14/05/2026
TCDC YATOA MAFUNZO YA KIMKAKATI KWENYE VYAMA VYA USHIRIKA ZANZIBAR
Tume ya maendeleo ya ushirika Tanzania (TCDC) kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Ushirika Zanzibar inatoa mafunzo ya kimkakati kwa Maafisa Ushirika, wanachama, viongozi na watendaji wa Vyama vya Ushirika Zanzibar.
Mafunzo yanayotolewa ni juu ya Uanachama wa kimkakati, Masoko ya kimkakati na endelevu na Ushirika biashara. Jumla ya maafisa Ushirika 11 upande wa Zanzibar wanachama, viongozi na watendaji 310 watanufaika na mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yameanza 11 Mei, 2026, ambapo yanaongozwa na Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo, Grace Msambaji, pamoja na Maafisa wengine kutoka Tume na Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU).
Aidha, timu hiyo ilipokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ajira, Vijana na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Wazir, kwa uratibu wa Mrajis na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika Zanzibar, Zainabu Hassan na Wakurugenzi mbalimbali wa wizara.
Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Randama ya Ushirikiano (MoU) baina ya TCDC na idara ya Màendeleo ya Ushirika Zanzibar.