Uongozi na siasa

Uongozi na siasa uongozi ndani ya nchi ulivyo mezwa na siasa

TAARIFA KWA UMMA  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Manyoni,  Dkt. Pius Stephen Chaya,  Naibu Waziri – Ofisi ya Rais (Mipango ...
27/05/2026

TAARIFA KWA UMMA
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Manyoni,
Dkt. Pius Stephen Chaya,
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji)

Kwa heshima na taadhima, Dkt. Pius Stephen Chaya anapenda kuwatakia wananchi wote wa Jimbo la Manyoni na Watanzania kwa ujumla Eid al-Adha Mubarak.

Katika siku hii tukufu ya kiimani, tunakumbushwa thamani ya imani, mshik**ano wa kijamii, na moyo wa kujitolea kwa ajili ya wengine. Ni wakati wa kushirikiana, kusaidiana, na kuimarisha undugu wa kitaifa.

Dkt. Chaya anawaomba wananchi wote kuendeleza mshik**ano, amani, na upendo katika familia na jamii, huku tukitumia sikukuu hii k**a daraja la kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Eid Mubarak!
Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Manyoni
Dkt. Pius Stephen Chaya
Naibu Waziri – Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji)

*SERIKALI KUENDELEA KUFANYA MAGEUZI YA SERA– DKT. MWIGULU*WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea k...
27/01/2026

*SERIKALI KUENDELEA KUFANYA MAGEUZI YA SERA– DKT. MWIGULU*

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kufanya mageuzi ya sera zinazogusa moja kwa moja maslahi na ustawi wa maisha ya wananchi.

Amesisitiza kuwa Serikali haitavumilia watendaji wa Serikali wanaotoa visingizio, wasiowajibika na wenye hulka ya kufanya kazi kwa mazoea, ujanja ujanja na kutoa taarifa za michakato badala ya majibu yanayotakiwa.

Amesema hayo Bungeni leo (Jumanne, Januari 27, 2026) wakati akitoa hoja ya kujadili hotuba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa jijini Dodoma wakati akizindua Bunge la 13 Novemba 14, 2025.

“Tunapozungumzia utendaji Serikalini, msisitizo ni uadilifu na uwajibikaji wa Serikali kwa wananchi waliotuchagua ili kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali za nchi pamoja na kupata huduma wanazostahili.”

Dkt. Mwigulu amesema kuwa hotuba aliyoitoa Rais Dkt. Samia ilitoa mwelekeo na dira ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha pili. “Hotuba ya Mheshimiwa Rais ilitoa maelekezo na kubainisha changamoto pamoja na majukumu yanayotupasa kuyatekeleza kwa kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa maendeleo.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kutekeleza vipaumbele vyote vilivyoainishwa. “Serikali imeainisha maeneo mbalimbali ya utekelezaji na kupanga mipango kazi ya utekelezaji wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu, na tayari utekelezaji wake umeshaanza kutekelezwa kwenye maeneo kadhaa”.

Baraka Tele na Mafanikio kwa Mama wa Taifa – Mhe. Dkt. Samia Suluhu HassanNa: comrade David Michael mlope (Zola d King K...
27/01/2026

Baraka Tele na Mafanikio kwa Mama wa Taifa – Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Na: comrade David Michael mlope (Zola d King

Katika siku hii adhimu ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, tunamwombea baraka tele, afya njema, na mafanikio yasiyo na kikomo Rais wetu mpendwa, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan – mama wa taifa, kiongozi wa kipekee, na dira ya matumaini kwa Watanzania wote.

Mhe. Rais Samia ni mfano wa uongozi wa hekima, uvumilivu, na maono ya kweli. Tangu alipochukua hatamu za uongozi, ameendelea kuonyesha dhamira ya dhati ya kuijenga Tanzania mpya – yenye usawa, maendeleo jumuishi, na heshima kwa utu wa kila Mtanzania. Kupitia kauli mbiu yake ya “Kazi na Utu”, amekuwa akihimiza maendeleo yanayozingatia haki, mazingira, na ustawi wa jamii.

Kupanda mti wa Muembe katika ardhi ya Bungi Kilimo, Unguja, si tu tukio la kimazingira bali ni ishara ya uhai, urithi, na matumaini. K**a mti huo utakavyokua na kuzaa matunda, ndivyo pia uongozi wake unavyoendelea kuzaa matunda ya maendeleo, mshik**ano, na heshima kwa taifa letu.

Tunamwombea:

- Baraka za Mungu katika kila hatua ya maisha na uongozi wake
- Afya njema ili aendelee kulitumikia taifa kwa nguvu na ari
- Hekima na busara katika kufanya maamuzi ya kitaifa
- Upendo wa wananchi na mshik**ano wa kitaifa
- Mafanikio ya kudumu katika juhudi za kuijenga Tanzania ya kisasa na endelevu

Kwa niaba ya Watanzania wote wenye mapenzi mema, tunasema:

Heri ya kuzaliwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan – mama yetu wa pekee, kiongozi wetu wa kipekee. Mungu akulinde, akubariki, na akufanikishe zaidi.





Address

SalaSala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uongozi na siasa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share