Or-tamisemim Zanzibar

Or-tamisemim Zanzibar Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

12/05/2026
Mafunzo ya Mfumo wa kupokea na kushughulikia Malalamiko (GRM) utakaotumika katika utekelezaji wa mradi wa uhimilivu wa m...
12/05/2026

Mafunzo ya Mfumo wa kupokea na kushughulikia Malalamiko (GRM) utakaotumika katika utekelezaji wa mradi wa uhimilivu wa mabadiliko ya Tabianchi (Scale program). Kwa wataalum wa mazingira na jamii kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa Zanzibar.

Mfumo huo unalenga kupokea, kushulikia na kutatua malalamiko yanayotokana na utekelezaji wa mradi huo kutoka kwa wadau na wananchi wakati wa utekelezaji wake.

Mafunzo hayo yamefanyika leo 12 Mei, 2026 katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Vuga Mkoa wa Mjini Magharib.

📆 12 Mei, 2026
📍 Vuga, Zanzibar.

12/05/2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa akiwasilisha Mukhtasari wa Hotuba Kuhusu M...

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa akiwa...
11/05/2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa akiwasilisha Mukhtasari wa Hotuba Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, Mbele ya Baraza La Wawakilishi Chukwani Zanzibar leo 11 Mei, 2026.

📆 11 Mei, 2026
📍 Chukwani, Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum  za SMZ  Mikidadi Mbarouk Mzee akifung...
09/05/2026

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mikidadi Mbarouk Mzee akifungua kikao cha Maandalizi ya miradi itakayotekelezwa kwa ushirikiano wa jumuia ya Umoja wa Ulaya baada ya kuisha kwa mradi wa GREEN AND SMART CITIES SASA.

Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 8 Mei, 2026. katika ukumbi wa Tume ya uchaguzi Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.

📆 08 Mei, 2026
📍 Maisara Zanzibar.

*MAAFISA HABARI MAWASILIANO, ITIFAKI NA  UHUSIANO SERIKALINI WAMETAKIWA KUITANGAZA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA SERIKALI  KW...
09/05/2026

*MAAFISA HABARI MAWASILIANO, ITIFAKI NA UHUSIANO SERIKALINI WAMETAKIWA KUITANGAZA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA SERIKALI KWA WANANCHI.*

Ndugu. Gerison Msigwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema atahakikisha vitengo vya habari serikalini vinaimarika ili kuzitangaza juhudi za serikali kwa wananchi wake.

Ameyazungumza hayo kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Paul Christian Makonda alipokua akifungua kikao kazi cha 21 cha Maafisa Habari na Mawasiliano kilichofanyika katika ukumbi wa Agreement Hotel Mkoani Njombe.

Katibu Mkuu amesema kazi zinazotekelezwa na Serikali zinapaswa kutangazwa kwa wananchi na kuwanyima nafasi wale wanoisema vibaya Serikali hivyo waandishi wa habari wanapaswa kutangaza kazi zinazofanywa na Serikali ili zipate kujulikanwa.

Aidha amewataka Maafisa habari kutimiza wajibu wao kwa kutumia vyema kalamu zao kwa kuyasema mazuri yanayofanywa na Serikali na kuzitangaza fursa zilizomo nchini kwa wananchi ili nao wazitumie kwa kujiajiri na kujiongezea kipato.

Msigwa amesema kwa sasa Tanzania imepata fursa ya kuchaguliwa kuwa wenyeji wa Miss World pamoja na mashindano ya Afcon 2027 hivyo Maafisa habari wanapaswa kuzitangaza fursa hizi kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Juma Suwedi amesema pamoja na Kikao kazi hicho Maafisa habari watumie fursa kwa kuitembelea Wilaya ya Njombe ili wajue mazingira na biashara zinazofanywa na wananchi wa Wilaya hiyo na kuzitangaza.

