15/06/2026
ARUSHA: SERIKALI itaendelea kuongeza nguvu katika uhifadhi wa wanyamapori aina ya faru ambao wapo haratini kutoweka kwa kuimarisha Mradi wa Kimkakati wa Uhifadhi wa Faru Weupe ili kuongeza chachu ya ongezeko la uhifadhi na utafiti wa wanyamapori waliopo nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamad Hasaan Chande wakati wa hafla maalumu ya kuwaachilia huru faru weupe 17 waliopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ikiwa ni mradi maalumu uliofadhiliwa kupitia Shirika la Andbeyond kwa ushirikiano na Serikali ya Afrika Kusini
“Kwa kweli mmebuni kitu kizuri ambacho kinaleta tija na ufanisi na kuleta lmaendeleo kwa nchi yoyote, lengo kuu ikiwa ni kuongeza utafiti, uhifadhi na kupata elimu.
"Wako wengi duniani watakuja kujifunza kupitia Faru hawa weile wakiwa ama ni wanafunzi, au wakufunzi," Chande.
Amempongeza na kumshukuru mhifadhi namba moja nchini katika uhifadhi na muongoza watalii, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa utayari na utashi wake katika uhifadhi huku akiishukuru pia Serikali ya Afrika Kusini kwa ushirikiano mzuri na Tanzania kwa ufadhili wa faru hao.
Zaidi tembelea//habarileo.co.tz
Imendaliwa na Mwandishi Wetu