02/06/2026
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa amefanya Mkutano maalum wa kiutendaji na uongozi wa Mkoa, Wilaya na Mbaraza ya Mkoa wa Kusini Unguja.
Lengo la mkutano huo ni kujitambulisha pamoja na kukumbushana mambo mbalimbali ili kuimarisha utendaji wa Mkoa huo.
Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Afisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Tunguu.