Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar

Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar Afisi ya Mwanasheria Mkuu ni miongoni mwa Afisi za mwanzo kuanzishwa Zanzibar toka mwaka 1914

Eid Njema
26/05/2026

Eid Njema

Wataalamu kutoka Tume ya Mipango Zanzibar wamefika katika Afisi ya Mwanasheria Mkuu, Mazizini, Zanzibar kupata maoni juu...
08/05/2026

Wataalamu kutoka Tume ya Mipango Zanzibar wamefika katika Afisi ya Mwanasheria Mkuu, Mazizini, Zanzibar kupata maoni juu ya Mpango Mkakati wa Maendeleo wa Miaka Mitano ijayo (ZADEP II ).
Viongozi wa Afisi ya Mwanasheria Mkuu pamoja na mambo mengine wameshauri Mpango huo usaidie kuimarisha sekta ya Sheria kuhusu mikataba ya sheria, mapitio ya Sheria pamoja na mpango wa usuluhishi nje ya Mahkama ili uweze kuleta tija zaidi kwa Serikali na wananchi kwa ujumla.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inategemea kuanza utekelezaji wa Mpango huo kwa kipindi cha miaka mitano 2026-2031.

#

Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji (mwenye Suti ya buluu) ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Wawaki...
06/05/2026

Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji (mwenye Suti ya buluu) ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi akiwa barazani kuendelea na shughuli za Mkutano wa Tatu wa Baraza la Kumi na Moja ulioanza leo May 06, 2026 huko Chukwani, Zanzibar.

#

Naibu Mwanasheria Mkuu Zanzibar Ndg. Shaaban R. Abdalla (katikati) naye amefika katika Banda la Afisi ya Mwanasheria Mku...
03/05/2026

Naibu Mwanasheria Mkuu Zanzibar Ndg. Shaaban R. Abdalla (katikati) naye amefika katika Banda la Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar na kujionea namna Watendaji wa Afisi hiyo wanavyoshiriki kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi katika maonesho ya siku ya wafanyakazi (Mei Mosi) yanayoendelea huko viwanja vya Dole Kizimbani, Wilaya ya Magharibi A.

#

#

01/05/2026

Tunakushukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kutangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka shilingi 300,000 hadi shilingi 500,000 kwa mwezi.

Tunakutakieni heri ya MEI MOSI, 2026.
01/05/2026

Tunakutakieni heri ya MEI MOSI, 2026.

Zoezi la utoaji elimu kwa wananchi linaendelea katika Banda la Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar ambapo Afisi hiyo inas...
30/04/2026

Zoezi la utoaji elimu kwa wananchi linaendelea katika Banda la Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar ambapo Afisi hiyo inashiriki maonesho ya siku ya wafanyakazi (Mei Mosi) katika viwanja vya Dole Kizimbani, Wilaya ya Magharibi A.

#

#

Watendaji wa Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar wakitoa elimu ya kisheria kwa wananchi mbali mbali wanaofika katika Band...
29/04/2026

Watendaji wa Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar wakitoa elimu ya kisheria kwa wananchi mbali mbali wanaofika katika Banda la Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar kwa lengo la kupata elimu.

Afisi ya Mwanasheria Mkuu inashiriki maonesho ya siku ya wafanyakazi (Mei Mosi) katika viwanja vya Dole Kizimbani, Wilaya ya Magharibi A ili kutoa elimu kwa wananchi wanaofika katika Banda la Afisi.

#
#

Kamati ya Quasi-Judicial ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZANUSO) imefanya mazungumzo na Watendaji w...
27/04/2026

Kamati ya Quasi-Judicial ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZANUSO) imefanya mazungumzo na Watendaji wa Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu, Utawala na Mipango Dkt. Abdul-Nasser Hikmany katika Ukumbi wa Afisi hiyo Mazizini Zanzibar.
Kupitia mazungumzo hayo, Kamati hiyo imejifunza taratibu za kisheria na uendeshaji wa mashauri katika ngazi ya kitaifa.

Aidha Kamati hiyi imepata muongozo wa kiutendaji kuhusu maadili na misingi ya haki (natural justice) katika kutoa maamuzi ya kinidhamu sambamba na kuimarisha mahusiano kati ya wanataaluma wa sheria wa baadaye na Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar.

#

26/04/2026

Address

Afisi Ya Mwanasheria Mkuu. S. L. P 259 Mazizini/Zanzibar
Zanzibar

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share