Mkuu wa Wilaya amesema Maafisa habari watu muhimu kwani huunganisha baina ya Wananchi na Serikali yao, hivyo ipo haja ya kutoa taarifa sahihi kwa wananchi kwa kuzitambua juhudi zinazofanywa na Serikali kwa watu wake.

Kikao kazi hicho ni chamuda wa siku tano na kimehudhuriwa na Maafisa zaidi ya 500 kutoka Mikoa mbali mbali ya Tanzania bara na Zanzibar.

📆 07 Mei, 2026
📍 Agreement Hotel, Njombe.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa amese...
06/05/2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa amesema Serikali kupitia Mradi wa BigZ inaendelea kutekeleza ujenzi wa vituo vya kukusanyia taka ngazi ya jamii (Primary Collection Points) kwa lengo la kuimarisha usafi wa mazingira na afya ya jamii katika maeneo ya Mijini na Vijijini.

Ameyasema hayo katika ukumbi wa Baraza la wawakilishi wakati akijibu swali la Muakilishi wa Jimbo la Magomeni Mhe. Mahfoudh Abdalla Mohammed kuhusu mpango wa Serikali wa kujenga madampo (waste collection) katika maeneo yanayotekelezwa mradi wa mitaro ya maji machafu.

Mhe. Kitwana amesema jumla ya vituo vitatu (3) vya kukusanyia taka vitajengwa katika maeneo yanayotekelezwa ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua, ikiwemo Shehia ya Meya (Magae), Nyerere (Mtumwajeni) na Sogea Jitini, ambapo mkandarasi M/s Faster Construction Group of Company tayari ameshayakagua na kukabidhiwa maeneo hayo.

Amesema Hatua hii ni sehemu ya mkakati maalum wa kuboresha mfumo wa usimamizi wa taka ngumu, kupunguza uchafuzi wa mazingira na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji, usafirishaji na uhifadhi wa taka katika Miji

📆 06 Mei, 2026
📍 Baraza la Wawakilishi, Zanzibar.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mheshimiwa Idrissa Kitwana Mustafa...
04/05/2026

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mheshimiwa Idrissa Kitwana Mustafa amewataka Wakuu wa Wilaya kutanguliza uzalendo na kuzingatia maadili kwani kufanya hivyo kutaongeza ufanisi katika utekelezaji wa majuku yao.

Ameyasema hayo wakati akifungua Mafunzo elekezi ya usalama na utunzaji wa siri za sirikali, Uzalendo na auadilifu kwa Wakuu wa Wilaya yaliofanyika Ofisini kwake Vuga amesema anaimani kua mafunzo hayo yatawasaidia viongozi kuboresha utendaji wao kwani ya tawajenga na kuwapa maarifa mapya.

Mhe. Waziri Kitwana amesma suala la uadilifu na uaminifu ni nguzo muhimu zitakazowawezesha viongozi kutunza siri za Serikali wakati wa utekelezaji wa majuku yao kila siku.

Kwa upande wao Wakuu wa Wilaya waliopatiwa mafunzo hayo wameushukuru uongozi wa wizara kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yatawasaisidia kufanya kazi kwa ubora ili kutimiza malengo ya serikali kwa wananchi wake.

Akifunga mafunzo hayo Naibu katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Ndg. Mikidadi Mbarouk Mzee amewataka wakuu wa wilaya hao kutumia nafasi zao kwa mujibu wa sheria kwani kufanya hivyo kutasaidia kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani nchini.

Mafunzo hayo ya siku moja yameandaliwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ambapo mada zilizowasilishwa ni pamoja na sharia za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, falsafa na utakelezaji wa mbio za Mweng wa Uhuru, utuzaji wa siri za Serikali, uzalendo na uadlifu.

📆 04 Mei, 2026
📍 Vuga, Zanzibar.

Heri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
30/04/2026

Heri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.

Address

Vuga Zanzibar
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Or-tamisemim Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share