Maelezo News

Maelezo News Ukurasa Rasmi wa Idara ya Habari - MAELEZO ~ Information Services Department πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

29/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akishuhudia Mhe. George Mcheche Masaju, Jaji Mkuu wa Tanzania akimuapisha, Mhe. Deogratius John Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma, leo Agosti 29, 2026.

πŸ“Œ
29/08/2026

πŸ“Œ

Katika kukenga uelewa kuhusu Ugonjwa wa Saratani, kupitia Maelezo Podcast tumemualika Daktari Bingwa wa magonjwa ya Sara...
29/08/2026

Katika kukenga uelewa kuhusu Ugonjwa wa Saratani, kupitia Maelezo Podcast tumemualika Daktari Bingwa wa magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (OTCI), Dkt. Chrispin Kahesa, tumezungumza kuhusu Saratani na namna inavyoathiri makundi mbalimbali katika jamii, jitihada za kuzuia na tiba ya saratani.

Bofya kusikiliza πŸ‘‡πŸΎ

https://www.buzzsprout.com/988291/episodes/19720972

Sikiliza MAELEZO PODCASTS β€” Tupo kwenye audio channels zote πŸ“Œ

Katika kujenga uelewa kuhusu ugonjwa wa saratani, kupitia Maelezo Podcast tumemualika Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), Dkt. Chrispin Kahesa, tumezungumza kuhusu saratani na namna inavyoathiri ...

Mazungumzo na Bw. Atufigwege Mwakabalile, Afisa Mwandamizi wa Benki kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) kuhusu sheria ya fed...
17/08/2026

Mazungumzo na Bw. Atufigwege Mwakabalile, Afisa Mwandamizi wa Benki kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) kuhusu sheria ya fedha nchini na marufuku iliyotilewa ya kutotunza fedha kwa kutupa chini.

Bofya kutazama πŸ‘‡πŸΎ

Mazungumzo na Bw. Atufigwege Mwakabalile, Afisa Mwandamizi wa Benki...

29/07/2026

Maadhimisho Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa ni kila mwaka, Julai 25 β€” Tukitambua mchango mashujaa wote katika kulinda uhuru, amani na mipaka ya Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

MKUTANO MKUU WA WANAHISA NA JUKWAA LA MIUNDOMBINU AFRIKA 2026
26/07/2026

MKUTANO MKUU WA WANAHISA NA JUKWAA LA MIUNDOMBINU AFRIKA 2026


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema ujenzi ...
15/07/2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa mpira wa miguu Dodoma umefikia asilimia 12, akieleza kuwa eneo la mzunguko la uwanja huo linatarajiwa kufikia asilimia 50 ifikapo Desemba 2026.

Msigwa amesema hayo Julai 15, 2026, alipofanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo unaotarajiwa kubeba mashabiki 32,000 pindi utakapokamilika katika eneo la Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema kuchelewa kwa mradi huo kwa kiasi fulani kumesababishwa na hatua ya Serikali kujiridhisha kuhusu ubora wa kazi inayotekelezwa na mkandarasi pamoja na kuhakikisha miundombinu na vifaa vyote muhimu vinavyohitajika katika uwanja huo vinawekwa kwa viwango vinavyostahili ili kiwango cha fedha zilizotolewa kiendane na ubora wa mradi.

"Ndugu zangu wananchi, pamoja na kwamba tunaye Mkandarasi hatuwezi kutekeleza mradi huu kwa kukurupuka. Lazima tujiridhishe kuhusu ubora wa kazi zinazofanywa na Mkandarasi na kuhakikisha vifaa vyote vinavyotakiwa vimewekwa ili tupate uwanja wa viwango vya kimataifa," amesisitiza Msigwa.

Amesema baada ya majadiliano kati ya Serikali na mkandarasi kukamilika, utekelezaji wa mradi unaendelea kwa kasi na ifikapo Desemba 2026 mradi huo unatarajiwa kufikia asilimia 50, ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa mzunguko wa kwanza wa ujenzi.

"Dodoma ni makao makuu ya nchi, hivyo ni lazima iwe na uwanja unaoakisi hadhi hiyo. Serikali itaendelea kusimamia mradi huu kwa umakini ili kuhakikisha tunapata uwanja wenye ubora tunaoutarajia," amesema Msigwa.

Aidha, amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha ifikapo Desemba 2027 mradi huo unakuwa umekamilika au umefikia hatua za mwisho za ukamilishaji, huku kasi ya ujenzi ikiendelea kuimarika.

Kwa upande wake, Mkandarasi na Mshauri elekezi wa mradi huo, Ashraf Shawky, amesema ifikapo Desemba, 2026 mzunguko wa kwanza wa uwanja wenye uwezo wa kubeba watazamaji 16,000 utakuwa umekamilika, wakati ujenzi wa mzunguko wa pili ukiendelea kwa kasi.

Pia amesema amepokea maelekezo ya Serikali na kuahidi kuhakikisha mradi unakamilika kwa ubora uliokusudiwa na kwa kuzingatia viwango na mahitaji yote muhimu yaliyowekwa.

Mwisho

Utekelezaji wa Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa uliopo Msalato jijini Dodoma umefikia asilimia 87.97 na unatarajiwa...
13/07/2026

Utekelezaji wa Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa uliopo Msalato jijini Dodoma umefikia asilimia 87.97 na unatarajiwa kukamilika Septemba, 2026.

Kiwanja hicho kitakuwa na uwezo wa kupokea ndege 17 kwa wakati mmoja zikiwemo ndege kubwa aina ya Boeing 787 Dreamliner au Airbus A330 na kitahudumia wananchi takribani milioni 1.5 kwa mwaka.

Utekelezaji wa Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa uliopo Msalato...

Taarifa kwa umma kuhusu makala ya BBC πŸ“Œ
13/07/2026

Taarifa kwa umma kuhusu makala ya BBC πŸ“Œ

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Ithibati ya Maisha utakaowezesha waandishi wa ...
11/07/2026

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Ithibati ya Maisha utakaowezesha waandishi wa habari wakongwe waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya tasnia ya habari nchini kutambuliwa rasmi, licha ya kutokukidhi vigezo vya kielimu vilivyowekwa na Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ya mwaka 2016.

SOMA ZAIDIπŸ‘‡πŸΎ
https://www.instagram.com/p/DaqfwPfDtEv/?igsh=emhzdzU0ejd4eDRo

Address

Mji Wa Serikali/Mtumba
Dodoma
40481

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maelezo News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share