Tanzania Coffee Board

Tanzania Coffee Board 𝐇𝐚𝐩𝐩𝐲 𝐂𝐨𝐟𝐟𝐞𝐞 𝐅𝐚𝐫𝐦𝐞𝐫

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akifuatilia kwa makini maelezo ya mmoja wa wazalishaji wa m...
27/04/2023

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akifuatilia kwa makini maelezo ya mmoja wa wazalishaji wa miche bora ya kahawa na mkulima Bw.Joseph Kanute,kutoka kata ya Mkumbi, Mbinga DC.

Mkulima huyu anazalisha miche bora aina ya Copmact Zaidi ya 100,000, huku akiwa na shamba la kahawa ekari zaidi ya 4.5, ambapo , Bw.Kajiru Kisenge, amemtia moyo na kusema mzalishaji huyu wa miche ni mfano wa kuigwa na kuwataka wazalishaji wengine kuiga mfano wake.

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akifuatilia kwa makini maelezo ya mmoja wa wazalishaji wa m...
27/04/2023

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akifuatilia kwa makini maelezo ya mmoja wa wazalishaji wa miche bora ya kahawa na mkulima Bw.Joseph Kanute,kutoka kata ya Mkumbi, Mbinga DC.

Mkulima huyu anazalisha miche bora aina ya Copmact Zaidi ya 100,000, huku akiwa na shamba la kahawa ekari zaidi ya 4.5, ambapo , Bw.Kajiru Kisenge, amemtia moyo na kusema mzalishaji huyu wa miche ni mfano wa kuigwa na kuwataka wazalishaji wengine kuiga mfano wake.

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akitoa maelekezo mafupi jinsi ya kuandaa kiriba, tayari kwa...
27/04/2023

Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, akitoa maelekezo mafupi jinsi ya kuandaa kiriba, tayari kwa kupandwa mbegu, kwa wafanyakazi wa shamba darasa la TaCRI, Mgano Mbinga, leo hii April 27/2023.

Bodi ya Kahawa Tanzania - TCB, inaendelea na zoezi la kuwatembelea wakulima na baadhi ya vyama vya msingi AMCOS, ili kuhakikisha zoezi la ugawaji miche bora na ya kisasa linafanikiwa kwa kiwango kikubwa ili kufikia malengo ya uzalishaji wa tani Zaidi ya 300,000 ifikapo mwaka 2025.

Pichani juu ni Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, {wa pili kutoka kulia) akitoa historia fupi ...
27/04/2023

Pichani juu ni Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kisenge, {wa pili kutoka kulia) akitoa historia fupi kwa Meneja wa kanda ya Ruvuma, njombe na Iringa, Bw.Peter Buberwa, {wa kwanza kutoka kulia}, Rashid Abdillah {wa tatu kutoka kulia na Meneja wa shamba la MBIFACU, lenye ukubwa wa hekari Zaidi ya 100, Bw.Henry Kindimbo {wa kwanza kutoka kushoto}

Mti huu wa kahawa ulipandwa katika shamba la MBIFACU na Mkurungezi wa Maendeleo ya Kahawa - DCDO, Bw.Kajiru Kiseng, akiwa na Mkurugenzi mkuu Bw.Jamali,{hayupo pichani} Nowemba 2020} wakiwa katika zoezi la ugawaji miche bora ya Kahawa kwa wakulima kupitia AMCOS.

Bodi ya Jahawa Tanzania - TCB, inaendelea na zoezi la kuwatembelea wakulima na baadhi ya vyama vya msingi AMCOS, ili kuhakikisha zoezi la ugawaji miche bora na ya kisasa limefanikiwa kwa kiwango kikubwa ili kufikia malengo ya uzalishaji wa tani Zaidi ya 300,000 ifikapo mwaka 2025.

Uongozi wa Bodi ya Kahawa Tanzania - TCB, unawatakia wafanyakazi na wadau wa Kahawa kote Duniani, heri ya maadhimisho me...
26/04/2023

Uongozi wa Bodi ya Kahawa Tanzania - TCB, unawatakia wafanyakazi na wadau wa Kahawa kote Duniani, heri ya maadhimisho mema ya miaka 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

TCB ina ahidi kuendelea kusimamia,kuratibu na kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima na wadau wote wa KAHAWA nchini.

25/04/2023

Bodi ya kahawa nchini - TCB, imeandelea na zoezi la ugawaji miche bora na ya kisasa kwa wakulima wa Kahawa kupitia vyama vyao vya msingi - AMCOS.

