17/07/2026
HAFLA YA KUKABIDHI GARI LILILOAHIDIWA NA MHE: DKT SAMIA SULUHU HASSANI
Wananchi wa Wilaya ya Kilindi na wadau wote wa maendeleo mnakaribishwa kushiriki katika hafla ya kukabidhi gari lililoahidiwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Beatrice Shelukindo,
Hafla hiyo itakayofanyika kesho, tarehe 18 Julai 2026, Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mheshimiwa Hashim Mgandilwa, akishirikiana na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali pamoja na wadau wa sekta ya elimu.
Hafla hii ni kielelezo cha utekelezaji wa ahadi za Serikali na dhamira yake ya kuendelea kuimarisha mazingira ya utoaji wa elimu bora nchini. Kukabidhiwa kwa gari hilo kutaimarisha ufanisi wa shughuli za kiutawala na kielimu katika Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Beatrice Shelukindo,
Sambamba na kuendeleza juhudi za Serikali za kuboresha huduma za elimu kwa manufaa ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.
Wananchi wote mnakaribishwa kushuhudia tukio hili muhimu linaloakisi azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuendelea kuwaletea wananchi maendeleo kupitia utekelezaji wa ahadi zake.