Awe ametimiza umri wa miaka minne (4)
iii. Muda wa kuingia madrasa ni kuanzia saa 01:00 Asubuhi hadi saa 01:30 Asubuhi, Kwa mchana ni saa 08:00 mpaka saa 09:00 Alasiri. Zaidi ya hapo mwanafunzi atakua amechelewa. Muda wa kutoka Madrasa ni saa 05:00 Asubuhi kwa Asubuhi, na saa 12:00 jioni. Mwanafunzi anatakiwa kufika Madrasa wakati wowte atakapohitajika. Iwapo mtoto hatafika Madrasa na hakuna taar
ifa ya Mzazi / Mlezi kwa Mwalimu, basi atakapofika kwanza ni adhabu kisha ndo ataulizwa sababu. Mwanafunzi anatakiwa aje Madrasa akiwa msafi wa Kiwiliwili, meno, nywele, kucha, nguo n.k. Ni marufuku Mwanafunzi yoyote kuvaa pambo la aina yeyote kama vile (piko, hina, hereni, saa, mkufu, kuunganisha nywele, n.k)
ii. Pia ni marufuku kwa mwanafunzi yeyote kukata mikato ya nywele isiyoendana na maadili ya dini yetu
i. Wavulana ni Kanzu na Kofia
ii. Wasichana ni Baibui jeusi na Juba jeusi
iii. Sare zipatikane ndani ya mwezi mmpja zaidi ya hapo mtoto atarudishwa nyumbani
i. Wazazi /Walezi wanatakiwa kushirikiana na Waalimu katika kuleta maendeleo ya Madrasa. Muislam yeyote anakaribishwa kuleta sadaka yake. Madrasa hii tunapumzika mara moja kwa mwaka na wanafunzi wote wanatakiwa kuwepo siku ya kufunga na kufungua Madrasa, na iwapo mtoto wako hatakuepo siku hizo basi atapata adhabu. Madrasa hii ni ya kiislamu, ieleweke kwamba maadili ya madrasa hii ni ya kiislam hivyo basi mwanafunzi anatakiwa kuhudhuria vipindi vya swala muda wote akiwa ndani na nje ya madrasa. Pia endapo mwanafunzi atahama madrasa kwasabu za msingi basi Mzazi / Mlezi unatakiwa umtolee ubani (kifuta jasho) ili apate radhi za waalimu
2. Sira iii. Hadithi iv. Tajweed vi. Tawheed n.k