Ofisi ya Rais - Tamisemim Zanzibar

Ofisi ya Rais - Tamisemim Zanzibar Ukurasa Rasmi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Wajumbe wa Bodi wakipatiwa mafunzo kuhusu taratibu za ununuzi wa umma kat...
05/09/2026

Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Wajumbe wa Bodi wakipatiwa mafunzo kuhusu taratibu za ununuzi wa umma katika utekelezaji wa Programu ya Uhimilivu wa Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, SCALE Program.

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa The Brean of Sau Inn Beach Hotel, Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja, yakilenga kuwajengea uwezo wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ili kufanya maamuzi yanayohusiana na michakato ya ununuzi wa umma katika utekelezaji wa programu hiyo.

Katika mafunzo hayo, washiriki wamepatiwa uelewa kuhusu umuhimu wa kuzingatia Sheria ya Ununuzi wa Umma, kanuni na taratibu zake, pamoja na miongozo ya Benki ya Dunia katika utekelezaji wa shughuli za ununuzi.

Pia mafunzo hayo yanatarajiwa kuongeza ujuzi na uwezo wa Wajumbe wa Bodi na Wakurugenzi katika kusimamia shughuli za ununuzi kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.

Aidha, ujuzi huo utasaidia katika utekelezaji bora wa Programu ya SCALE pamoja na miradi mingine inayotekelezwa na Serikali.

πŸ“† 05 Sept, 2026
πŸ“ Jambiani, Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Ndugu Issa Mahfoudh Haji, amewataka...
01/09/2026

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Ndugu Issa Mahfoudh Haji, amewataka wahandisi kuandaa michoro na makisio halisi ya bajeti ya miradi mbalimbali iliyoibuliwa, ili kuhakikisha inatekelezwa kwa ufanisi, uwazi na uwajibikaji.

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya wahandishi kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa za Unguja na Pemba, yaliyofanyika katika Hoteli ya Visitor’s Inn, Jambiani, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema miradi hiyo inalenga kupunguza uharibifu wa miundombinu unaosababishwa na mvua kubwa, ukame na athari nyingine za mabadiliko ya tabianchi.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo, Mhandisi wa Miradi kutoka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini, TARURA, Eng. Thobias Malando, amesema ni muhimu kushirikisha jamii katika hatua za awali za uandaaji wa taarifa na michoro ya miradi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Serikali za Mitaa, Zainab Khamis Kibwana, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea wahandisi uwezo wa kuibua na kuandaa miradi yenye tija inayozingatia mahitaji ya ya jamii katika kukabilinana Athari za mabadilko ya Tabia nchi,

Nao Wahandisi walioshiriki mafunzo hayo wamesema wamepata ujuzi utakaowasaidia kuandaa michoro na makisio ya gharama kwa usahihi, hatua itakayorahisisha utekelezaji wa mirad hiyo.

Jumla ya miradi 38 iliobuliwa katika Mikoa mbali mbali inatarajiwa kutekelezwa kupitia Program ya Uhimilivu wa Athari za mabadiliko ya Tabianchi (Scale Program) inayofadhiliwa na Benki ya Dunia.

πŸ“† 01 Septemba, 2026
πŸ“ Jambiani, Zanzibar.

Pongezi
30/08/2026

Pongezi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa ame...
29/08/2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa amewataka Maafisa waliopandishwa vyeo vya Kapteni na Luteni kuzingatia nidhamu, weledi na uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi.

Ameyasema hayo wakati wa Sherehe za Maafisa waliopandishwa vyeo, zilizofanyika katika Skuli ya ufundi na Sekondari ya Jeshi la kujenga Uchumi JKU Mtoni Wilaya ya Magharibi A.

Amesema kupandishwa cheo ni hatua muhimu inayopaswa kwenda sambamba na kuongezeka kwa uwajibikaji, hivyo maafisa hao wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa nidhamu na weledi, huku wakiheshimiana na kuwaheshimu Viongozi wao.

Aidha Mhe. kitwana amewataka Maafisa hao kuhakikisha wanatekeleza maagizo wanayopewa na viongozi wao kwa wakati na kwa ufanisi, ubunifu pamoja na kuongeza bidii na juhudi katika kazi ili kuleta matokeo chanya katika maeneo wanayosimamia.

