01/06/2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, ndugu Joseph Kashushura na Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Mhe. Desderius Haule wamepokea vitenge kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Rizex For Life, Dkt. Riziki Nkya, ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono na kuhamasisha viongozi na watumishi kushiriki katika Mtoko wa Familia unaotarajiwa kufanyika tarehe 04 Julai,2026 katika ukumbi wa Songea Klabu, Songea Mjini.
Akizungumza leo, tarehe 01Juni, 2026 Dkt. Riziki Nkya amebainisha kuwa lengo la Mtoko wa Familia ni kuwakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kubadilishana mawazo na kufurahi pamoja.
Aidha, Dkt. Riziki ameeleza kuwa katika mtoko huo washiriki watapata kadi kwa gharama nafuu pamoja na vitenge. Alifafanua kuwa mtu mmoja (Single) atapata kadi kwa shilingi 70,000/=, Maalum ( V.I.P) shilingi 150,000/=, mume na mke (Couple) 170,000/=, meza ya watu kumi(10) shilingi milioni moja tu.
" Siku hiyo itapambwa na wanamuziki maarufu, MC mahiri na washiriki watapata mada motomoto kuhusu familia na burudani mbalimbali zitakuwepo." Aliongeza Dkt. Riziki.