U.S. Embassy Tanzania

U.S. Embassy Tanzania The U.S. Mission to the United Republic of Tanzania. Terms of Use: https://www.state.gov/tou

Zaidi ya Kukimbia Pamoja! Ushirikiano mzuri haujengwi katika kumbi za mikutano.Unajengwa kupitia mafunzo, kazi ya pamoja...
04/09/2026

Zaidi ya Kukimbia Pamoja!
Ushirikiano mzuri haujengwi katika kumbi za mikutano.
Unajengwa kupitia mafunzo, kazi ya pamoja na uzoefu wa pamoja.

Wataalamu wa kijeshi wa Marekani na Tanzania wameanza mafunzo ya kwanza barani Afrika yaitwayo Psychological Operations Joint Combined Exchange Training, yakileta pamoja wataalamu kutoka nchi zote mbili kujifunza kutoka kwa wenzao na kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu wa kiusalama kati ya Marekani na Tanzania.

Mazoezi hayo ya pamoja yanalenga kuwezesha kila upande kujifunza kutokana na uzoefu wa mwenzake katika kuzuia migogoro, kujenga imani na jamii za kiraia, pamoja na kutekeleza shughuli za uokoaji na kampeni za mawasiliano wakati wa majanga ya asili.

—————————————————————————

More Than Just a Run!

Good partnerships are rarely built in conference rooms.
They’re built through training, teamwork, and shared experiences.

U.S. and Tanzanian military professionals kicked off the first Psychological Operations Joint Combined Exchange Training conducted in Africa, bringing together experts from both countries to learn from one another and strengthen our long-standing U.S.-Tanzanian security partnership.

The joint exercise is aimed at each force learning from the experience of the other on conflict prevention, building trust with civilian populations, and conducting rescue operations and communication campaigns during natural disasters.

Kwa pamoja, Marekani na Tanzania zinashirikiana kufikia malengo makubwa ya kuzuia malaria.K**a sehemu ya juhudi hizo, ka...
02/09/2026

Kwa pamoja, Marekani na Tanzania zinashirikiana kufikia malengo makubwa ya kuzuia malaria.

K**a sehemu ya juhudi hizo, katika kipindi cha wiki nne zilizopita, Marekani imetoa vyandarua 3,209,476 vyenye dawa ya kuua mbu, ambavyo vimesambazwa katika mikoa ya Katavi, Mara na Lindi, na hivyo kuzipatia familia njia iliyothibitishwa ya kujikinga na malaria na kulinda afya zao.

Kwa kuzingatia afua zenye matokeo makubwa na kuimarisha uwezo wa Tanzania kuziendeleza kwa ufanisi, tunajenga mfumo wa afya ulio imara zaidi na wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto, unaowalinda watu leo huku ukiweka msingi wa maisha yenye afya bora na mustakabali wenye uwezo mkubwa zaidi wa kujitegemea.

Kwa pamoja, tunaweza kupunguza vifo vinavyotokana na malaria duniani kwa asilimia 90 ifikapo mwaka 2030.

---------------------------------------------------------------------

Together, the United States and Tanzania are partnering to accomplish ambitious goals in malaria prevention.

As part of that effort, in the last four weeks the U.S. provided 3,209,476 insecticide-treated bed nets distributed across Katavi, Mara, and Lindi regions, giving families a proven tool to prevent malaria and stay healthy.

By focusing on high-impact interventions and strengthening Tanzania’s capacity to sustain them, we are building a stronger, more resilient health system that protects people today while strengthening the foundation for a healthier, more self-reliant future.

Together, we can reduce global malaria mortality by 90% by 2030.

Vituo vya Kimarekani (American Spaces) ni mahali pa kujifunza kuhusu utamaduni wa Marekani na kushiriki katika programu ...
01/09/2026

Vituo vya Kimarekani (American Spaces) ni mahali pa kujifunza kuhusu utamaduni wa Marekani na kushiriki katika programu mbalimbali zinazofadhiliwa na Marekani.

