11/08/2026
Ì
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Ziwa imeshiriki katika Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Ilemela jijini Mwanza Agosti 11, 2026 kwa kutoa elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya kwa wananchi waliofika katika Viwanja vya Kabwali ambako pia kunafanyika mkesha wa Mwenge wa Uhuru kabla ya kukabidhiwa Wilaya ya Magu.
Kupitia banda lake DCEA imetoa elimu kuhusu madhara ya matumizi na biashaa ya dawa za kulevya huku wananchi wakihamasishwa kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya tatizo hilo.
Aidha, ujumbe wa dawa za kulevya ni ajenda muhimu katika mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa unaolenga kuhamasisha jamii kujiepusha na matumizi na biashara ya dawa za kulevya pamoja na kushirikiana na Serikali katika kuzuia na kupambana na tatizo hilo.
DCEA Kanda ya Ziwa itaendelea kutumia fursa mbalimbali za kitaifa kuifikia jamii kwa elimu na kuhamasisha wananchi kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya.