07/08/2023
Mkulima akipata maelezo ya kina ya teknolojia ya kuchakata zao la chikichi ili kupata mafuta ya kula kutoka kwa Mtalamu Mosses Chalamila alipo tembelea banda la TEMDO katika maonesho ya Nane Nane kanda ya Kaskazini.
TEMDO ni Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania iliopo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Katika maonesho ya 29 Nane Nane (88) TEMDO imeshiriki na Teknolojia mbalimbali k**a vile Mtambo wa kumamua na kusafisha mafuta ya Alizeti, Mtambo wa kuchakata unga wa Muhogo, Mtambo wa kuchakata siagi ya karanga, Mtambo wa kuchakata unga wa lishe, Mtambo wa kuchakata juisi ya matunda, Mtambo wa kuchakata viungo vya chakula, Mashine ya kutoa mjuzi wa zabibu kwaajili ya viwanda vya mvinyo.
Pia Taasisi imeshiriki na vifaa tiba vya hosipitali k**a vile vitanda vya kuwagulia wagonjwa, vitanda vya kulazia wagonjwa na kujifungulia Wamama wajawazito, Majokofu ya kuifadhia Maiti ya ngazi mbili mpaka sita na pia kiteketezi cha taka hatarishi zinazo zalishwa na hosipitali- "Biomedical Solid Waste Incinerator".