16/08/2026
repost from HABARILEO DAR ES SALAAM; MTOTO Mtanzania Xyleen Mapunda (15) amesema amefurahi kujifunza namna madini ya urani yanavyotumika kutengeneza nishati ya nyuklia na faida zake.
-
Xyleen alisema hayo alipowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo Agosti 16, 2026 akitoka nchini Urusi.
-
Alikwenda huko kwa safari ya kielimu na kisayansi baada ya kushinda shindano la kimataifa la Icebreaker of Knowledge 2026 kupitia programu ya kampuni ya Nishati ya Nyuklia ya Urusi, Rosatom.
-
Xyleen ameweka historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza kufika Ncha ya Kaskazini (North Pole) katika safari ya siku 10 akiwa na wanafunzi wenzake wenye vipaji kutoka nchi 22 duniani.
-
Katika safari hiyo kutoka mji wa Murmansk kwenda Ncha ya Kaskazini, Franz Josef Land na kurejea Murmansk, wanafunzi hao walitumia meli kubwa zaidi duniani inayotumia nishati ya nyuklia 50 Let Pobedy.
-
“Meli yenyewe inatumia nyuklia, tumejifunza namna madini ya urani yanavyotumika kutengeneza nishati ya nyuklia na namna inavyotumika kwenye masuala mbalimbali… nimejifunza jambo zuri sana ambalo sikuwahi kufikiria,” alisema Xyleen.
-
Isome zaidi kupitia kiunganishi cha http://epaper.tsn.go.tz
Imeandaliwa na Zena Chande