Halmashauri ya Mji Kasulu

Halmashauri ya Mji Kasulu Kasulu ni yetu sote, Karibu sana

KATA 15 ZAWASILISHA TAARIFA ZA MAENDELEO KASULU TCKatika kuchochea maendeleo ya Halmashauri ya Mji Kasulu, Kata zote 15 ...
28/08/2026

KATA 15 ZAWASILISHA TAARIFA ZA MAENDELEO KASULU TC

Katika kuchochea maendeleo ya Halmashauri ya Mji Kasulu, Kata zote 15 za zimewasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika kikao cha Madiwani na Wakuu wa Idara kilichofanyika katika Ukumbi wa Fatina H. Raay.

Taarifa hizo zimeainisha hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo ikiwemo masuala ya uchumi, afya, elimu, usalama, usafi wa mazingira na utoaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mgeni Rasmi ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu Therezia Mtewele, amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu na kuwataka viongozi katika ngazi za Kata kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Mwl. Vumilia J. Simbeye ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa Kata na wadau mbalimbali katika kuhakikisha miradi na shughuli za maendeleo zinatekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi.

Madiwani wamepokea taarifa hizo na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ili kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hongera MHE. DEOGRATIUS JOHN NDEJEMBI kwa kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Mwenyezi Mung...
28/08/2026

Hongera MHE. DEOGRATIUS JOHN NDEJEMBI kwa kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenyezi Mungu akuongoze 🤲✅️

TAARIFA YA BARAZA LA MADIWANI  ROBO YA NNE MWAKA WA FEDHA 2025/2026 ✅️
28/08/2026

TAARIFA YA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA NNE MWAKA WA FEDHA 2025/2026 ✅️

BADO SIKU 13 TUTAUPOKEA,TUTAKESHA NAO NA TUTAZUNGUKA NAO KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MJI KASULU ✅️
27/08/2026

BADO SIKU 13 TUTAUPOKEA,TUTAKESHA NAO NA TUTAZUNGUKA NAO KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MJI KASULU ✅️

27/08/2026

MWL. FURAHA AMOS AFICHUA SIRI, UGUMU WA MASHINDANO YA UCHORAJI SHIMISEMITA 2026

Katika mashindano ya uchoraji SHIMISEMITA 2026, Mwl. Furaha Amos amefichua siri iliyomsaidia kushika nafasi ya tano kati ya washiriki 27 kutoka Halmashauri mbalimbali nchini huku akiahidi kuyafanyia kazi maelekezo na ushauri aliopewa ili kuboresha zaidi na kuhakikisha anafanya vizuri katika mashindano yajayo.

Mwl. Furaha ameyasema hayo baada ya kutamatika kwa mashindano ya uchoraji yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mkapa, Jijini Mbeya.

Amesema nafasi hiyo ni hatua muhimu kwake na imempa uzoefu mkubwa akitambua maeneo yanayohitaji maboresho ili kuongeza ushindani na kufikia nafasi za juu katika mashindano yajayo.

26/08/2026

HAYA HAPA MATOKEO YA MCHEZO WA UCHORAJI SHIMISEMITA 2026, KASULU TC YASHIKA NAFASI YA TANO KATI YA HALMASHAURI 37 ZILIZOSHIRIKI.

Halmashauri ya Mji Kasulu imeendelea kuonesha ushindani katika Mashindano ya Watumishi wa Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) 2026 yanayoendelea Jijini Mbeya, baada ya kushika nafasi ya tano katika matokeo ya jumla ya uchoraji.

Kasulu TC imekusanya jumla ya alama 127 sawa na wastani wa asilimia 63.50 katika michoro miwili iliyochorwa ndani ya ukumbi wa Benjamin Mkapa.

Katika picha ya kwanza, Kasulu TC imepata alama 63 huku picha ya pili ikipata alama 64 na kufanya jumla ya alama kufikia 127.

Matokeo hayo yanaifanya Kasulu TC kushika nafasi ya tano kati ya Halmashauri 37 zilizoshiriki katika mchezo huo huku Handeni DC ikishika nafasi ya kwanza kwa kuvuna alama 148, Mbeya Jiji imeshika nafasi ya pili baada ya kuvuna alama 147, Arusha Jiji nafasi ya tatu kwa kuvuna alama 134 na Ngara DC ikishika nafasi ya nne kwa kuvuna alama 132.

Hata hivyo, Kasulu TC bado inaendelea kuwania medali mbalimbali ikiwemo riadha ya mita 1,500 pamoja na urushaji wa tufe.

Mwakilishi wa Halmashauri ya Mji Kasulu katika mchezo wa kurusha kisahani (Discus), Silvesta Sugwejo ameshika nafasi ya ...
26/08/2026

Mwakilishi wa Halmashauri ya Mji Kasulu katika mchezo wa kurusha kisahani (Discus), Silvesta Sugwejo ameshika nafasi ya nne kati ya washiriki 63 kutoka Halmashauri mbalimbali nchini katika mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yanayoendelea Jijini Mbeya.

Silvesta amefanikiwa kushika nafasi hiyo baada ya kurusha kisahani kwa umbali wa mita 24.92 na kufanya vyema kwa kushinda washiriki kutoka Halmashauri mbalimbali nchini.

Ikumbukwe kuwa zaidi ya Halmashauri 177 zinashiriki katika mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yanayoendelea Jijini Mbeya.

UKIFUATA TU VIGEZO HIVI TAYARI UNAJIPATIA MKOPO NAFUU ZAIDI ✅️
24/08/2026

UKIFUATA TU VIGEZO HIVI TAYARI UNAJIPATIA MKOPO NAFUU ZAIDI ✅️

KARIBU UJIPATIE MKOPO NAFUU ZAIDI USIOKUWA NA MAKANDOKANDO✅️
24/08/2026

KARIBU UJIPATIE MKOPO NAFUU ZAIDI USIOKUWA NA MAKANDOKANDO✅️

23/08/2026

KABLA JOGOO KUWIKA FABIAN MANYAMA DOTTO ASHINDA TENA RIADHA MITA 1500 NA KUKWEA FAINALI YA PILI.

Mwakilishi wa Halmashauri ya Mji Kasulu katika mchezo wa riadha Fabian Manyama Dotto ameshinda tena riadha mita 1500 kwa kushika nafasi ya kwanza baada ya kutumia dakika 4:50 na kufanikiwa kukwea hatua ya fainali mashindano ya SHIMISEMITA 2026 Jijini Mbeya.

Manyama ametinga fainali yake ya pili kufuatia ushindi wake wa nafasi ya kwanza katika mbio za mita 1500 na 3000 .

Address

475
Kasulu
48500

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halmashauri ya Mji Kasulu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share