05/05/2026
NEMC KANDA YA MOROGORO-RUFIJI NA MABALOZI WA MAZINGIRA WAFANYA ZIARA SHULE YA SEKONDARI MWEMBESONGO
๐Watoa Elimu ya Mazingira ya Mazingira
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa Kushirikiana na Mabalozi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Grit Godfrey Mwimanzi na Chage Alex Chage wamefanya ziara katika Shule ya Sekondari ya Mwembesongo na kutoa elimu ya Mazingira katika Shule hiyo hususan kuhusu fursa zilizopo kwenye taka, Utunzaji wa Mazingira pamoja na kupanda miti.
Tukio hilo liliongozwa na mwenyeji ambaye ni Meneja wa NEMC Kanda ya Morogoro - Rufiji
Ndugu Arnold Mapinduzi akiambatana na Maafisa wa Kanda hiyo.
Aidha tukio hilo lilihusisha Afisa Mazingira wa Manispaa ya Morogoro na wadau wengine wakiwemo Masai wa Maji (Tone la Maji lihifadhiwe) Kipaji changu Foundation na Wananchi kwa ujumla.
Aidhaa Maafisa wa NEMC pamoja na mabalozi wa Mazingira walisisitiza juu ya namna ambavyo taka si uchafu tena bali zinaweza kubadilika Kuwa Fursa.
Aidha, Mabalozi wa Mazingira Waliahidi kupeleka Dustbins kwenye Shule Hiyo Walau watoto waanze kwa vitendo swala la utenganishaji Wa Taka kwenye Shule Hiyo lakini pia na kuwatafutia Mdau kwa ajili ya kupata kizimba Cha utenganishaji Wa Taka.
Pia Pongezi Kubwa zilitolewa Kwa Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi sambamba na timu nzima ya NEMC Nchini kwa muendelezo wa kampeni ya Taka ni Fursa kwa nchi nzima, kwa mlengo wa kuhakikisha Miji na Majiji yanakuwa Safi lakini pia Kuhakikisha Madampo sasa hayatafurika uchafu badala yake Taka Nyingi zitatumika k**a ni Fursa Kwa kuzirejeleza au kwa Matumizi Mengine