Office of the Ward Administrator Mwanda/Mgange Ward

Office of the Ward Administrator Mwanda/Mgange Ward County Government Services brought closer to you. Let's engage!!

Tulifanya ukaguzi na tathmini ya maendeleo ya ujenzi wa Soko la Mwanda ili kujiridhisha na ubora wa kazi iliyotekelezwa ...
15/07/2026

Tulifanya ukaguzi na tathmini ya maendeleo ya ujenzi wa Soko la Mwanda ili kujiridhisha na ubora wa kazi iliyotekelezwa na mkandarasi. Kwa sasa, shughuli za mwisho za ukamilishaji zinaendelea ili kuhakikisha wananchi wa Mwanda wanapata mazingira salama na bora ya kufanya biashara.

Serikali ya Kaunti ya Taita Taveta itaandaa kikao cha umma kwa lengo la kuwachagua wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Soko na kuwahamasisha wananchi kuhusu namna bora ya kulitumia soko hilo k**a fursa ya kukuza biashara zao, kuongeza kipato cha familia na kuchochea maendeleo ya uchumi wa eneo letu.

Soko hili ni uwekezaji muhimu unaolenga kuboresha huduma za biashara, kuimarisha uchumi wa wananchi na kuendelea kufungua fursa za maendeleo katika Wadi ya Mwanda/Mgange.

Shukrani za dhati kwa Mustahiki Gavana H.E Dr. Andrew Mwadime - Wakujaa, EGH, Governor Taita Taveta County , mwakilishi wadi Anselm Mwana Wa Chao , idara ya biashara pamoja na washikadau wote walioshirikiana kufanikisha mradi huu. Ama kwa hakika pamoja tunawezafika mbali.


UKAGUZI WA MRADI WA MAJI WA MWAREKERONYI WATOA MWANGA WA KUKAMILIKA KWAKE HIVI KARIBUNIMaafisa wa Serikali ya Kaunti, wa...
19/06/2026

UKAGUZI WA MRADI WA MAJI WA MWAREKERONYI WATOA MWANGA WA KUKAMILIKA KWAKE HIVI KARIBUNI

Maafisa wa Serikali ya Kaunti, wakiongozwa na msimamizi wa mradi, walifanya kikao cha ukaguzi wa maendeleo ya mradi wa ukarabati wa Mradi wa Maji wa Mwarekeronyi pamoja na mkandarasi, wanak**ati wa mradi, wananchi, Msimamizi wa Wadi na mwakilishi wa Mheshimiwa MCA.

Kikao hicho kililenga kutathmini maendeleo ya kazi na kushughulikia masuala mbalimbali yanayojitokeza katika utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa wakazi wa lokesheni ndogo ya Mgange Dawida.

Katika kikao hicho, wadau walikubaliana kuwa ni muhimu kazi zilizobaki zikamilishwe kwa haraka ili mradi uweze kukabidhiwa kwa wananchi ifikapo mwishoni mwa wiki ijayo. Aidha, ilisisitizwa kuwa miundombinu yote, ikiwemo vitekeo vya maji, ijengwe kwa viwango vya ubora na udhabiti unaohitajika.

Pia ilikubaliwa kuwa bomba la kusambaza maji kuelekea eneo la Mlambenyi karibu na mpaka wa Mrughua liongezwe urefu ili kuhakikisha wakazi wengi zaidi wanapata huduma ya maji safi na salama.

Kwa sasa, kazi ya uchimbaji na ulazaji wa mabomba imekamilika, ujenzi wa tangi la maji lenye uwezo wa kuhifadhi takriban lita 50,000 unaendelea, huku ujenzi wa vitekeo vya maji ukiendelea katika maeneo yaliyopangwa. Mradi huu unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa maji na kuimarisha maisha ya wakazi wa Mgange Dawida na maeneo jirani, taasisi za umma k**a vile kituo cha afya cha Mgange Dawida, makanisa, biashara na kadhalika.


MKUTANO WA UMMA WA MGANGE DAWIDALeo viongozi na maafisa mbalimbali wa serikali walikutana na wakazi wa Lokesheni Ndogo y...
15/06/2026

MKUTANO WA UMMA WA MGANGE DAWIDA

Leo viongozi na maafisa mbalimbali wa serikali walikutana na wakazi wa Lokesheni Ndogo ya Mgange Dawida katika mkutano wa umma uliolenga kujadili masuala muhimu yanayogusa maisha ya wananchi na maendeleo ya eneo hilo.

Miongoni mwa ajenda zilizojadiliwa ni pamoja na tahadhari dhidi ya mkurupuko wa ugonjwa wa Ebola, masuala ya usalama, shughuli za kilimo, uhifadhi wa mazingira pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayowanufaisha wananchi.

Mkutano huo ulitoa fursa kwa maafisa wa serikali kutoa elimu, hamasisho na ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi, huku wananchi wakipata nafasi ya kutoa maoni, mapendekezo na changamoto zinazowakabili.

Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wananchi na wadau mbalimbali katika kuhakikisha usalama, afya bora na maendeleo endelevu yanaimarika katika gatuzi la Taita Taveta.

MAENDELEO YA MRADI WA KUKAMILISHA KICHINJIO CHA MWANDAShughuli za utekelezaji wa mradi wa kukamilisha Kichinjio cha Mwan...
10/06/2026

MAENDELEO YA MRADI WA KUKAMILISHA KICHINJIO CHA MWANDA

Shughuli za utekelezaji wa mradi wa kukamilisha Kichinjio cha Mwanda zinaendelea vyema huku mwanakandarasi akiendelea na kazi mbalimbali za ujenzi na ukarabati katika eneo la mradi.

Kufikia sasa, ua wa kuzunguka eneo la kichinjio unaendelea kujengwa, mnara wa kushikilia tangi la maji umejengwa, eneo la mradi limefyekwa na kusafishwa, huku milango pamoja na mabomba ya kupitisha maji taka yakifanyiwa ukarabati.

Mradi huu ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Kaunti za kuboresha miundombinu ya mifugo na kuhakikisha huduma za uchinjaji zinazingatia viwango vya afya, usafi na usalama.

Ukikamilika, mradi huo utaimarisha mazingira ya kazi kwa wafugaji na wachinjaji, kuboresha ubora wa nyama inayowafikia walaji, na kuchangia afya bora ya jamii kwa ujumla.

MATUMAINI MAPYA KWA WAFANYABIASHARA WA MWANDASerikali ya Kaunti ya Taita Taveta imemkabidhi rasmi mkandarasi kazi ya kuk...
02/06/2026

MATUMAINI MAPYA KWA WAFANYABIASHARA WA MWANDA

Serikali ya Kaunti ya Taita Taveta imemkabidhi rasmi mkandarasi kazi ya kukamilisha ujenzi wa Soko la Mwanda. Hatua hii inalenga kuboresha mazingira ya biashara na kuimarisha shughuli za kiuchumi kwa wafanyabiashara wa eneo hilo.

Kazi za ukamilishaji zitahusisha ujenzi wa vyoo, kuunganishwa kwa huduma ya maji safi, ujenzi wa makabati ya kuhifadhia bidhaa pamoja na ukarabati wa jumla wa jengo hilo ili kulifanya kuwa tayari kwa matumizi ya umma.

Mradi huu ulipatiwa kipaumbele kufuatia maoni ya wananchi yaliyotolewa kupitia vikao vya ushirikishwaji wa umma, ambapo wakazi walitaka serikali kuelekeza rasilimali katika kukamilisha miradi ya zamani iliyokwama badala ya kuanzisha mingine mipya.

Kukabidhiwa kwa mradi huu kunaongeza orodha ya miradi iliyokamilishwa katika eneo la Mwanda ikiwemo Ukumbi wa Mikutano wa Njawuli, Banda la Boda Boda la Kisangarinyi na Shule ya Ufundi ya Mwanda (VTC), huku ukamilishaji wa Kichinjio cha Mwanda ukiendelea kutekelezwa.

Wananchi wa Wundanyi Waadhimisha Sikukuu ya Madaraka kwa Shamrashamra KubwaKulikuwa na shamrashamra za aina yake katika ...
01/06/2026

Wananchi wa Wundanyi Waadhimisha Sikukuu ya Madaraka kwa Shamrashamra Kubwa

Kulikuwa na shamrashamra za aina yake katika uwanja wa Shule ya Lushangonyi wakati wananchi walipokusanyika kuadhimisha Sikukuu ya Madaraka. Hafla hiyo iligubikwa na mbwembwe, vifijo na nderemo huku wakazi wakishiriki kwa furaha katika shughuli mbalimbali za kitamaduni na burudani.

Wananchi walipata fursa ya kushuhudia na kushiriki ngoma za kitamaduni zikiwemo Mwazindika na Kishawi, pamoja na nyimbo za uzalendo zilizosisitiza umuhimu wa umoja, amani na maendeleo ya taifa. Vilevile, vikundi vya maigizo vilitoa maonyesho yaliyobeba ujumbe wa maendeleo, uzalendo na mshik**ano wa kijamii.

Kilele cha maadhimisho hayo kilikuwa usomaji wa hotuba ya Rais wa Kenya iliyowasilishwa na Jane Kaingati. Vilevile, hotuba ya Gavana wa Taita Taveta County, Andrew Mwadime Wakujaa, ilisomwa kwa niaba yake na Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo, Bw. Mcharo.

Sherehe hizo zilihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kaunti akiwemo Mheshimiwa Anselm Chao na Mheshimiwa Newton Kifuso, ambao ni Wawakilishi wa Wadi ya Mwanda/Mgange na Wumingu/Kishushe mtawalia. Vilevile, Anne Mwatika, Msimamizi wa Gatuzi Dogo la Taita, alihudhuria hafla hiyo pamoja na Dickson Ngati, Msimamizi wa Wadi ya Mwanda/Mgange.

