23/04/2019
SHIRIKA LA KUHUDUMIA VIWANDA VIDOGO, SIDO SIMIYU
UTANGULIZI
Shirika la kuhudumia viwanda vidogo, SIDO ni shirika la umma lililoanzishwa kwa sheria ya Bunge No.28 ya mwaka 1973. Shirika hili liko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara na linasimamiwa na bodi ya shirika ambayo huteuliwa na serikali, ambapo mwenyekiti huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wajumbe wa bodi huteuliwa na Waziri mwenye dhamana na viwanda. Mtendaji Mkuu wa shughuli za kila siku za shirika ni Mkurugenzo Mkuu ambaye anasaidiwa na wakurugenzi wanne k**a ifuatavyo:
1. Mkurugenzi wa Utawala na Fedha
2. Mkurugenzi wa Uendelezwaji Teknolojia na Viwanda
3. Mkurugenzi wa Mafunzo na Tawala za Mikoa
4. Mkurugenzi wa Masoko na Uwekezaji.
SIDO ina ofisi katika kila mkoa wa Tanzania bara na ofisi hizi ziko chini ya Mkurugenzi Mkuu kupitia kwa Mkurugenzi wa mafunzo na tawala za Mikoa.
Kwenye ngazi ya Mikoa kuna watalaam k**a ifuatavyo:
Meneja wa Mkoa ambaye ndiyo msimamizi wa kazi zote, mkoani kwa niaba ya mkurugenzi mkuu.
Chini yake kuna wataalamu k**a ifuatavyo:
i. Afisa Ufundi
ii. Afisa Mwendeleza biashara na mafunzo
iii. Afisa Mikopo
iv. Mhasibu
v. Meneja wa karakana (kwa baadhi ya mikoa)
Ofisi ya SIDO Simiyu imezinduliwa rasmi tarehe 02/01/2018 na Disemba mwaka 2018, SIDO Simiyu ilihamia kwenye jengo lake la ofisi lililoko eneo la viwanda Isanga, mjini Bariadi.
HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA SIDO SIMIYU
1. UENDELEZWAJI WA TEKNOLOJIA:
• Ushauri wa kiufundi: jinsi ya kupata teknolojia na mashine mbalimbali, mpangilio wa jengo la kiwanda na mazingira yake, mahitaji muhimu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda, namna ya kuboresha kiwanda chako, uzalishaji wa tija nk.
• Kuwahilisha teknolojia mbalimbali
• Uinjikaji wa mashine (machines installation)
• Kutafuta teknolojia mbalimbali hapa ndani na nje ya nchi na kuifikisha teknolojia hizo kwa wajasiriamali wenye uhitaji
• Kutoa mafunzo za kuzalisha bidhaa mbalimbali: uzalishaji bidhaa za ngozi, kusindika ngozi, usindikaji bidhaa za kilimo, batiki, sabuni na viosheo, mishumaa, chaki nk.
2. UENDELEZWAJI BIASHARA:
• mafunzo ya biashara yanatolewa ili kuwawezesha wajasiriamali kuendesha biashara zao kitaalam: jinsi ya kupata wazo la biashara, jinsi ya kuanza biashara, jinsi ya kuendeleza biashara, uandikaji wa mpango wa biashara, masoko, vyanzo vya mitaji nk.
• Kuunganishwa na taasisi za kihuduma k**a TBS, TFDA, GS1, BRELA nk.
• Uimarishaji vikundi
• Usajili wa majina ya biashara na kampuni na kupata mistari milia (barcodes)
3. HUDUMA ZA MASOKO NA UWEKEZAJI:
• SIDO Simiyu ina eneo la ekari 25 katika eneo la viwanda Isanga, mjini Bariadi na tayari ofisi imejengwa na ipo kwenye hatua za kuanza ujenzi wa majengo kwa ajili viwanda eitha, wajasiriamali wana nafasi pia kuyajenga majengo ya viwanda na kuyatumia kwa muda mpaka warejeshe hela zao na kisha kuendelea kuyatumia kwa kulipa kodi. Wajasiriamali wanakaribishwa kuwekeza kwenye viwanda vya mazao ya kilimo(pamba, alizeti na karanga, mazao ya nafaka, dengu/mbaazi/choroko nk), madini, chuma/bati, vipuri, mashine nk).
• Tunandaa maonyesho ya bidhaa za wajasiriamali wa kitanzania ambapo maonyesho ya kanda ya Ziwa yatafanyika Shinyanga Mei na Maonyesho ya SIDO kitaifa yatafanyika Geita, Octoba.
4. HUDUMA YA KIFEDHA: Tunatoa Mikopo kwa ajili ya biashara ndogo na za kati na kipaumbele chetu ni uzalishaji/viwanda.
KARIBUNI NYOTE KWA HUDUMA ZILIZOTUKUKA
MAWASILIANO:
MENEJA WA SIDO,
MKOA WA SIMIYU,
P.O.BOX 379,
BARIADI
MOBILE:
0754800500 - Meneja SIDO Mkoa
0754093932 - Afisa Ufundi wa SIDO Mkoa
0754315585 - Afisa Mwendeleza Biashara SIDO Mkoa