoma iliibuka na ushindi wa mabao 8-3 dhidi ya Pwani, Dodoma ikaifunga Njombe mabao 11-1, Kagera ikaizamisha Geita kwa mabao 10-0, na Arusha kuibuka na ushindi wa mabao 8-2 dhidi ya Iringa.

Mashindano hayo yanaendelea katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Lugalo huku timu zikisaka nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali kupitia michezo ya makundi inayoendelea kuchezwa kwa ushindani mkubwa.

Bondia wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo ‘Champez’, anatarajiwa kupanda ulingoni leo Juni 10, 2026 mjini Abidjan...
10/06/2026

Bondia wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo ‘Champez’, anatarajiwa kupanda ulingoni leo Juni 10, 2026 mjini Abidjan, Ivory Coast kumenyana na Michel Soro katika pambano la raundi 12 la uzani wa kati.

Pambano hilo litakuwa la kuwania taji la IBO lililo wazi na ndilo pambano kuu la usiku wa masumbwi wa Dream 1 litakalofanyika katika Ukumbi wa Parc des Expositions.

Mabondia wengine wa Tanzania, Abdul Ubaya na Amiri Matumla, pia watakuwa ulingoni wakiwakabili wapinzani wao kutoka Ulaya.

Tunawatakia kila la heri mabondia wetu katika kuendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa.

SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO NCHINI-PROF.SHEMDOEWaziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mh...
09/06/2026

SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO NCHINI-PROF.SHEMDOE

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha miundombinu ya michezo nchini, ili kuendelea kukuza sekta hiyo.

Prof.Shemdoe amesema hayo leo tarehe 9 Juni 2026 Mjini Iringa, wakati akizungumza katika ufunguzi wa Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA yanayofanyika Kitaifa Mkoani humo.

Amesema kuwa lengo la kuimarisha miundombinu ni kuhakikisha kuwa vipaji vinavyoibuliwa havipotei, na vinaendelezwa kwa ajili ya kuja kulitumikia Taifa kupitia team mbalimbali za ndani na nje ya nchi.

"Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa michezo na Sanaa inapewa kipaumbele katika shule, kwa michezo ni uchumi iwapo itawekeza msingi mzuri" amesisitiza Prof. Shemdoe.

BMT YAIKABIDHI TAMISEMI JEZI ZA MPIRA WA MIGUU KWA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETAAfisa Michezo wa Baraza la Miche...
09/06/2026

BMT YAIKABIDHI TAMISEMI JEZI ZA MPIRA WA MIGUU KWA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA

Afisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Bw. Adam Tunga, amekabidhi jezi za mpira wa miguu kwa ajili ya kutumika katika Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendeleza michezo na kukuza vipaji vya wanafunzi nchini.

Jezi hizo zimepokelewa na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw. Yusuph Singo.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Tunga alisema kuwa lengo la kukabidhizu jezi ni kuimarisha ushiriki wa wanafunzi katika michezo, kukuza vipaji vyao na kuweka mazingira bora yatakayowawezesha kufikia ndoto zao za kuwa wanamichezo wa kiwango cha juu.

Alibainisha kuwa mashindano ya UMITASHUMTA yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kutambua, kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo mashuleni, huku yakichangia pia kujenga nidhamu, afya na uzalendo kwa wanafunzi.

Kwa upande wake, Bw. Singo alilishukuru Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kwa mchango huo, akisema kuwa utasaidia kuongeza hamasa kwa washiriki wa mashindano na kuendelea kuimarisha maendeleo ya michezo nchini.

Aidha, alisema kuwa pamoja na kukuza vipaji vya vijana, mashindano hayo yanatumika k**a sehemu ya maandalizi na uhamasishaji kuelekea mashindano ya AFCON 2027, ambayo yataandaliwa kwa ushirikiano wa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

SERIKALI KUIMARISHA MICHEZO SHULENI ILI KUKUZA VIPAJI NA NIDHAMU KWA WANAFUNZISerikali itaendelea kuimarisha michezo shu...
09/06/2026

SERIKALI KUIMARISHA MICHEZO SHULENI ILI KUKUZA VIPAJI NA NIDHAMU KWA WANAFUNZI

Serikali itaendelea kuimarisha michezo shuleni ambayo ni nyenzo muhimu ya kukuza vipaji, nidhamu, kukuza shughuli za kitaaluma, uzalendo, kuboresha afya pamoja na kujenga umoja wa kitaifa miongoni mwa wanafunzi nchini.

