Chalinze District Council

Chalinze District Council Facebook Official page for Chalinze District Council

Kila la Kheri Wanafunzi wa kidato cha Nne katika mtihani wenu wa Taifa 2025
17/11/2025

Kila la Kheri Wanafunzi wa kidato cha Nne katika mtihani wenu wa Taifa 2025

Madiwani wa Pangani Waipongeza Halmashauri ya Chalinze kwa Miradi ya Mapato ya NdaniNa John Mlyambate,ChalinzeKamati ya ...
11/06/2025

Madiwani wa Pangani Waipongeza Halmashauri ya Chalinze kwa Miradi ya Mapato ya Ndani

Na John Mlyambate,Chalinze

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Pangani imefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze, mkoani Pwani, kwa lengo la kujifunza mbinu mbalimbali za ukusanyaji wa mapato ya ndani na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotokana na mapato hayo. Ziara hiyo ilifanyika hivi karibuni na ilijumuisha madiwani pamoja na wataalam kutoka Halmashauri ya Pangani.

Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, Mheshimiwa Akida Omari Bahorera, ambaye aliongozana na wajumbe wa k**ati yake pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo. Katika ziara hiyo, walitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayosimamiwa na Halmashauri ya Chalinze kwa kutumia mapato ya ndani.

Miongoni mwa miradi waliyoitembelea ni pamoja na ujenzi wa vyumba 80 vya maduka katika stendi ya mabasi ya Halmashauri iliyopo katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Chalinze, pamoja na soko la Bwilingu. Miradi hii inatajwa kuwa mfano bora wa matumizi ya mapato ya ndani katika kuboresha huduma kwa wananchi na kuongeza vyanzo vya mapato kwa halmashauri.

Aidha, madiwani hao walitembelea vizuia vya kukusanyia mapato ya ndani vilivyopo maeneo ya Lugoba na Kinzagu. Katika maeneo hayo walipata fursa ya kujifunza kwa kina mfumo wa ukusanyaji wa mapato, ikiwemo matumizi ya teknolojia na usimamizi wa vyanzo vya mapato ili kuhakikisha halmashauri inajitegemea kifedha.

Baada ya ziara hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Pangani, Mheshimiwa Bahorera, alitoa pongezi kwa Halmashauri ya Chalinze kwa ubunifu na ufanisi katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya ndani. Alisisitiza kuwa Pangani imejifunza mambo mengi yenye manufaa ambayo wataenda kuyatekeleza katika halmashauri yao ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Hakika tumejifunza mengi kutoka kwenu. Tunahakikisha mazuri haya tuliyoyaona tunayachukua na kuyatekeleza kwa manufaa ya wananchi wa Pangani na Watanzania kwa ujumla,” alisema Mheshimiwa Bahorera kwa niaba ya wenzake.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Pangani kujifunza na kuboresha mifumo yake ya ndani ya mapato pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo endelevu na kuboresha maisha yao kwa kutumia rasilimali zilizopo.

DC Ndemanga Aongoza Kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa LisheNa John MlyambateChalinze, Juni 10, 2025 – Mkuu...
10/06/2025

DC Ndemanga Aongoza Kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe
Na John Mlyambate

Chalinze, Juni 10, 2025 – Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Mheshimiwa Shaibu Ndemanga, ameongoza kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa robo ya tatu, kilichofanyika leo katika ukumbi wa masafa wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze. Kikao hicho kililenga kupitia hatua zilizochukuliwa na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa mkataba huo kati ya Mkurugenzi Mtendaji na watendaji wa kata.

Katika kikao hicho, Afisa Lishe wa halmashauri aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mkataba huo kuanzia ngazi ya kijiji hadi kata, huku akiainisha maeneo yaliyoimarika na changamoto zilizopo. Taarifa hiyo ilipokelewa kwa mapokezi chanya na wajumbe wa kikao, ambao walieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha juhudi za kupambana na utapiamlo kwenye jamii.

