18/03/2026
Kikao cha pamoja na Wakuu wa Wilaya kilifanyika kwa lengo la kutoa mrejesho wa mafunzo ya kukabiliana na majanga yaliyowezeshwa na Norwegian Church Aid Tanzania kwa kushirikiana na Kanisa Anglikana Dayosisi ya Morogoro.
Malengo ya kikao hicho yalikuwa ni:
1. Kujitambulisha rasmi kwa ofisi husika kuhusu ushiriki wa DDSCDO-Kupitia Kanisa Anglikana Dayosiai ya Morogoro katika juhudi za kusaidia Serikali katika maandalizi na mwitikio wa dharura ya majanga, hususan mafuriko katika maeneo ya Wilaya ya Mvomero.
2. Kuwasilisha mrejesho wa awali wa mafunzo yaliyofanyika tarehe 13–14 Machi 2026, ambayo yalilenga kuimarisha uratibu na ushirikiano kati ya wadau katika kukabiliana na majanga.
3. Kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya DDSCDO na Serikali ya Wilaya pamoja na Halmashauri ili kuhakikisha hatua za maandalizi na mwitikio wa majanga zinafanyika kwa uratibu na ufanisi.
Katika kikao hicho, pia tulijadiliana kwa kina namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya wadau mbalimbali pamoja na kubainisha mahitaji muhimu ya msingi kwa wananchi waliopo katika kata zilizoathirika na mafuriko katika Wilaya za Kilosa na Mvomero. Aidha, tulitambua baadhi ya kata zilizoathirika zaidi, zikiwemo Doma, Mhonda na Sungaji (Mvomero), pamoja na Tindiga, Mhenda na Myombo (Kilosa).