Tax Ombudsman Services Tanzania

Tax Ombudsman Services Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tax Ombudsman Services Tanzania, Government Organization, P. O BOX 1441, Dodoma.

πŸš€ π‡πšπ›πšπ«π’ 𝐧𝐣𝐞𝐦𝐚!Suluhu ya Kodi App sasa inapatikana kwa Android na iPhone (iOS). πŸ“±Furahia huduma za Ofisi ya Usuluhishi w...
03/06/2026

πŸš€ π‡πšπ›πšπ«π’ 𝐧𝐣𝐞𝐦𝐚!

Suluhu ya Kodi App sasa inapatikana kwa Android na iPhone (iOS). πŸ“±

Furahia huduma za Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) kwa urahisi, popote ulipo na wakati wowote, kiganjani mwako.

Pakua sasa na uanze kutumia.

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) na Wakala wa Kodi wa Denmark wamefanya kikao cha pamoja cha ...
01/06/2026

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) na Wakala wa Kodi wa Denmark wamefanya kikao cha pamoja cha ushirikiano Wizara ya Fedha Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Kikao hicho kililenga kujadili na kubainisha maeneo muhimu ya ushirikiano yatakayochangia maendeleo endelevu ya Taasisi hizo mbili. Aidha, pande hizo zilijadiliana kuhusu kubadilishana uzoefu na mbinu bora za utendaji kwa lengo la kuongeza ulipaji kodi wa haiari na kupunguza gharama kwenye usimamizi na ukusanyaji wa kodi.

Ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza chachu katika mlolongo mzima wa ukusanyaji wa kodi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wadau mbalimbali wa sekta ya kodi.

27/05/2026
Baadhi ya matukio katika picha za Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taari...
15/05/2026

Baadhi ya matukio katika picha za Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST), uliofanyika tarehe 14–15 Mei 2026 mjini Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya 4R’s ya Mheshimiwa Ra...
14/05/2026

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya 4R’s ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inayolenga kuimarisha mazingira ya ulipaji kodi wa hiari pamoja na kuongeza uaminifu kati ya mlipakodi na Serikali.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha, Bw. Lusius Mwenda, wakati akifungua Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi wa TOST uliofanyika Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Aidha, Bw. Mwenda amewataka wafanyakazi wa Taasisi hiyo kuendelea kuzingatia ushirikiano na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ili kufanikisha maono ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Erastus Mtui, amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kujadili na kufanyia kazi hoja mbalimbali kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

Matukio katika Picha ni Wafanyakazi wa Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) ambao wameungana na W...
01/05/2026

Matukio katika Picha ni Wafanyakazi wa Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) ambao wameungana na Wafanyakazi wengine katika kusherehekea maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) inaendelea kuboresha huduma zake kwa kuhakikisha Wananchi wa...
29/04/2026

Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) inaendelea kuboresha huduma zake kwa kuhakikisha Wananchi wanapata huduma kwa urahisi, haraka na bila ulazima wa kufika ofisini.

Kupitia maboresho ya mifumo ya huduma kupitia simu za kiganjani, TOST inalenga kumfikia kila mwananchi popote alipo, ikiwa ni pamoja na watumiaji wa simu za kawaida ambazo sio za kupapasa, ili waweze kupata huduma muhimu kwa urahisi hata bila matumizi ya kifurushi cha intaneti.

Hii ni hatua muhimu katika kujenga huduma jumuishi, bora na inayomfikia kila mtu bila kujali aina ya simu anayomiliki. Maboresho hayo yanatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwisho wa Mwezi Mei 2026.

Address

P. O BOX 1441
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tax Ombudsman Services Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share