Akizungumza wakati wa kikao, Mheshimiwa Ndemanga alipongeza jitihada zilizofanyika hadi sasa, akieleza kuwa utekelezaji wa mkataba wa lishe umeonyesha mafanikio makubwa kwa kuzingatia mwongozo wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Aliwataka watendaji wa kata kuongeza juhudi na ubunifu katika kuwafikia wananchi kwa elimu ya lishe.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa halmashauri hiyo, Bi Atuganile Chisunga, aliwasilisha taarifa ya kitengo chake kuhusu hali ya lishe katika jamii na mikakati ya kuimarisha lishe kwa makundi mbalimbali ikiwemo watoto, wajawazito, na wazee. Alieleza kuwa kitengo hicho kinaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutoa elimu ya lishe na ushauri wa kiafya.

Katika maelezo yake ya hitimisho, Mheshimiwa Ndemanga aliwataka maafisa lishe na watendaji wa kata kuendelea kutoa elimu ya lishe kwa jamii kwa bidii na bila kuchoka, akisisitiza kuwa mkataba wa lishe hautakuwa na maana k**a hautatekelezwa kwa vitendo hadi kwenye ngazi ya kaya.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa idara ndani ya halmashauri, wakiwemo maafisa maendeleo ya jamii, maafisa afya, na maafisa mipango, ambao walitoa michango yao kuhusu namna bora ya kushirikiana katika utekelezaji wa mkataba huo.

Kwa ujumla, kikao kimekuwa jukwaa muhimu la kupima mafanikio, kushirikiana uzoefu, na kuweka mikakati mipya ya kuhakikisha lishe bora kwa wananchi wa Chalinze inafikiwa na kudumu.

MKUTANO MKUU WA KIJIJI CHA TUKAMISASA WAAZIMIA MWENYEKITI KUPISHA UCHUNGUZINa John MlyambateKijiji cha Tukamisasa, wilay...
10/06/2025

MKUTANO MKUU WA KIJIJI CHA TUKAMISASA WAAZIMIA MWENYEKITI KUPISHA UCHUNGUZI
Na John Mlyambate
Kijiji cha Tukamisasa, wilayani Bagamoyo, kimetawaliwa na mvutano mkubwa baada ya Mkutano Mkuu wa Kijiji hicho, uliofanyika hivi karibuni, kuazimia Mwenyekiti wa Kijiji, Bwana Ramadhani Zahaki, asimame kazi ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazomkabili.

Mkutano huo uliitishwa na Mwenyekiti Zahaki mwenyewe kwa lengo la kujadili na kupokea kero mbalimbali za wananchi, na kufanyika katika ofisi ya kijiji hicho mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mheshimiwa Shaibu Ndemanga.

Katika kikao hicho, wananchi walipata nafasi ya kueleza matatizo yao hadharani, ambapo Bwana Malaki Mamungiti, ambaye ni Mwenyekiti wa wafugaji wa kijiji hicho, aliibuka na tuhuma nzito dhidi ya Mwenyekiti Zahaki, akidai amekuwa akijimilikisha ardhi ya kijiji kinyume cha sheria.

Malaki alidai kuwa Mwenyekiti huyo anamiliki zaidi ya ekari 500 ambazo anazidai kuwa ni za familia yake, akitumia nafasi yake vibaya kwa maslahi binafsi, jambo linalokiuka taratibu za kisheria na kiutawala.

Mbali na suala la ardhi, Malaki alieleza kuwa Mwenyekiti huyo amekuwa akiwaingiza wawekezaji kwenye vitega uchumi vya kijiji bila idhini ya vikao halali, huku akijipatia mapato yasiyo halali bila uwazi au ufuatiliaji wa fedha hizo.

Wananchi wengine pia walitoa tuhuma mbalimbali, akiwemo Mzee Mathias Mkundi, ambaye alisema kuwa Mwenyekiti Zahaki hana ushirikiano na Mtendaji wa Kijiji pamoja na Halmashauri ya Kijiji, hali inayozorotesha utendaji wa serikali ya kijiji.

