05/01/2026
UELEKEO WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Ndugu, Dorothy Semu leo 05 Januari, 2026 ameanza ziara yake katika majimbo ya mikoa ya kusini ya kukutana na viongozi juu ya kupata maoni na kufafanua hatua zilizochukulia pamoja na msimamo wa chama baada ya uchaguzi mkuu 2025 kumalizika. Ziara hiyo imeanza katika majimbo ya Tunduru Kusini na Tunduru Kaskazini katika Mkoa wa Kichama Selous.
Kwenye kikao hicho kiongozi wa chama amepokea maoni ya viongozi wa chama waliohudhuria kikao hicho kwamba uchaguzi haukuwa wa huru, haki na kuaminika. Mbali na maoni hayo wapo wameoshauri chama kiende kwenye maridhiano kuwaeleza uso Kwa macho ubadhirifu uliofanyika na wapo ambao wameshauri mapambano ya kusaka katiba mpya hayapaswi kuwa na mbadala.
Baada ya kupokea maoni ya viongozi kiongozi wa chama amehutubia na kutoa ufafanuzi juu ya msimamo wa chama baada ya uchaguzi mkuu ambapo amesema;
Kwanza, tulisema tutashiriki huku tukipambana na tutapambana huku tukishiriki katika hili ni wajibu tuliubeba viongozi tukitambua kuwa tunaenda kuyakabili mapambano katika uwanja usiokuwa huru na haki. Hatutakata tamaa tutaendelea kupambana bila kurudi nyuma kwa kusimama na Wananchi, kusimama na haki mpaka hapo mabadiliko ya kweli na kuaminika yatakapopatikana.
Mbili, Bado tunasisitiza juu ya serikali kusitisha mara Moja vitisho na kamatakamata watu na kuwaweka ndani viongozi wa upinzani bila kufuata Sheria.
Tatu, Sauti za watu wanaodai haki na manadiliko zinapaswa kusikilizwa na kuleta majawabu ya kupatikana Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.
Nne, wito wetu ni serikali kuwaachia huru viongozi wote wa kisiasa na wananchi wote waliobambikiziwa kesi za uchaguzi
Tano, iundwe Tume huru ya Uchuguzi njee ya serikali iweze kuchunguza matukio ya Oktoba 29, 2025. Tume hii inapaswa kuwa yenye uwezo wa kuhoji bila ya maelekezo ili iweze kutupa taarifa zenye ukweli juu ya kilichojili Oktoba 29. Tume hiyo ya Jaji Chande tuliikataa na sasa tunaikataa na hatutaipa ushirikiano kwasababu imekosa uhalali.
Sita, tume ya maridhiano iliyo huru na sio ya Serikali. Tume hiyo iundwe njee ya Serikali. Ituite pamoja wadau wote tuweze kutengeneze mazingira bora ya kuleta mabadiliko yenye kuaminika.
Saba, tunahitaji Katiba Mpya itakayokuja na Tume huru na kutoa uhuru wa mihimili itayotoa haki sawa kwa wote.
Nane, Uporaji wa haki za wananchi kuchagua viongozi wao tulisema tutaipeleka INEC na Serikali Mahakamani na sasa tumefungua kesi 25 kwa upande wa Zanzibar na 30 kwa upande wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hitimisho
Kiongozi amehitimisha kwa kusema Tanzania haitajengwa kwa hofu na risasi bali kwa uadirifu na uongozi unaoleta majawabu kwa watu wake. CCM wamebadilisha uchaguzi kuwa uwanja wa vita badala ya kuwa uwanja wa kupata viongozi bora.