21/10/2023
Chama cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Sumbawanga kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga kimeendesha Bonanza kubwa la michezo mbalimbali katika Shule ya Sekondari Kizwite.
Bonanza hilo lililohusisha michezo ya kukimbia kwenye magunia, kuvuta kamba, mpira wa pete na mpira wa miguu lilifanyika tarehe 20 Oktoba, 2023 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kizwite kwa kuwakutanisha wanafunzi mashabiki wa Simba na Yanga wasichana na wavulana katika michezo hiyo.
Akizungumza katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bonanza hilo lilioitwa Samia Day Bonanza Mgeni Rasmi Comrade Kombat ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kalambo aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alieleza kwamba watoto(wanafunzi) ndio hazina ya Taifa kwenye nyanha zote za maendeleo Nchini ikiwemo michezo hivyo lazima Serikali kupitia kwenye Shule iendelee kujenga misingi ya kuhakikisha wanafunzi wanashiriki kwenye michezo kikamilifu ili kuwaweka sawa kimwili, kujenga mahusiano, kuboresha afya zao na kuendeleza vipaji vyao.
Komba alikishukuru Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia kwa Katibu Mkuu wa Chama hicho Taifa Comrade Chongolo kwa kutoa zawadi ya jezi na kuelekeza kuwepo kwa bonanza na mashindano ya michezo alipotembelea katika Shule hiyo ya Sekondari Kizwite akiwa katika Ziara ya Ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Chama hicho mwanzoni mwa mwezi Oktoba 2023.
Aidha akizungumza kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi Mkoa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa Comrade Maufi ambaye alikuwa Mgeni Rasmi mwenza, alieleza umuhimu wa michezo kwa wanafunzi k**a inavyoelezwa kwenye Ilani ya Chama hicho na kuitaka Serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya michezo katika Mkoa na kuhakikisha ushiriki wenye tija wa wanafunzi katika Sekta hiyo.