Mzee Mkundi alieleza kuwa hakujawahi kufanyika kikao chochote cha kisheria tangu Mwenyekiti huyo aingie madarakani, hali inayomnyima mamlaka na sauti ya wananchi katika maamuzi ya kijiji.

Kwa upande wake, Mzee Ismail Lugoma, alieleza kuwa Mwenyekiti hajawahi kusoma mapato na matumizi ya kijiji hadharani, licha ya kijiji hicho kuwa na vyanzo vingi vya mapato vinavyoendelea kukusanya fedha.

Mzee Lugoma alipendekeza kuwa ni busara kwa Mwenyekiti Zahaki kupisha uchunguzi ili ukweli ubainike na hatua stahiki zichukuliwe, kwa kuwa hali ya sasa inarudisha nyuma maendeleo ya kijiji hicho.

Wananchi waliunga mkono hoja hiyo kwa kauli moja, wakimtaka Mkuu wa Wilaya kuingilia kati na kuhakikisha tume huru inaundwa kuchunguza tuhuma hizo, kwa lengo la kulinda maslahi ya umma na kurejesha imani ya wananchi kwa uongozi.

Kutokana na hali hiyo, Mkutano Mkuu wa Kijiji cha Tukamisasa uliamua rasmi kwamba Mwenyekiti Zahaki asimame kazi kwa muda, hadi uchunguzi kamili ufanyike, na walimkabidhi rasmi ombi hilo Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo.

Mkuu wa Wilaya, Mheshimiwa Shaibu Ndemanga, alikubaliana na ombi hilo na kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze, ambaye aliiwakilishwa katika kikao hicho na Afisa Utumishi, kuunda tume ya uchunguzi mara moja.

Tume hiyo itapitia na kuchunguza tuhuma zote zilizotolewa na wananchi, zikiwemo za matumizi mabaya ya madaraka, ubaguzi, ukabila, ubadhirifu wa mali ya kijiji na uvunjaji wa taratibu za kiutawala.

Mkuu wa Wilaya alisisitiza kuwa tume hiyo itafanya kazi kwa weledi na itatoa ripoti ya uchunguzi mbele ya Mkutano Mkuu wa Kijiji cha Tukamisasa kwa ajili ya hatua zaidi, kuhakikisha haki na uwajibikaji vinazingatiwa.

Wananchi wa Tukamisasa walionyesha matumaini kuwa hatua hiyo ya kusimamishwa kwa Mwenyekiti Zahaki itasaidia kurejesha utawala bora na uwazi katika uongozi wa kijiji chao.

Ujenzi wa vyumba vya kufanyia biashara 80 vinavyojengwa katika stendi ya Chalinze ni mahitaji ya wananchi ya muda mrefu ...
06/06/2025

Ujenzi wa vyumba vya kufanyia biashara 80 vinavyojengwa katika stendi ya Chalinze ni mahitaji ya wananchi ya muda mrefu na smradi huu unatekelezwa kwa mapato ya ndani ya halmadhauri kwa asilimia 100

EID AL ADHA
06/06/2025

EID AL ADHA

WAZIRI KIKWETE ATUA GENEVA KUSHIRIKI MKUTANO WA 113 WA ILOWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na ...
04/06/2025

WAZIRI KIKWETE ATUA GENEVA KUSHIRIKI MKUTANO WA 113 WA ILO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amewasili Jijini Geneva, Uswisi kushiriki Mkutano wa 113 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaoendelea katika Makao Makuu ya shirika hilo. Mkutano huo unahusisha nchi wanachama kutoka kote duniani kujadili masuala ya kazi na ajira.

Katika mkutano huo, Mhe. Ridhiwani anatarajiwa kutoa taarifa ya utekelezaji wa Tanzania kuhusu viwango vya kimataifa vya kazi, pamoja na hatua mbalimbali ambazo nchi imechukua katika kuhakikisha haki na usalama wa wafanyakazi zinaimarishwa. Aidha, atashiriki mijadala ya nchi wanachama kuhusu utekelezaji wa mpango kazi na bajeti ya uendeshaji wa ILO kwa mwaka 2026/2027.

