Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar Ukurasa rasmi wa Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ)

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Makatibu...
02/07/2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Makatibu Wakuu ya Maandalizi ya AFCON 2027, Dkt. Jim Yonazi, ameowangoza Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ziara ya ukaguzi wa maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 hiyo Zanzibar.

Kamati ilitembelea Uwanja wa New Amaan Complex na uwanja mpya unaojengwa Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi, ambapo Dkt. Yonazi amesema maendeleo ya ujenzi na ukarabati yanaendelea vizuri ili kuhakikisha viwanja hivyo vinakidhi viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Amesema Serikali imeweka mikakati madhubuti inayohusisha ujenzi na ukarabati wa viwanja, uboreshaji wa miundombinu ya barabara, usalama na utangazaji wa vivutio vya utalii, kwa lengo la kuongeza uwekezaji, ajira na kuimarisha uchumi kupitia AFCON 2027.

"AFCON 2027 si mashindano ya soka pekee, bali ni fursa ya kuitangaza Tanzania kimataifa na kuchochea maendeleo ya sekta mbalimbali za uchumi," amesema Dkt. Yonazi.

Aidha, ametoa wito kwa sekta binafsi kutumia fursa zitakazotokana na mashindano hayo, hususan katika sekta za utalii, hoteli na huduma nyingine.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Bw. Salhina Mwita, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na ukarabati wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumiwa na timu shiriki na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Muungano ili kuhakikisha maandalizi ya AFCON 2027 yanafanikiwa kwa viwango vinavyohitajika.

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) linaipongeza Klabu ya Kikosi Cha Valantia Zanzibar kwa Ubingwa wa Ligi Kuu Za...
20/06/2026

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) linaipongeza Klabu ya Kikosi Cha Valantia Zanzibar kwa Ubingwa wa Ligi Kuu Zanzibar msimu wa 2025/2026.

Tunawatakia maandalizi mema ya msimu ujao, na katika Mashindano ya Kimataifa.

19/06/2026

Katibu Mtendaji Baraza la Taifa Ndugu Neema Msita akizungumzia ujio wa Wakaguzi kutoka CAF kukagua miundombinu ya ujenzi wa viwanja unaoendelea kwa ajili ya matayarisho ya AFCON2027.

19/06/2026

Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) Said Kassim Marine akingumzia muendelezo wa Ujenzi wa Viwanja kwa ajili ya matayarisho ya Mashindano ya Kombe la AFCON 2027.

Wakaguzi kutoka Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Bw. Lakshmikanth Karunanithi na Bw. Eduard Captan, wamefanya zia...
18/06/2026

Wakaguzi kutoka Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Bw. Lakshmikanth Karunanithi na Bw. Eduard Captan, wamefanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya viwanja vinavyotarajiwa kutumika katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027), na kueleza kuridhishwa na hatua ambayo mpaka sasa imefikiwa.

Katika ziara hiyo, wakaguzi hao walitembelea wa Kizimkazi na Uwanja wa Fumba Arena, ambapo walikagua maendeleo ya ujenzi wa viwanja hivyo na maeneo maalumu ya wageni na viongozi mashuhuri (VVIP), pamoja na sehemu zitakazotumika na wanahabari wakati wa mashindano.

Baada ya ukaguzi huo, wakaguzi wa CAF walieleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Ujenzi wa Viwanja hivyo pamoja na maendeleo ya ujenzi wa miundombinu yote Viwanja na Barabara, wakibainisha kuwa hatua zilizofikiwa zinaonyesha dhamira ya kuhakikisha viwanja vinakidhi viwango vinavyohitajika kwa ajili ya mashindano hayo makubwa ya soka barani Afrika.

Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) Said Kassim Marine alikua sehemu ya ziara hiyo akaiambatana na wajumbe wa Kamati ya Mashindano ya AFCON 2027, amesema Uwanja wa Fumba tayari umefikia asilimia 55% ya ujenzi na wanatarajia ikifika mwezi Agosti utakua Umefika kiwango kinachotakikana.

Hongera Tanzanite Queens kufuzu Kombe la Dunia Poland 2026
10/05/2026

Hongera Tanzanite Queens kufuzu Kombe la Dunia Poland 2026

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar tunashiriana na Watanzania wote kuadhimisha Miaka 62 ya Sikukuu ya Muungano wa Tanga...
26/04/2026

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar tunashiriana na Watanzania wote kuadhimisha Miaka 62 ya Sikukuu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

07/04/2026

15/02/2026

Mrajis wa Vyama vya Michezo Zanzibar Ndugu, Abubak Lunda amekipongeza Chama Cha Mchezo wa Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA) kwa kuendeleza Ushirikiano wao katika kutafuta viongozi kwa utaratibu ulioweka katika kanuni zao.

15/02/2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Ndugu Ali Bakar Ali (Cheupe) akitangaza Matokeo ya Uchaguzi wa Chama Cha Mchezo wa Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA).

Katika Uchaguzi huo Uliofanyika katika Skuli ya Sekondari ya Tumekuja Mjini Unguja Kamati imemtangaza Ndugu Said Suleiman Said kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho.

Address

Unguja

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share