Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Karibu katika ukurasa rasmi wa Facebook wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo ni Wizara inayoendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji stahiki wa Habari, kukuza Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa lengo la kuleta maendeleo ya jamii na kiuchumi.

Watumishi Wapya Wizara ya Habari Wanolewa  Misingi ya Utumishi wa UmmaWizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imet...
08/09/2026

Watumishi Wapya Wizara ya Habari Wanolewa Misingi ya Utumishi wa Umma

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetoa mafunzo kwa Watumishi wapya walioajiriwa wizarani hapo kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu misingi, taratibu, na maadili ya Utumishi wa Umma.

Akifungua mafunzo hayo leo Septemba 08, 2026 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Methusela Ntonda amewataka watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi, uadilifu, nidhamu na uwajibikaji, akisisitiza umuhimu wa kuifahamu vyema Sheria, Kanuni na Taratibu zinazoongoza utumishi wa umma.

Amesema, mafunzo hayo ni sehemu muhimu ya kuwaandaa ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

08/09/2026

MAMBO MAWILI, LUGHA CHAFU NA RUSHWA

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KATIKA TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
08/09/2026

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KATIKA TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

07/09/2026
06/09/2026

MAKONDA ATOA MILIONI 10 KUUNGA MKONO UJENZI WA KANISA KUU ARUSHA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Paul Makonda, amechangia Shilingi milioni 10 katika harambee ya ujenzi wa Kanisa Kuu la Arusha, akisema mchango huo ni sehemu ya kumuunga mkono Waziri Mkuu pamoja na waumini katika kufanikisha ujenzi huo.

Makonda amesema akiwa mwakilishi wa wananchi wa Arusha, anaona umuhimu wa kuunga mkono jitihada za maendeleo ya jamii na taasisi za dini, huku akimuomba Baba Askofu kuendelea kumuombea katika utekelezaji wa majukumu yake ya kulitumikia Taifa.

Amesema anaamini kupitia ushirikiano wa viongozi, waumini na wananchi, ndoto ya kukamilisha ujenzi wa Kanisa Kuu la Arusha itatimia.

TANZANIA YAKABIDHIWA BENDERA  KUWA MWENYEJI WA MASHINDANO YA MISS WORLD 27Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Mi...
06/09/2026

TANZANIA YAKABIDHIWA BENDERA KUWA MWENYEJI WA MASHINDANO YA MISS WORLD 27

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, amekabidhiwa rasmi bendera ikiwa ni ishara ya kupokea kijiti cha kuandaa mashindano ya 74 ya Ulimbwende wa Dunia (Miss World 2027)

Amekabidhiwa bendera hiyo Septemba 05, 2026 nchini Vietnam wakati wa mashindano ya Miss World 2026.

05/09/2026

TANZANIA YAKABIDHIWA BENDERA KUWA MWENYEJI WA MASHINDANO YA MISS WORLD 27

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, amekabidhiwa rasmi bendera ikiwa ni ishara ya kupokea kijiti cha kuandaa mashindano ya 74 ya Ulimbwende wa Dunia (Miss World 2027)

Amekabidhiwa bendera hiyo leo, Septemba 05, 2026 nchini Vietnam wakati wa mashindano ya Miss World 2026. Baraza la Sanaa (BASATA)

Address

S. L. P 25 Mtumba
Dodoma
00000

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share