Kabla ya kushiriki kwenye mkutano huo, Mhe. Ridhiwani ametembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Uswisi zilizopo Geneva na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania, Mhe. Dkt. Abdallah Possi ambaye pia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. Mazungumzo yao yalilenga kuimarisha ushirikiano na maandalizi ya ushiriki wa Tanzania katika mkutano huo muhimu.

Aidha, Waziri Kikwete alipata fursa ya kukutana na Balozi Dkt. Hoyce Temu pamoja na watendaji mbalimbali wa Ubalozi huo. Katika mazungumzo hayo, walijadili kwa kina namna Tanzania inavyoweza kutumia jukwaa la ILO kuonesha mafanikio na changamoto katika sekta ya kazi na ajira.

Katika hatua nyingine, Mhe. Ridhiwani alitumia nafasi hiyo kumpongeza Balozi Dkt. Possi kwa kazi nzuri anayoifanya kupitia Ofisi ya Ubalozi, ikiwemo kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika majukwaa ya kimataifa na kuhakikisha sauti ya nchi inasikika vyema katika mijadala ya Umoja wa Mataifa na mashirika ya kimataifa.

Mkutano wa 113 wa ILO ni jukwaa muhimu linalowakutanisha viongozi, wataalamu na wadau wa kazi kutoka mataifa mbalimbali duniani, ambapo pamoja wanajadiliana kuhusu mustakabali wa kazi, haki za wafanyakazi na ajira zenye staha, sambamba na kupanga mikakati ya kisera inayolenga kuimarisha ustawi wa jamii kupitia kazi.

NAIBU KATIBU MKUU TAMISEMI APONGEZA UTEKELEZAJI WA SEKTA YA AFYA CHALINZENa John MlyambateNaibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rai...
03/06/2025

NAIBU KATIBU MKUU TAMISEMI APONGEZA UTEKELEZAJI WA SEKTA YA AFYA CHALINZE
Na John Mlyambate

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia masuala ya Afya, Profesa Tumaini Joseph Nagu, leo amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze akiwa ameambatana na timu ya wataalamu kutoka TAMISEMI kwa lengo la kukagua na kujionea maendeleo ya sekta ya afya katika halmashauri hiyo.

Profesa Nagu alianza ziara yake kwa kutembelea Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze kisha kuelekea katika Kituo cha Afya Chalinze ambapo alikagua miundombinu mbalimbali ikiwemo majengo ya huduma za afya na vifaa tiba vinavyotumika katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika ukaguzi wake, Naibu Katibu Mkuu alionesha kuridhishwa na hali ya miundombinu ilivyoboreshwa kwa ushirikiano kati ya serikali kuu na mapato ya ndani ya halmashauri. Alisema hatua hiyo inaakisi dhamira ya serikali ya awamu ya sita katika kuboresha huduma za afya nchini kwa lengo la kumrahisishia mwananchi kupata huduma bora karibu na makazi yake.

Profesa Nagu alipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wagonjwa waliokuwa wakipata huduma kituoni hapo, ambapo walieleza kufurahishwa na ubora wa huduma na kuwepo kwa vifaa tiba vya kisasa vinavyowezesha huduma kutolewa kwa haraka na kwa ufanisi.

Katika ziara hiyo, Profesa Nagu pia alitembelea na kukagua Duka la Dawa la Jamii lililopo katika Kituo cha Afya Chalinze. Alilipongeza duka hilo kwa kuwa la kisasa na lenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi dawa, jambo linalosaidia wananchi kupata dawa kwa wakati bila usumbufu.

Msafara huo ulielekea pia katika Hospitali ya Wilaya ya Chalinze iliyopo Msoga, ambapo Profesa Nagu alikagua Kituo cha Dharura cha Matibabu (EMD) pamoja na majengo mbalimbali ya hospitali hiyo. Alifurahishwa na kiwango cha ujenzi wa miundombinu ya kisasa yenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya utoaji wa huduma bora.

