Kilindi District Council

Kilindi District Council 🏛️ Karibu katika Ukurasa Rasmi wa Halmashauri ya Wilaya Kilindi
📍 Kilindi, Tanga - Tanzania
🌐https://kilindidc.go.tz
Makao Makuu ya Ofisi Songe

HAFLA YA KUKABIDHI GARI LILILOAHIDIWA NA  MHE: DKT SAMIA SULUHU HASSANIWananchi wa Wilaya ya Kilindi na wadau wote wa ma...
17/07/2026

HAFLA YA KUKABIDHI GARI LILILOAHIDIWA NA MHE: DKT SAMIA SULUHU HASSANI

Wananchi wa Wilaya ya Kilindi na wadau wote wa maendeleo mnakaribishwa kushiriki katika hafla ya kukabidhi gari lililoahidiwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Beatrice Shelukindo,

Hafla hiyo itakayofanyika kesho, tarehe 18 Julai 2026, Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mheshimiwa Hashim Mgandilwa, akishirikiana na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali pamoja na wadau wa sekta ya elimu.

Hafla hii ni kielelezo cha utekelezaji wa ahadi za Serikali na dhamira yake ya kuendelea kuimarisha mazingira ya utoaji wa elimu bora nchini. Kukabidhiwa kwa gari hilo kutaimarisha ufanisi wa shughuli za kiutawala na kielimu katika Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Beatrice Shelukindo,

Sambamba na kuendeleza juhudi za Serikali za kuboresha huduma za elimu kwa manufaa ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Wananchi wote mnakaribishwa kushuhudia tukio hili muhimu linaloakisi azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuendelea kuwaletea wananchi maendeleo kupitia utekelezaji wa ahadi zake.

ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA KILINDI KWA WANANCHIWananchi wa Jimbo la Kilindi mnakaribishwa kushiriki katika ziara ya Mbu...
14/07/2026

ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA KILINDI KWA WANANCHI

Wananchi wa Jimbo la Kilindi mnakaribishwa kushiriki katika ziara ya Mbunge wa Jimbo la Kilindi, Mhe. Salehe Mhando Mbwana itakayoanza rasmi tarehe 17 Julai 2026 katika maeneo mbalimbali ya jimbo.

Lengo la ziara hiyo ni kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na imani waliyoendelea kuonyesha pamoja na kusikiliza kero, maoni na mapendekezo ya wananchi ili kuendelea kuboresha utoaji wa huduma na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kilindi.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mbunge ataambatana na Wakuu wa Idara na Vitengo mbalimbali kutoka Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ambao watatoa ufafanuzi na kupokea changamoto zinazohusu sekta zao.

Wananchi wote mnahimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mikutano hiyo, kutoa maoni yenu na kushiriki katika kujenga maendeleo ya Jimbo

HONGERA KIDATO CHA SITA – KILINDI YANG'ARA KATIKA MATOKEO YA ACSEE!Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilin...
08/07/2026

HONGERA KIDATO CHA SITA – KILINDI YANG'ARA KATIKA MATOKEO YA ACSEE!

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi Ndg John K Mgalula inatoa pongezi za dhati kwa wanafunzi wote wa Kidato cha Sita kwa kufanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita.

Hongera za pekee ziwaendee walimu, wakuu wa shule, Maafisa Elimu, Kamati za Shule, wazazi pamoja na wadau wote wa elimu kwa ushirikiano, juhudi na kujitolea zilizowezesha kufikiwa kwa mafanikio haya makubwa.

Tunajivunia kuwa shule zote tatu zenye Kidato cha Sita katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ambazo ni Beatrice Shelukindo Girls Secondary School, Mafisa Secondary School na Mkindi Secondary School zimefaulisha kwa asilimia 100 ya wanafunzi waliofanya mtihani.

Mafanikio haya ni ushahidi wa ubora wa ufundishaji, usimamizi madhubuti na dhamira ya pamoja ya kuendelea kuinua kiwango cha elimu katika Wilaya ya Kilindi.

Hongera sana! Tuendelee kushirikiana kujenga taifa lenye wasomi, maadili na uzalendo.

Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi Wanawatakiwa , Wakulima , Wafanyabiashara na Wanan...
06/07/2026

Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi Wanawatakiwa , Wakulima , Wafanyabiashara na Wananchi wote wa Wilaya ya Kilindi na Tanzania kwa Ujumla Maadhimisho mema ya Sikukuu ya SabaSaba 2026

25/06/2026

DC HASHIM MGANDILWA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI HOSPTAL YA WILAYA KILINDI

22/06/2026

MKUU WA MKOA TANGA AIPONGEZA KILINDI KWA KUPATA HATI SAFI

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mheshimiwa Balozi Batilda Buriani, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kwa kupata Hati Safi katika usimamizi wa fedha za umma, akieleza kuwa mafanikio hayo ni kielelezo cha uwajibikaji, uwazi na usimamizi mzuri wa rasilimali za wananchi.

Akizungumza katika Baraza Maalum la Madiwani la Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) lililofanyika katika Ukumbi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, Mhe. Buriani amesisitiza umuhimu wa kujibu na kufunga hoja zote za ukaguzi kwa wakati ili kuendelea kuimarisha utendaji na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Aidha, amelitaka Baraza pamoja na watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanafanyia kazi maelekezo yote yanayotolewa na mamlaka za ukaguzi na usimamizi wa fedha za umma kwa lengo la kudumisha hadhi ya Halmashauri na kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI
19/06/2026

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe. Hashim Mgandilwa, leo Tarehe 18/06/2026 amekabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wil...
18/06/2026

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe. Hashim Mgandilwa, leo Tarehe 18/06/2026 amekabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, baada ya Mwenge wa Uhuru kukamilisha mbio zake katika Wilaya ya Kilindi.

Katika ziara hiyo, Mwenge wa Uhuru umeangazia, kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua jumla ya miradi saba (7) ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 860. Miradi hiyo inalenga kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kuchochea maendeleo ya wananchi wa Wilaya ya Kilindi.

Mwenge wa Uhuru unaendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa kuhamasisha uwajibikaji, uzalendo na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo ya Taifa.

18/06/2026

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndg. Wazo Michael Mwang'onda, amezindua Upanuzi wa Mradi wa maji katika kijiji cha Ludewa
Upanuzi huu unaenda kupunguza changamoto ya maji Ludewa na Vijiji vya jirani ndani ya Wilaya ya Kilindi

Address

Kilindi
Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilindi District Council posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share