Mwezi huu, Vituo vya Kimarekani nchini Tanzania vitaandaa programu za maonyesho ya filamu, programu za kuboresha umahiri wa lugha ya Kiingereza, kuongeza uelewa kuhusu Akili Mnemba (AI), na kujenga ujuzi wa vitendo, ikiwemo utayarishaji wa podcast.

ungana nasi katika American Space iliyo karibu nawe jijini Dar es Salaam, Dodoma, Unguja, Pemba au Mwanza, au shiriki katika programu zetu kwa njia ya mtandao.

Usikose fursa hii ya kujifunza, kuungana na wengine, na kujenga ujuzi mpya!

————————————————————————————

American Spaces are the place to engage with U.S. culture and programs.

This month, American Spaces Tanzania will host programs showcasing American excellence through film, improving English language proficiency, building AI literacy, and developing practical skills, including podcast production.

Join us at an American Space near you in Dar es Salaam, Dodoma, Unguja, Pemba, or Mwanza, or take part in our virtual sessions.

Don’t miss out on this opportunity to learn, connect, and build new skills!

Nini hutokea sayansi inapokutana na sinema?Katika American Corner Unguja, onyesho la Jurassic Park kupitia American Film...
01/09/2026

Nini hutokea sayansi inapokutana na sinema?

Katika American Corner Unguja, onyesho la Jurassic Park kupitia American Film Showcase liliibua mazungumzo yenye hamasa, yaliyoongozwa na mwanasayansi anayeishi Zanzibar, Daniel Joshua, kuhusu mikrobiolojia, bioteknolojia, na maadili yanayohusu uvumbuzi wa kisayansi.

Filamu k**a Jurassic Park zinaonyesha nguvu ya usimuliaji wa hadithi wa Marekani katika kuchochea udadisi, kupanua mtazamo wetu kuhusu yale yanayowezekana, na kuwahamasisha wanasayansi na wavumbuzi wa kesho.

---------------------------------------

What happens when science meets cinema?

At American Corner Unguja, an American Film Showcase screening of Jurassic Park prompted a lively conversation led by Zanzibar-based scientist Daniel Joshua about microbiology, biotechnology, and the ethics of scientific innovation.

Films like Jurassic Park show the power of American storytelling to spark curiosity, expand our sense of what is possible, and inspire the scientists and innovators of tomorrow.

Je, diplomasia inaweza kupanuaje biashara, kuvutia uwekezaji, na kuunda fursa?Wiki iliyopita, Ubalozi wa Marekani uliwak...
31/08/2026

Je, diplomasia inaweza kupanuaje biashara, kuvutia uwekezaji, na kuunda fursa?

Wiki iliyopita, Ubalozi wa Marekani uliwakaribisha wanafunzi kutoka Kituo cha Mahusiano ya Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim kwa majadiliano yenye hamasa kuhusu diplomasia ya kiuchumi na ushirikiano kati ya Marekani na Tanzania.

Wanafunzi walijadili jinsi diplomasia inavyoweza kuimarisha mahusiano ya kibiashara na kukuza ustawi wa pamoja kwa nchi zetu mbili.

--------------------------------------------------------------

How can diplomacy expand trade, attract investment, and create opportunity?

Last week, the U.S. Embassy welcomed students from the Dr. Salim Ahmed Salim Centre for Foreign Relations for a lively discussion on economic diplomacy and the U.S.-Tanzania partnership.

Students explored how diplomacy can strengthen commercial ties and advance shared prosperity for both our countries.