Akizungumza na watumishi wa sekta ya afya katika halmashauri hiyo, Profesa Nagu aliwapongeza kwa juhudi kubwa wanazozifanya katika kuwahudumia wananchi licha ya changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo kazini. Alisema serikali inatambua mchango wao na itaendelea kuboresha mazingira ya kazi.

Aliwahimiza watumishi hao kuendeleza moyo wa uzalendo kwa kutoa huduma kwa upendo na uadilifu kwa wananchi, pamoja na kuitunza miundombinu na vifaa tiba ili viweze kudumu kwa matumizi ya muda mrefu.

Profesa Nagu alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita imejipanga kikamilifu kuhakikisha kila mtanzania anapata huduma bora za afya, na kwamba Chalinze ni mfano wa mafanikio ya utekelezaji wa mpango huo kutokana na usimamizi mzuri wa viongozi wa halmashauri hiyo.

JAMII YAASWA KUZINGATIA MATUMIZI YA KIASI KATIKA VYAKULA VYENYE MAFUTA, SUKARI NA CHUMVIJamii imetakiwa kuzingatia matum...
03/06/2025

JAMII YAASWA KUZINGATIA MATUMIZI YA KIASI KATIKA VYAKULA VYENYE MAFUTA, SUKARI NA CHUMVI

Jamii imetakiwa kuzingatia matumizi ya kiasi katika ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, sukari nyingi na chumvi kupita kiasi, ili kuepuka hatari ya kupata magonjwa sugu yasiyoambukiza.Wito huo umetolewa leo na Afisa Lishe wa Halmashauri ya Chalinze, Lucas Eliakim Molell, wakati akizungumza katika kipindi cha Gumzo Leo kinachorushwa na Chalinze FM kila Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 4:00 hadi 7:00 mchana.

Aidha Molell amesema ulaji wa chumvi nyingi huongeza hatari ya shinikizo la damu, ugonjwa wa moyo na kiharusi. Aidha, alibainisha kuwa matumizi ya sukari kupita kiasi yanachangia kuongezeka kwa uzito wa mwili, kuibuka kwa ugonjwa wa kisukari pamoja na matatizo ya moyo.

Pia afisa lishe aliongeza kuwa jamii inapaswa kuepuka unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi k**a soda, juisi bandia, pamoja na ulaji wa vitafunwa k**a keki na p**i. Badala yake, ameshauri watu kutumia matunda halisi na kunywa maji ya kutosha k**a njia bora ya kujikinga na magonjwa hayo.

Vile vile, Molell amesisitiza umuhimu wa kuepuka ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, hasa yale yanayoganda, akieleza kuwa vyakula hivyo huweza kusababisha ongezeko la uzito, kuziba kwa mishipa ya damu, na hatimaye kusababisha magonjwa ya moyo. Ametoa ushauri kwa jamii kutumia mafuta yanayotokana na mimea ambayo ni salama zaidi kwa afya.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeweka miongozo madhubuti kuhusu ulaji wa vyakula vyenye chumvi nyingi, mafuta mengi, na sukari nyingi ili kupunguza hatari ya magonjwa yasiyoambukiza k**a shinikizo la damu, kisukari, magonjwa ya moyo, na kiharusi

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAFANYA KIKAO KUJADILI MAPATO NA MATUMIZI YA APRILI 2025Chalinze, PwaniKamati ya Fed...
30/05/2025

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAFANYA KIKAO KUJADILI MAPATO NA MATUMIZI YA APRILI 2025
Chalinze, Pwani

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze imefanya kikao chake leo kujadili taarifa ya mapato na matumizi kwa mwezi Aprili 2025, kikao kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mheshimiwa Hassani Mwinyikondo. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya mwezi huo na kuweka mikakati ya kuboresha hali ya kifedha ya Halmashauri.

