12/04/2026
KATIBU WA HAMASA NA CHIPUKIZI MKOA WA DAR ES SALAAM ATEMBELEA VIJANA WA HAMASA TEMEKE
๐Temeke,Dar es salaam
๐ 09-04-2023
Ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa uhuru unaotarajiwa kuwasili Dar es Salaam mnamo tarehe 13-04-2026 katibu wa hamasa na chipukizi mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Khassim Ngonyani amewatembelea vijana wa hamasa wa wilaya ya temeke na kushiriki nao mazoezi.
Ziara hiyo imelenga kutazama maandalizi ya hamasa ya Mwenge pamoja na changamoto zinazowakabili vijana wa hamasa.Ambapo katika ziara hiyo aliambatana na mjumbe wa baraza la UVCCM mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Elizabeth Mmonda sambamba na wajumbe wa baraza la UVCCM wa wilaya ya Temeke.
Alipukuwa akizungumza na vijana hao Ndg. Khassim Ngonyani alisema " Mwenyekiti wetu wa UVCCM mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Nasra Mohamed amenituma niwape salaam zake za upendo wake juu yenu na kwamba amewasisitiza kutanguliza uzalendo,nidhamu na kutanguliza maslahi ya taifa lenu mbele kabla ya chochote".