Kwa upande wake Kanal Makame Abdalla Daima Mkuu wa Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) amesema maafisa hao wataendelea kufanya kazi kwa kuzingatia nidhamu, ushirikiano na uwajibikaji ili kuhakikisha wanatimiza majukumu waliyopewa kwa maslahi ya nchi na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wa maafisa waliopandishwa vyeo wamesema watavitumikia vyema vyeo hivyo kwa kufuata taratibu na maelekezo ya wakuu wao, pamoja na kuwashukuru Viongozi wao kwa hatua waliyofikia.

πŸ“† 28 Agosti, 2026
πŸ“ Jku Mtoni, Zanzibar.

Ndugu. Issa Mahfoudh Haji Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  amevitaka ...
27/08/2026

Ndugu. Issa Mahfoudh Haji Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ amevitaka Vikosi vya Ulinzi na Usalama kuzingatia Mafunzo watakayopatiwa ili kuhakikisha mashindano ya Afcon 2027 yanafanyika kwa amani Visiwani Zanzibar .

Ameyasema hayo wakati akifungua Mafunzo ya siku mbili kwa Vikosi vya Ulinzi na Usalama yaliyofanyika katika ukumbi wa Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Maisara Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa lengo la kuwajengea uwezo Maafisa hao.

Amesema ulinzi utahitajika katika viwanja wakati wa mechi, maeneo ya Viwanja vya Mazoezi, Hotelini pamoja na maeneo ya vivutio vya watalii yatakayotumiwa na wageni kutoka Mataifa mbalimbali, hivyo ipo haja ya kuyatumia vyema mafunzo muda utakapofika.

Kwa upande wake katibu mtendaji baraza la michezo Said Marin amesema Zanzibar ipo tayari kwa mashindano baada ya kufanyiwa ukaguzi wa miundombinu inayohusiana na mpira wa miguu, huku akisisitiza umuhimu wa usalama katika mashindano hayo.

Nao wakufunzi wa mafunzo hayo Ramadhan Abdalla Bakar Mkuu wa ulinzi na usalama wa chama cha mpira Zanzibar ZFF na Mrakibu wa Jeshi la Polisi Mohammed Manyahe kutoka Dar Es Salaam wamesema mafunzo hayo yatawasaidia wadau wa ulinzi kwa kupunguza hatari na kujua namna ya kuchukua hatua wakati wa dharura.

Kwa upande wao waliopatiwa mafunzo hayo wamesema watayatumia vyema mafunzo waliyopatiwa ili kuipatia sifa nzuri Zanzibar na Tanzania kwa ujumla ambapo mashindano hayo ya Afcon yanatarajiwa kufanyika mwakani kwa nchi ya Tanzania,Uganda na Kenya.

πŸ“† 27 Agosti, 2026
πŸ“ Maisara Zanzibar,

24/08/2026
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Nd. Issa Mahfoudh Haji amewataka wak...
20/08/2026

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Nd. Issa Mahfoudh Haji amewataka wakufunzi wa Idara maalum za SMZ kuendeleza Mafunzo kwa Vikosi hivyo ili kuwaweka utayari kwa kulinda nchi yao.

Ameyasema hayo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya Uongozi Mdogo mwaka 2026 katika chuo cha kufundishia Maaskari Pangatupu Wilaya kaskazini B.

Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inathamini mchango wa Vikosi hivyo, kwa hiyo ipo haja ya kuzidisha uzalendo pamoja na kujitolea kwa kulinda nchi yao.

Luteni kanali Said Ali Shamhuna Mkuu wa Kikosi cha Valantia Zanzibar amesema wahitimu hao wamejitolea kwa kununua Ex-ray moja na Magari manne wakati wakiwa chuoni hapo jambo ambalo litaondoa usumbufu wa usafiri kwa upande wa Unguja na Pemba na kuwataka waliokabidhiwa gari hizo kuzitunza vyema ili zidumu kwa muda mrefu.

Nae Mkuu wa chuo Cha kvz Pangatupu Luteni kanali Ramadhan Khamis Hassan amesema kwa sasa wanahitaji hati miliki ya eneo la chuo hicho ili kuepusha wavamizi wa maeneo ya chuo hicho.

Akisoma risala kwa niaba ya wahitimu hao Zawadi Maliki Mzee amesema mafunzo waliopatiwa yatawasaidia kufanyakazi zao kwa ueledi na kujitolea kwa nchi yao.

πŸ“† 20 Agosti, 2026
πŸ“ Pangatupu, Zanzibar.

20/08/2026

Address

Vuga Zanzibar
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Rais - Tamisemim Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share