03/06/2026
Katika kuelea kwenye maazimisho ya Mazingira Dunia leo tumeshirikians na uongozi wa Serikali kijiji ikiongozwa na Zmh Diwani wa Kata ya Magole katika kampeni ya upandaji miti katika Zahanati inayojengwa kijiji cha Mandela pamoja na Ofisi ya Serikali ya Kijiji.
Zoezi hili limeratibiwa na kikundi cha Mazingira ambacho kiliandaa kitalu cha miche zaidi ya 300 ambayo imepandwa leo katika maeneo husika na mingine kugawiwa kwa wananchi walijitokeza kushiriki kampeni hii ya mazingira ikiwemo na kusafisha(Kufyeka) eneo la Zahanati na kuchimba choo cha Dharula kitakacho tumika kipindi cha ujenzi .
Kupitia Program ya Mazingira na uwakili(Climate abd Environmental Stewarship-CES) inafadhiliwa ba kuelekea kupitia Vikundi vya huduma ndogo za Kifedha(IR-VICOBA) wanajamii wameendelea pia na ujenzi wa majiko bsnifu na Sanifu ili kukabiliana na Athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuendsna ba kauli mbiu ya mwaka inayosema “Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi”