13/05/2026
Mhandisi Mwalami Kapipi kutoka Ofisi za Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini akizungumza na wasikilizaji wa Redio Access FM jijini Mbeya, amefafanua kwa kina utekelezaji wa miradi ya mawasiliano inayosimamiwa na UCSAF nchini.
Ameeleza jinsi miradi hiyo inavyolenga kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano, hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni, na namna inavyochangia kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi kupitia kuboresha mawasiliano.