14/07/2020
*KOSA LA JINAI.
Je, wajua kuhusu kosa la jinai, aina na adhabu zake? Basi ungana nasi katika makala yetu..
Kosa la jinai ni tendo lolote ambalo limekatazwa kwa sheria, ambapo mtu yeyote
akilitenda anakuwa ameikosea Jamhuri. Katika makosa ya jinai, mlalamikaji anakuwa ni
Jamhuri, ikiwakilishwa na mwendesha mash*taka wa Serikali. Mtu binafisi aliyedhurika
kwa tendo lakijinai siye anayesh*taki mahak**ani.Yeye anabakia kuwa ni shahidi tu,
nani marachache kwamba Mahak**a inaweza kuagiza kulipwa fidia kwa mtu
aliyedhuriwa na tendo la kijinai.
Katika Makosa ya Jinai, mtu anaye patikana na hatia huadhibiwa, na anayeonekana
hana hatia huachiwa huru.
*ADHABU ZA KOSA LA JINAI
Adhabu za makosa ya Jinai ni pamoja na :kuachiwa kwa
masharti, kifungo cha nje, faini, kifungo gerezani kwa muda maalum, kifungo cha
maisha na kunyongwa hadi kufa.
Makosa ya aina hii ni pamoja na wizi, mauaji, kumiliki silaha kinyume cha sheria,
ubakaji, kutozingatia sheria za barabarani,nk. Makosa yote ya Jinai sharti yawe
ya meandikwa katika sheria mbalimbali. Hatahivyo, kwa nchi ya Tanzania, makosa
mengi ya Jinai yametajwa katika Kanuniya Adhabu (Suraya16yaSheriazaTanzania).
Mtu anayefikishwa mahak**ani kwa kosa la jinai huitwa mtuhumiwa kwa muda wote
baada ya kuk**atwa, kupelekwa kituo cha polisi na hata wakati wa kujitetea
mahak**ani. Akishapatikana na hatia huitwa mhalifu, na akiadhibiwa kwa kifungo
gerezani huitwa mfungwa.
*VITU VINAVYO KAMILISHA KOSA LA JINAI.
Kimsingi, kosa lolote la jinai linakamilishwa na vitu viwili; tendolenyewe lililo katazwa,
na nia ovu ya kutekeleza tendo hilo. Mahak**a inaposikiliza shauri lolote la jinai
hutafuta kujiridhisha iwapo mambo yote hayo mawili yamethibitika kutokea. Katika
mchakato wa kuthibitisha mambo hayo upande wa mash*taka na ule wa utetezi
husikilizwa kwa makini, mashahidi huitwa mahak**ani na wakati mwingine, ikibidi,
vidhibiti mbalimbali huwasilishwa mbele ya mahak**a ilikuthibitisha kwamba kweli
tendo lililo haramishwa lilitokea, na aliyelitenda alifanya hivyo kwa makusudi.
ITAENDELEA....