24/12/2018
THAMANI ya mwanadamu ni ndogo sana imeambatanishwa kwenye pumzi,na hii pumzi kazi yake kwa mwanadamu huwa ni kumpeleleza kwa kila TENDO jema ama baya analolitenda hii ikiwa ni kwa siri ama kwa uwazi!...
Hebu leo tena tuujue huu ukweli ninaokuletea online kwenye madhabahu huru ya FOCOAA2™.
Tupate PICHA ya ukweli wenyewe Hapa...Mithali 20:29"pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake."
+
Waebrania 4:13"wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake,lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu".
Mwenye kuzijua siri za mwanadamu kwa hali zote ni MUNGU tu peke yake kwa sababu yeye ndiye mwenye dhamana ya uhai wa mwanadamu!
Siri zote huitwa siri zikiwa pa mwanadamu lakini siri huwa si siri zikiwa mbele za MUNGU ambapo huitwa "utupu".
Maana ya utupu kwa lugha yakinifu ni "kuwa WAZI".
Kazio la kuwa wazi mbele za MUNGU ni hili hapa ...Mithali 15:3"Macho ya BWANA yako kila mahali; Yakimchunguza na ."
Haya ndiyo mambo murua ninayoyaweka wazi bila hata kuogopa cho chote!
Namaliza kwa kukiri hivi ..siri ni yako ila mbele za Mungu inaitwa ni utupu...
Na palipogemwa na mgema pameliwa na dumunzi.
Asanteni!
©Rev.Mdiujr® FOCOAA2™.