Kilindi District Council

Kilindi District Council ๐Ÿ›๏ธ Karibu katika Ukurasa Rasmi wa Halmashauri ya Wilaya Kilindi
๐Ÿ“ Kilindi, Tanga - Tanzania
๐ŸŒhttps://kilindidc.go.tz
Makao Makuu ya Ofisi Songe

20/08/2026 Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO), Dkt. Petro Mboya amefungua mafunzo ya maoteo ya dawa na vifaa tiba yaliyofanyika...
20/08/2026

20/08/2026 Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO), Dkt. Petro Mboya amefungua mafunzo ya maoteo ya dawa na vifaa tiba yaliyofanyika katika Ukumbi Mkubwa wa Mikutano, Makao Makuu ya Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

Mafunzo hayo yamewashirikisha Waganga Wafawidhi na Wafamasia kutoka vituo 51 vya kutolea huduma za afya katika Wilaya ya Kilindi, kwa lengo la kuwajengea uwezo katika kufanya maoteo sahihi ya mahitaji ya dawa na vifaa tiba.

Akifungua mafunzo hayo, Dkt. Mboya amesisitiza umuhimu wa kufanya maoteo sahihi kwa kuzingatia mahitaji halisi ya vituo vya afya, ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa wakati na kuendelea kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Mafunzo haya ni sehemu ya jitihada za kuimarisha usimamizi wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya na kuhakikisha wananchi wa Wilaya ya Kilindi wanapata huduma bora za afya.

19/08/2026

SERIKALI YAAHIDI KUIMARISHA HUDUMA ZA KIJAMII AREA ''A, MSOMERA

19/08/2026 Serikali kupitia uongozi wa Wilaya ya Kilindi imeahidi kuendelea kuimarisha na kuboresha huduma za kijamii katika Area A, Msomera kufuatia ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe. Hashim Mgandilwa, ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Katika ziara , wananchi walipata fursa ya kueleza changamoto zao moja kwa moja, huku Mkuu wa Wilaya MH Hashim Mgandilwa akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kusikiliza wananchi, kuchukua hatua stahiki na kuhakikisha huduma muhimu za kijamii k**a shule , zahanati , maji na Barabara zinaimarika kwa manufaa ya wananchi.

Serikali ipo kwa ajili ya wananchi; kero zenu ni sehemu ya majukumu yetu na tutazifanyia kazi kwa kadiri ya uwezo na taratibu zilizopo.

TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MKOPO UNAOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU
18/08/2026

TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MKOPO UNAOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

17/08/2026

17/08/2026 JESHI LA ZIMAMOTO LAOTOA ELIMU YA USALAMA WA MOTO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI KWA VITENDO

14/08/2026
TANGAZO
13/08/2026

TANGAZO

Warsha ya Ushirikiano wa Wazazi na Walimu (UWAWA), chini ya Programu ya Shule Bora kwa mwaka 2026, imefanyika leo katika...
13/08/2026

Warsha ya Ushirikiano wa Wazazi na Walimu (UWAWA), chini ya Programu ya Shule Bora kwa mwaka 2026, imefanyika leo katika Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, ikiwakutanisha wadau mbalimbali wa elimu, wakiwemo Maafisa Elimu Kata, Wenyeviti wa Kamati za Shule pamoja na Walimu Wakuu.

Akifungua warsha hiyo, Ndugu Dastan J. Ntauka, Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ambaye pia alikuwa Mgeni Rasmi, amewataka wadau hao kuimarisha ushirikiano kati ya wazazi na walimu katika utekelezaji wa shughuli za elimu ya awali na msingi.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wa wazazi na jamii katika kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji, ili kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora na yenye tija.

09/08/2026

''TAMBUA SOKO ZALISHA KWA TIJA KUTEKELEZA DIRA 2050''

Address

Kilindi
Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilindi District Council posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share