Wajumbe wa k**ati hiyo wakiwemo madiwani na wataalamu kutoka idara mbalimbali walipitia kwa kina taarifa za mapato ya ndani, ikiwa ni pamoja na vyanzo vya mapato vilivyokusanywa na changamoto zilizojitokeza katika ukusanyaji wake. Aidha, walijadili matumizi yaliyofanyika na kujiridhisha k**a yamezingatia mpango wa bajeti ulioidhinishwa na Baraza la Madiwani.

Katika mjadala huo, baadhi ya changamoto zilizobainishwa ni pamoja na ucheleweshaji wa mapato kutoka kwa baadhi ya vyanzo, upungufu wa vifaa vya ukusanyaji, pamoja na uelewa mdogo wa baadhi ya wananchi kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na tozo mbalimbali. Hali hii ilipelekea kupungua kwa mapato yaliyokusanywa ikilinganishwa na malengo ya mwezi Aprili.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti Mwinyikondo, k**ati imeazimia kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya mapato vya ndani, kutoa elimu kwa wananchi kuhusu wajibu wao wa kulipa kodi, pamoja na kuongeza uwazi na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma. Alisisitiza kuwa Halmashauri itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wakati.

Kikao hicho ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya kisheria ya k**ati hiyo ya kuhakikisha Halmashauri inatekeleza mipango yake ya maendeleo kwa uwazi, ufanisi na kwa kuzingatia vipaumbele vya wananchi wa Chalinze. Kamati hiyo hufanya vikao vya tathmini kila mwezi ili kuhakikisha mwenendo wa kifedha unaenda sambamba na matarajio ya bajeti na malengo ya maendeleo.

HALMASHAURI YA CHALINZE YATEMBELEWA NA WAWEKEZAJI WA NYUMBA                   Na John Mlyambate,Chalinze, PwaniMkurugenz...
30/05/2025

HALMASHAURI YA CHALINZE YATEMBELEWA NA WAWEKEZAJI WA NYUMBA
Na John Mlyambate,Chalinze, Pwani

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze leo amepokea ujumbe wa wawekezaji kutoka Chama cha Ushirika cha Ujenzi wa Nyumba Mwenge waliokuja kuonesha nia ya kuwekeza kwenye ujenzi wa makazi katika halmashauri hiyo.

Ujumbe huo umeongozwa na Mtendaji Mkuu wa chama hicho, Bwana Thomas Mosha, ambaye amesema lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha rasmi kwa uongozi wa halmashauri pamoja na kufungua milango ya ushirikiano wa uwekezaji katika sekta ya makazi. Ameeleza kuwa chama hicho kimejipanga kujenga nyumba za kisasa kwa ajili ya wananchi na watumishi katika maeneo ya Chalinze.

Katika mazungumzo yao na Mkurugenzi Mtendaji, wawekezaji hao wameeleza kuwa wako katika hatua za awali za kutambua na kukagua maeneo yanayofaa kwa ajili ya uwekezaji huo, pamoja na kujiridhisha juu ya usalama wa maeneo hayo na miundombinu iliyopo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze amewakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia ushirikiano wa karibu kutoka kwa wataalamu wa halmashauri katika kila hatua ya mchakato huo. Ameeleza kuwa halmashauri inafurahia kuona wawekezaji wakionesha nia ya kuchangia maendeleo ya makazi kwa wananchi wake.

Uwekezaji huo unatarajiwa kusaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa nyumba za makazi katika mji wa Chalinze ambao unaendelea kukua kwa kasi, pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi wa eneo hilo.

27/05/2025

Madiwani wameshuhudia ng’ombe mwenye uzigo wa kg 732 katika shamba la mifubo la ASAS kagika Manispaa ya Iringa

Address

Ofisi Ya Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri Ya Wilaya Ya Chalinze114 Barabara Ya Morogoro 61383 CHALINZE
Pwani

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chalinze District Council posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Chalinze District Council:

Share