05/06/2026
Akikabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchini leo 5.6.2026 jijini Dodoma amesema tuzo hiyo imetolewa kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kutambua mchango wake mkubwa katika kuendeleza kilimo himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi na matumizi endelevu ya rasilimali za asili na uwekezaji katika teknolojia rafiki kwa mazingira.
Tuzo hiyo imepokelewa na Bi. Hawabai Adbulla kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji akiambatana na Bw. Alex Ndikile Katibu wa Mkurugenzi Mtendaji.