14/10/2023
“ Nimekabidhi mipira ya maji kwa Wakaazi wa Mtopepo Chem chem kwa lengo la kusogeza huduma ya maji safi na Salam ya ZAWA Katika maeneo yao wanayoishi ”
Wakaazi wa Mtopepo Chem chem wamemshukuru mbunge wa jimbo la Welezo kwa kuwapatia mipira ya Maji kwa ajili ya kusogeza huduma ya maji safi na Salama katika maeneo ya karibu na nyumba zao.
Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa mipira hiyo wananchi wanaoishi katika maeneo hayo Abdalla Saleh Othman na Tatu Kassim Silima wamesema kwa kipindi kirefu wamekosa huduma ya maji safi na Salama kutoka Zawa, hivyo kupatiwa kwa mipira hiyo kutasaidia huduma hiyo kuwafikia karibu na kuweza kuunga katika nyumba zao.
Wananchi hao wameelezea jitihada zinazochukuliwa na mbunge wa Jimbo la welezo ikiwemo kushirikiana katika kuwasogezea huduma ya umeme ambayo tayari imeshapatikana sambamba na kumuomba kuendelea kuwatatulia matitizo ambayo bado yamekuwa kikwazo kwa wananchi hao ikiwemo tatizo la kukosekana kwa kituo cha afya katika maeneo ya karibu.
Mbunge wa Jimbo la Welezo Mhe. Maulid Saleh Ali amesema ataendelea kushirikiana na wakaazi wa maeneo hayo katika kuhakikishasha wanayapatia ufumbuzi matatizo yanayowakabili ,sambamba na kuwasihi wananchi kuitunza miundo mbinu ya mipira hiyo pamoja na kujisajili katika mamlaka ya maji Zawa ili waweze kuungiwa huduma hiyo ya maji katika nyumba zao
Zaidi ya Shilingi Milioni nne Zimetumika katika kununulia Mipira hiyo ya Maji fedha ambazo zimetokana na Mfuko wa Jimbo hilo la Welezo.