Tume ya Madini

Tume ya Madini Ukurasa Rasmi wa Tume ya Madini Tanzania | The Official Account of Tanzania Mining Commission.

06/06/2026
05/06/2026

Welcome to the Tanzanite Exchange Centre (TEC) in Mirerani, Manyara Region—the world’s premier hub for the trading, certification, and marketing of tanzanite, a rare gemstone found only in Tanzania.

Established to enhance transparency, promote value addition, and expand access to global markets, the Centre is poised to transform Tanzania into a leading international gemstone trading destination while creating greater opportunities for miners, dealers, brokers, lapidarists, and international buyers.

04/06/2026

TUME YA MADINI YAHAMASISHA UWEKEZAJI KUPITIA MAONESHO YA UBUNIFU IRINGA

TUME YA MADINI YAHAMASISHA UWEKEZAJI KUPITIA MAONESHO YA UBUNIFU IRINGA📍IRINGATume ya Madini kupitia Ofisi ya Afisa Madi...
04/06/2026

TUME YA MADINI YAHAMASISHA UWEKEZAJI KUPITIA MAONESHO YA UBUNIFU IRINGA

📍IRINGA

Tume ya Madini kupitia Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Iringa imeendelea kuhamasisha uwekezaji katika Sekta ya Madini kwa kutoa elimu na kuonesha fursa mbalimbali zilizopo kupitia Maonesho ya Utafiti, Ubunifu na Huduma kwa Jamii yanayoendelea katika viwanja vya Garden Posta, Manispaa ya Iringa.

Maonesho hayo, yaliyowakutanisha taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi, yanalenga kuelimisha wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na taasisi hizo pamoja na fursa za kiuchumi zinazopatikana katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo sekta ya madini.

Akizungumza katika maonesho hayo, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mjiolojia Bertha Luzabiko, amesema ushiriki wa Tume ya Madini unalenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu shughuli za madini, taratibu za upatikanaji wa leseni za madini na fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta hiyo.

Amesema Mkoa wa Iringa una rasilimali mbalimbali za madini zenye mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi, hivyo wananchi na wawekezaji wanapaswa kuzitumia fursa hizo kwa kufuata sheria, kanuni na miongozo inayosimamia sekta ya madini nchini.

Awali akifungua maonesho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, aliwataka wananchi kutumia maonesho hayo kujifunza, kufanya ubunifu na kunufaika na fursa zinazotolewa na taasisi mbalimbali kwa maendeleo yao na ya taifa.

Maonesho hayo yameandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Mkwawa, yakilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za umma, sekta binafsi na wananchi katika kuchochea maendeleo kupitia utafiti, ubunifu na utoaji wa huduma bora kwa jamii.

04/06/2026
KAMATI YA KITAIFA YA UFUNGAJI MIGODI YAPITIA MPANGO WA UFUNGAJI WA MGODI WA SHANTA📍SONGWEKamati ya Kitaifa ya Ufungaji M...
03/06/2026

KAMATI YA KITAIFA YA UFUNGAJI MIGODI YAPITIA MPANGO WA UFUNGAJI WA MGODI WA SHANTA

📍SONGWE

Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi imekagua na kupitia Mpango wa Ufungaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Shanta (New Luika Gold Mine) uliopo mkoani Songwe ili kuhakikisha mpango huo unazingatia matakwa ya Sheria ya Madini, Sura ya 123, pamoja na Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira za mwaka 2010.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi, Mhandisi Hamisi Kamando, amesema mapitio hayo yanalenga kuhakikisha mgodi una mpango madhubuti wa kurejesha mazingira katika hali salama baada ya shughuli za uchimbaji kukamilika, sambamba na kulinda afya na usalama wa wananchi wanaouzunguka mgodi huo.

Amesema kwa mujibu wa Sheria ya Madini na Kanuni ya 206 ya Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira za mwaka 2010, migodi yote ya kati na mikubwa inatakiwa kuandaa na kuwasilisha mipango ya ufungaji migodi kwa Mkaguzi Mkuu wa Migodi kwa ajili ya mapitio ya kitaalam kabla ya kuidhinishwa na Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi.

Mhandisi Kamando amefafanua kuwa jukumu la Kamati hiyo ni kupitia mipango ya ufungaji migodi na kutoa ushauri wa kitaalam ili kuhakikisha migodi inafungwa kwa kuzingatia viwango vya mazingira, usalama na afya, na siyo kusitisha shughuli za uzalishaji kabla ya migodi kumaliza rasilimali zake.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Shanta (New Luika Gold Mine), Mhandisi Exupery Lyimo, amesema mgodi huo unaendelea kutekeleza viwango vya usalama, afya na utunzaji wa mazingira na upo tayari kutekeleza maelekezo yote yatakayotolewa na Kamati ili kuboresha mpango wake wa ufungaji.

Kikao hicho kimewakutanisha wataalam kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Madini, Wizara ya Maji, Wizara ya Maliasili na Utalii, Tume ya Matumizi Endelevu ya Ardhi, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Tume ya Madini pamoja na viongozi wa Serikali wa ngazi ya wilaya.

Address

Mining Commission HQ
Dodoma

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 07:30 - 17:00
Thursday 08:00 - 15:30
Friday 08:00 - 15:30

Telephone

+255262320051

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tume ya Madini posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tume ya Madini:

Shortcuts

Share