Aidha, Chifu wa Mgange, Adline Zighe, alihudhuria akiambatana na machifu na manaibu chifu kutoka maeneo mbalimbali. Timu ya usalama ya Wundanyi pia ilikuwepo kuhakikisha sherehe hizo zinafanyika kwa utulivu, usalama na mafanikio makubwa. Wawaniaji wa nyadhifa mbalimbali pia walihudhuria na kishiriki katika kutoa michango mbalimbali ili kufanikisha sherehe hizo.

Maadhimisho hayo yalidhihirisha uzalendo, mshik**ano na ari ya wananchi wa Wundanyi katika kuenzi historia ya taifa huku wakisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wananchi, viongozi na wadau mbalimbali katika kuharakisha maendeleo ya Wundanyi taifa kwa ujumla.

Mwarekeronyi Water Project Set for a Major Facelift Courtesy of the County GovernmentResidents of Mgange Dawida Sub-loca...
30/04/2026

Mwarekeronyi Water Project Set for a Major Facelift Courtesy of the County Government

Residents of Mgange Dawida Sub-location are set to benefit from the rehabilitation of the Mwarekeronyi Water Project funded by the County Government of Taita Taveta.

The project site has already been handed over to the contractor, paving the way for the commencement of works that will directly benefit residents of Kisheda, Mlambenyi, and Mwangea villages.

The scope of works includes sump construction, pipeline supply and installation, construction of chambers at the Ngulu intake, replacement of GI pipes from Mwarekeronyi Tank I to the Mlambenyi area, and installation of community water points.

Once complete, the project will enhance access to clean and safe water for residents and key institutions including Mgange Dawida Model Health Centre and Mwangea Comprehensive School, among other social amenities.

This intervention underscores the County Government’s commitment to improving access to clean and potable water for all residents.

The County Government of Taita Taveta has officially handed over the project site for the completion of the Mwanda Slaug...
27/04/2026

The County Government of Taita Taveta has officially handed over the project site for the completion of the Mwanda Slaughterhouse. ​The tender awarded to Greenlance Limited, is a major step forward for our local economy and public health standards.

Among works set to be implemented include securing the site with a chain link perimeter fencing and constructing of a dedicated holding bay for livestock. To ensure high hygiene standards, the work includes full plumbing, drainage, installation of a water tower and supplying and installation of a plastic tank to the facility. The interior will be completely upgraded with professional floor and wall finishes, hanging rails for processing, and new concrete worktables.

​Speaking at the site today, Taita Sub Countu Veterinary Officer Dr. Nasra Mwavula noted that by investing in infrastructure upgrade, the Government is ensuring that livestock farmers have better facilities and meat consumers receive the highest quality products with proper consideration on health standards.

The project that will commence in a weeks time is expected to be completed in 4 weeks time and will ease the hustle for meat traders who have to travel for over 5KM to access slaughterhouse services in Mgange. The planned upgrades will transform the facility into a modern, hygienic hub for meat processing.

Grading works are currently ongoing along the Kisangarinyi–Mwalashi–Mghwala-Ivunyi road in Mwanda Location.This activity...
31/03/2026

Grading works are currently ongoing along the Kisangarinyi–Mwalashi–Mghwala-Ivunyi road in Mwanda Location.

This activity forms part of the broader rehabilitation works, whose scope includes bush clearing, slab installation, climate change mitigation measures, and other cross-cutting interventions aimed at enhancing sustainability and resilience.

Upon completion, the project is expected to significantly improve accessibility to Upper Njawuli villages, opening up key access routes to Vuria ECDE, Ndumbinyi ECDE, Mghwala, and Shashame townships.

This initiative is one of several road development projects being implemented under the leadership of Governor Andrew Mwadime Wakujaa across the ward and the County at large.

The project implementation team, comprising Sub-County Roads Officers, the Project Management Committee (PMC), the Area Ward Administrator, and the Ward Office Manager, conducted a site visit today to monitor progress and ensure adherence to implementation standards.

We convened a community engagement meeting featuring users of the Lolo–Ndau Water Project  which serves a section of Mga...
10/02/2026

We convened a community engagement meeting featuring users of the Lolo–Ndau Water Project which serves a section of Mgange Dawida residents to discuss challenges facing the project and chart a way forward.

The meeting, initiated by the Ward Administrator and the Sub-County Water Officer, focused on the sustainable use of the water resource. We sensitized the users on the importance of conservation, transparency, and accountability to ensure they discharge their responsibilities in harmony.

Participants agreed that the operation of the community water project is a collective responsibility and called on every user to play their role effectively.

During the meeting, users elected their representatives to the project’s operational committee. The committee will undergo training by the Taita Sub-County Water Officer on best practices for sustainable water management.

Residents were also cautioned against rampant bush fires affecting nearby forests, which threaten to drive some plant and animal species to extinction.

The meeting was facilitated by Area Assistant Chief Erick Kera, Ward Administrator Dickson Ngati, and Taita Sub-County Water Officer Wilbard Chombo.

Address

Mgange
80306

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+254753685457

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Office of the Ward Administrator Mwanda/Mgange Ward posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share