15/06/2026
Kijana mmoja aitwaye Lameck Jonathan Mlay (30) mfanya usafi wa bar na mkazi wa Maji ya Chai mkoani Arusha anadaiwa kumuua Husna Shabani (33) mkazi wa Majengo Jijini Arusha na kisha kutupa mwili huo katika chemba ya maji taka iliyopo katika bar hiyo.
SWAHILI MEDIA imefika eneo la tukio na kuzungumza na wajumbe wa serikali wa mtaa wa samanga ilipo bar hiyo na kudai kuwa walifika na kuonyeshwa video za cctv camera ikimuonyesha mtuhumiwa huyo akifanya tukio Hilo.
Aidha Akitoa taarifa hiyo leo Juni 15, 2026 Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 14, 2026 muda wa jioni huko katika Bar iitwayo Sh**ha Village iliyopo kata Elerai Jijini Arusha.
Kaamanda masejo Ameendelea kufafanua kuwa uchunguzi wa awali wa Jeshi hilo umebaini kuwa kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa na marehemu walikuwa pamoja kwenye starehe katika eneo hilo, huku akibainisha wanakamilisha uchunguzi kwa taratibu nyingine za kisheria.