12/08/2026
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Mhe. Prof Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa Wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) kufanya kazi kwa bidii na Ushirikiano kwa Maslahi ya Wananchi kwani Baraza hilo lipo kimkakati.
Waziri Kabudi amesema hayo katika Ziara aliyoifanya Ofisi za Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) zilizopo katika Viwanja vya Nanenane Nzuguni, hii leo Agosti 12,2026.
Waziri amesema “Baraza hili liko kwa ajili ya kuwasaidia Wananchi kwa kuwawezesha kiuchumi katika sekta mbalimbali, hivyo basi inabidi muendelee kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kuinua Uchumi wa Wananchi na Taifa kwa ujumla”
Vilevile alilishauri Baraza kujitangaza zaidi kwa Wananchi waweze kulitambua, na kunufaika na fursa zinazotolewa.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) Bw. Gwakisa Bapala amemwomba Waziri kusaidia katika upitishaji wa kanuni za Mifuko ya Uwezeshaji lakini pia kuharakisha utaratibu wa kuanzisha mfuko wa Uwezeshaji wa Baraza.
Nae pia Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) Prof. Aurelia Kamuzora amemshukuru Waziri kwa ujio wake na kuahidi wao k**a bodi wataenda kuyasimamia yale yote aliyoelekeza.