12/06/2026
Makonda: Kombe la Dunia 2026 kutupa Dira ya Kuandaa na Kusimamia AFCON 2027
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesema anatarajia kujifunza namna mashindano makubwa duniani yanavyoandaliwa na kusimamiwa kupitia ushiriki wake kwenye mechi za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Mexico.
Amesema hayo Juni 11, 2026, wakati akizungumza kwa njia ya simu akiwa Mexico kushuhudia michuano hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino, na kubainisha kuwa, ushiriki wake ni fursa ya kujionea kwa karibu namna mashindano makubwa ya kimataifa yanavyoandaliwa na kusimamiwa.
Mwaka 2027 Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano makubwa ya AFCON, hivyo uzoefu kutoka Kombe la Dunia 2026 utatumika kuboresha mashindano hayo na sekta ya michezo hapa nchini.