Handeni Town Council

Handeni Town Council Imeanzishwa, Julai 2015
Ipo Mkoa wa Tanga,
Wilaya ya Handeni

Halmashauri ya Mji Handeni tupo tayari kushiriki SHIMISEMITA 2026SHIRIKISHO LA MICHEZO LA WATUMISHI WA SERIKALI ZA MITAA...
17/07/2026

Halmashauri ya Mji Handeni tupo tayari kushiriki SHIMISEMITA 2026

SHIRIKISHO LA MICHEZO LA WATUMISHI WA SERIKALI ZA MITAA
OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI

Bonanza la Watumishi Tarehe 11/07/2026
09/07/2026

Bonanza la Watumishi Tarehe 11/07/2026

Pongezi kwa ufaulu mzuri  wa Mtihani wa Kidato cha Sita Mwaka 2026Haya ni matokeo ya juhudi, ushirikiano na bidii ya kil...
07/07/2026

Pongezi kwa ufaulu mzuri wa Mtihani wa Kidato cha Sita Mwaka 2026

Haya ni matokeo ya juhudi, ushirikiano na bidii ya kila mmoja katika kuhakikisha kuwa elimu bora inatolewa kwa wanafunzi.

Tuendelee kushirikiana na kuongeza ubunifu na weledi ili tufikie ufanisi zaidi katika mia

02/07/2026

WaterAid Wamaliza Adha ya Kutembea Umbali wa Kilomita 10 Kutafuta Maji Handeni Mji

Wananchi wa Kata ya Kideleko, Halmashauri ya Mji Handeni, wameeleza namna walivyokuwa wakitembea umbali wa hadi kilomita 10 kutafuta maji kutokana na ukosefu wa huduma hiyo karibu na makazi yao. Kupitia Mradi wa Usambazaji wa Maji wa Kwamaizi uliotekelezwa na WaterAid Tanzania kwa kushirikiana na Serikali na washirika wa maendeleo, adha hiyo imeondolewa kwa kiasi kikubwa, na kuwawezesha wananchi zaidi ya 6,000 kupata huduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao.

WATERAID YAKABIDHI MRADI WA MAJI WA SH. MILIONI 465  HANDENI  MJINa Job Karongo - Handeni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji,...
02/07/2026

WATERAID YAKABIDHI MRADI WA MAJI WA SH. MILIONI 465 HANDENI MJI

Na Job Karongo - Handeni

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, leo Julai 2, 2026, amepokea rasmi Mradi wa Usambazaji wa Huduma ya Maji ya Mtandao wa Bomba wa Kwamaizi uliotekelezwa katika Kata ya Kideleko, Halmashauri ya Mji Handeni, Mkoa wa Tanga.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mhandisi Waziri amesema Serikali itaendelea kushirikiana na washirika wa maendeleo katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za maji safi, usafi wa mazingira na usafi binafsi ili kuboresha afya na ustawi wa wananchi.

Mradi huo uliotekelezwa na WaterAid Tanzania kwa ufadhili wa OKF, kwa kushirikiana na Wizara ya Maji, RUWASA, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Handeni (HTM) pamoja na Halmashauri ya Mji Handeni, umetumia Shilingi Milioni 465,182,915.20 TZS na unatarajiwa kunufaisha wananchi 6,037 wa maeneo ya Kideleko, Kampene, Muungano, Ndekai na Bangu.

Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chujio la maji lenye uwezo wa kuhifadhi lita 100,000, tenki la kuhifadhi maji lenye ujazo wa lita 100,000, ulazaji wa bomba kuu la kusafirisha maji lenye urefu wa mita 1,485, uchimbaji na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa mita 2,358, pamoja na ujenzi wa vituo vitatu vya kuchotea maji vyenye mfumo wa malipo ya kabla.

Mhandisi Waziri amesisitiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Handeni (HTM), RUWASA, viongozi wa Serikali za Mitaa na wananchi kuendelea kulinda, kutunza na kusimamia miundombinu hiyo ili huduma ya maji iendelee kuwa endelevu na kuwanufaisha wananchi kwa muda mrefu.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa WaterAid Tanzania, Bi. Anna Mzinga, ameitaka RUWASA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Handeni (HTM) pamoja na Halmashauri ya Mji Handeni kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza na kupanua huduma za mradi huo ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Mkurgugenzi huyo amebainisha kuwa usimamizi bora wa miundombinu wa mradi huo utahakikisha uwekezaji uliofanywa unaendelea kuleta matokeo chanya kwa muda mrefu.

TANZIA
21/06/2026

TANZIA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Maryam Ukwaju akishiriki Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zilizofanyika Halmashauri...
21/06/2026

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Maryam Ukwaju akishiriki Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zilizofanyika Halmashauri ya Mji Handeni Juni 18,2026

Mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2926 Halmashauri ya Mji tarehe 18/06/2026  Juma Nature atakuwepo isipange kukosa
18/06/2026

Mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2926 Halmashauri ya Mji tarehe 18/06/2026 Juma Nature atakuwepo isipange kukosa

HANDENI MJI YAPOKEA MWENGE WA UHURU, WAKAGUA MIRADI YA THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.2Halmashauri ya Mji Handeni imepoke...
18/06/2026

HANDENI MJI YAPOKEA MWENGE WA UHURU, WAKAGUA MIRADI YA THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.2

Halmashauri ya Mji Handeni imepokea Mwenge wa Uhuru 2026 ambao umepita na kukagua, kuzindua, kuweka mawe ya msingi na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 2.2.

Miradi hiyo inahusisha sekta za elimu, afya, maji, miundombinu na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu na kuboresha huduma za kijamii.

Tanzania ni yetu sote Tushikamane kwa pamoja kuleta Maendeleo

TangamkoaRS
OFISI YA WAZIRI MKUU TAMISEMI
@

Wasanii watakaotumbuiza kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2026 Halmashauri ya Mji Handeni  tarehe 18/06/2026Ofisi ya  Mku...
17/06/2026

Wasanii watakaotumbuiza kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2026 Halmashauri ya Mji Handeni tarehe 18/06/2026

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni
TangamkoaRS

Address

P. O. BOX 51
Handeni
21801

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Handeni Town Council posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share