24/04/2023

Katibu tawala wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Lodrick Lazaro Mpogoro, akifanya utambulisho wa viongozi meza kuu na wadau wengine mbele ya mgeni rasmi na mwenyekiti wa mkutano huo, Mh.Homera, ambaye amewakilishwa na Mh.Mkuu Wilaya ya Mbeya mjini Beno Malisa.

Mkuto huo umefanyika tarehe 19 Aprili, 2023, katika ukumbi mpya wa mikutano uliopo jengo la mkuu wa mkoa wa Mbeya.

24/04/2023

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya mjini, Mh.Beno Malisa,akimkaimu Mkuu wa mkoa wa Mbeya, ambaye ndio aliyekuwa mgeni rasmi na mwenyekiti wa mkutano huo, akifungua mkutano wa wadau wa KAHAWA kanda ya Mbeya jana Aprili 19.2023.

Aidha amewataka wadau wote wa Kahawa kanda ya Mbeya, kufuata taratibu za kilimo cha kisasa kinachozingatia ubora.

Mh.Beno Malisa amesema wakulima wanapaswa kutambua kilimo bora chenye tija ndio kinachoweza kuongeza thamani ya zao la kahawa nakuifanya kuongeza thamani ya bei duniani.

Ameongeza kuwa zao la kahawa zamani mkoani Kilimanjaro wakati alikuwa walikuwa wakiambiwa na wazazi wao kuwa wasichezee kahawa ina madhara kiafya, ila lengo la wazee hao ilikuwa ni kutunza thamani ya kahawa na kuifanya kuwa zao kuu la biashara lililowapa uchumi mzuri na imara.

Mwisho amewataka maafisa ugani kuhamishia ofisi zao mashambani ili kuwasadia wakulima kufanya kilimo bora cha kahawa kuanzia hatua za awali hadi kuhifadhiwa ghalani tayari kwa kuuzwa.

Mh.Beno ameitaka Bosi ya Kahawa Tanzania-TCB, kuongeza nguvu zaidi katika kugawa miche bora ya kawaha kwa wakulima wa kanda ya Mbeya na mkoa wa SONGWE na Mbozi.

24/04/2023

Uongozi wa Bodi ya kahawa - TCB, umeahidi neema nyingine kwa wakulima na wadau wa KAHAWA nchini, muda si mrefu itaendelea na zoezi la ugawaji wa miche bora ya kahawa.

Hayo yamesemwa na Bw.Shamba mkuu wa Bodi hiyo, Ndg Kajiru, wakati akitolea ufafanuzi wa moja ya hoja na maswali kutoka kwa wadau wa mkutano huo kuhusu miche bora.

Aidha Bw.Kajiru aliyemuwakilisha mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Ndugu Primus Kimaryo, amesema kuwa bosi tayari imeshafanyia kazi changamoto hiyo na tayari imeshaanza utekelezaji wake na inatarajia hivi karibuni kuendelea na zoezi hilo la ugawaji wa miche bora na ya kisasa, kwa wakulima kupitia vyama vyao vya msingi-Amcos, hivyo ni suala la muda tu ila watagawa kulinagana na mahitaji ya mwanzo wa msimu.

Ameongeza kuwa Bodi ya Kahawa, imeendelea na zoezi la ugawaji miche bure kwa wakulima wa kahawa nchini ikiwa ni moja ya jitihada za kuongeza uzalishaji kufikia tani 300,000 mwaka 2025.

Hatua hii inalenga kufikia lengo la uzalishaji na ugawaji miche milioni 20 kila mwaka, ambapo hadi kufikia Aprili 2023 jumla ya miche zaidi ya 8,784,146, imegawiwa katika msimu wa 2022/2023.

Mwisho ametoa wito kwa wakulima wa Kahawa kote nchini, kufuata kanuni na misingi ya Wizara ya Kilimo, ambapo amewashauri kupeleka mazao yao kwenye AMCOS, ili kupata bei nzuri na elekezi.

Amewaahidi kuwa Bodi itazidi kuboresha mfumo na mazingira wezeshi kwa wakulima na wadau nchini, ikiwemo kutangaza bei za kahawa za kidunia kila siku kupitia vyombo mbalimbali vya habari hasa kupitia mitandao yake ya kijamii.

Address

P. O. Box 732
Moshi
25101

Opening Hours

Monday 07:30 - 16:00
Tuesday 07:30 - 16:00
Wednesday 07:30 - 16:00
Thursday 07:30 - 16:00
Friday 07:30 - 16:00

Telephone

+255272752324

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Coffee Board posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tanzania Coffee Board:

Share