U.S. embassy employees provide the critical expertise and operational support that allows American diplomacy to function...
24/08/2026

U.S. embassy employees provide the critical expertise and operational support that allows American diplomacy to function. The U.S. Embassy in Dar es Salaam invites all qualified candidates to apply for the below position:

*Economic Specialist
*Political Specialist

For details on all available positions, required qualifications, and application instructions, please visit: http://bit.ly/36QUjeh

Kaimu Balozi Lentz aliendeleza ziara yake baada ya ushiriki wake katika Data Tamasha kwa kufanya mazungumzo ya kina na y...
19/08/2026

Kaimu Balozi Lentz aliendeleza ziara yake baada ya ushiriki wake katika Data Tamasha kwa kufanya mazungumzo ya kina na yenye tija na Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya na Rais Mstaafu wa Zanzibar.

——————————————————————-

Charge Lentz followed his engagement at Data Tamasha with a deep and fruitful conversation with Amani Abeid Karume, Chancellor of Mbeya University of Science and Technology and former President of Zanzibar.

Akili ni mali.Tanzania ina vipaji na ari ya kuchangia katika kuunda mustakabali wa kidijitali wa Afrika—na si kuwa mtumi...
19/08/2026

Akili ni mali.

Tanzania ina vipaji na ari ya kuchangia katika kuunda mustakabali wa kidijitali wa Afrika—na si kuwa mtumiaji tu wa teknolojia.

Kaimu Balozi Andy Lentz alitoa hotuba leo katika tamasha la tano la Data Tamasha linalofanyika kila baada ya miaka miwili, lililoandaliwa na Tanzania Data Lab (dLab).

Tamasha hilo linaangazia jinsi data, akili bandia (AI), na teknolojia ya kidijitali zinavyoweza kupanua fursa za kiuchumi na kuchangia mustakabali wa kidijitali wa Tanzania.

dLab ina uhusiano wa muda mrefu na Marekani, na kwa pamoja, kwa kutumia teknolojia bora zaidi ya Marekani, tunaweza kujenga mfumo wa ubunifu uliounganishwa kimataifa ambao ni salama kwa watumiaji.
——————————————————————-

Akili ni mali. Wisdom is wealth. 

Tanzania has the talent and ambition to shape Africa’s digital future—not simply consume it.

Chargé d’Affairs Andy Lentz delivered remarks today at the Tanzania Data Lab’s (dLab’s) fifth biennial Data Tamasha - a festival highlighting how data, AI, and digital technology can expand economic opportunity and support Tanzania’s digital future.

dLab has longstanding ties to the United States, and together, leveraging best-in-class American technology, we can build a globally-interconnected innovation ecosystem that is secure and safe for users.

Mkurugenzi Mwenza wa Kitengo Kitengo kunachoshughulikia masuala ya Akili Mnemba na Sheria cha Chuo Kikuu cha Washington,...
18/08/2026

Mkurugenzi Mwenza wa Kitengo Kitengo kunachoshughulikia masuala ya Akili Mnemba na Sheria cha Chuo Kikuu cha Washington, Oliver Roberts, alikutana na waandishi wa habari na wanaharakati wanaofanya kazi kuunga mkono uhuru wa habari na kujadili jinsi akili mnemba (AI) inavyowakilisha fursa na changamoto kwa vyombo vya habari, hususan katika uandishi wa habari unaolenga maslahi ya umma na uchambuzi wa data.
Uandishi wa habari unaweza kunufaika kwa kiasi kikubwa na zana hizi, lakini sera za matumizi yenye uwajibikaji pamoja na usimamizi wa binadamu ni muhimu ili kudumisha uaminifu, maadili ya uandishi wa habari, na viwango vya kitaaluma vya uandishi wa habari katika siku zijazo.
……………………..

Co-Director of the WashU Law AI Collaborative Oliver Roberts met with journalists and activists working to support information freedom and examined how AI represents both an opportunity and challenge for the media related to public interest journalism and data analysis.
Journalism stands to benefit greatly from these tools, but responsible use policies and human oversight are required to maintain credibility, journalistic integrity, and maintain journalistic standards in the future.

Address

686 Old Bagamoyo Road, Msasani
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 11:30

Telephone

+255222294000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when U.S. Embassy Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share