Hayo yameelezwa leo Mjini Iringa na Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wakati akifungua mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) pamoja na Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) ambayo kitaifa mwaka huu yanafanyika Mkoani hapo.

Akizungumza kwa niaba ya Mhe. Mwigulu Mchemba, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alikua mgeni rasmi katika mashindano hayo, Prof. Shemdowe amesema mashindano hayo yameendelea kuwa msingi muhimu wa kutambua na kuendeleza vipaji vya michezo vinavyoisaidia Tanzania kupata wanamichezo bora katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

Amewataka wanafunzi kushiriki mashindano hayo muhimu kwa kuzingatia nidhamu, ushindani wa haki na kuheshimu kanuni za michezo, huku akisisitiza umuhimu wa kuunganisha elimu na michezo kwa maendeleo ya taifa.

Hafla ya ufunguzi wa mashindano hayo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali hususani sekta ya elimu, michezo pamoja na wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.

Prof. Shemdoe Awasili Iringa Kufungua UMITASHUMTA NA UMISSETA 2026Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Mhe. Pr...
09/06/2026

Prof. Shemdoe Awasili Iringa Kufungua UMITASHUMTA NA UMISSETA 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewasili Mkoani Iringa kufungua Mashindano ya michezo kwa Shule za Msingi na Sekondari UMITASHUMTA na UMISSETA 2026, leo tarehe 9 Juni.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Methusela Ntonda na viongozi wengine wameshiriki ufunguzi huo.

09/06/2026

Michezo Yaendelea Kuunganisha Jamii na Kuondoa Dhana Potofu kwa Watu Wenye Ualbino

Nahodha wa Bunge Sports Club, Suleiman Mohammed Rashid, amesema michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuondoa dhana potofu dhidi ya watu wenye ualbino.

Akizungumza baada ya mchezo wa kirafiki kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3 katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Juni 6, 2026, Rashid amesema watu wenye ualbino wana uwezo mkubwa wa kushiriki na kufanya vizuri katika sekta mbalimbali ikiwemo michezo.

Amesisitiza umuhimu wa jamii kuendelea kuwaunga mkono watu wenye ualbino ili kuwapa fursa sawa za kushiriki katika shughuli za maendeleo na michezo kwa manufaa ya taifa

09/06/2026

Katibu Mkuu wa Albinism Sports Club, Joseph Sinda, ametoa wito kwa wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wadau wa maendeleo kujitokeza kuunga mkono mbio ya kimataifa ya Albinism inayotarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza mkoani Mara.

Sinda amesema mbio hizo, zilizoandaliwa kwa ushirikiano wa Tanzania Albinism Society (TAS), Serikali na wadau mbalimbali, zinalenga kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya ualbino, kuibua vipaji vya watu wenye ualbino na kuimarisha ushiriki wao katika michezo na shughuli za kijamii.

Akizungumza baada ya mchezo wa kirafiki uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3 dhidi ya Timu ya Bunge jijini Dodoma Juni 6, 2026, Sinda pia aliishukuru Serikali, TAS na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kupitia Katibu Mtendaji Neema Msita kwa mchango wao katika kuwezesha shughuli mbalimbali za klabu hiyo, ikiwemo usafiri na programu za maendeleo ya michezo kwa watu wenye ualbino nchini.

09/06/2026

Maandalizi ya ufunguzi wa Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA 2026 yanatarajiwa kukamilika leo kuelekea hafla ya ufunguzi itakayofanyika kesho, Juni 9, 2026, katika Viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Mashindano hayo yanawakutanisha wanafunzi kutoka shule mbalimbali nchini kushiriki na kushindana katika michezo tofauti, yakiwa na kaulimbiu isemayo: "Michezo na Sanaa Shuleni, Daraja la Ajira, Afya na Ushindani wa Kimataifa."

Address

MKAPA STADIUM, 2nd Floor
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baraza la Michezo la Taifa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Baraza la Michezo la Taifa:

Share