Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Ukurasa rasmi wa Facebook wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

04/09/2026

MADIWANI JIJI LA DAR WAPITISHA MPANGO MKAKATI WA UBIA (PPP) KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS.

Na:Shalua Mpanda

Baraza la Madiwani la Halmashuri ya Jiji la Dar es salaam kwa kauli moja wamepitisha azimio la kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha Jiji hilo linakuwa safi kwa kushirkisha sekta binafsi katika zoezi la usafishaji wa Mazingira na uzoaji wa taka katika Halmashuri hiyo.

Akizungumza katika Baraza hilo maalum Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ndugu Elihuruma Mabelya amesema kutokana na ongezeko kubwa la watu katika Jiji la Dar es salaam, uzalishaji wa taka umeongezeka hali inayofanya maeneo mengi kuwa na mrudikano wa taka.

Mkurugenzi Mabelya aliomba Baraza hilo kuridhia mchakato wa kuingia ubia kati ya Halmashauri na sekta binafi ili kuweza kumpata mkandarasi atakayekuwa na uwezo wa kufanya kazi ya kukusanya na kuhudumia dampo la Pugu.

"Ni ukweli usiopingika kuwa uondoshaji wa taka katika Halmashuri ya Jiji letu hauendani na kasi ya uzalishaji wa taka hizo, hivyo mpango huu wa PPP (Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi) hatuwezi kuuepuka, hivyo naomba mridhie mpango huu". Alisisitiza Mkurugenzi Mabelya

Diwani wa kata ya Ukonga Mhe. Ramadhan Bendera ameusifu mpango huo huku akitolea mfano wa hali halisi ya dampo la Pugu kuzidiwa kwa kukosa wakandarasi wenye uwezo ambao wanaweza kuhudumia dampo hilo.

Baada ya Mkurugenzi huyo wa Jiji kuomba Baraza hilo kupitisha ajenda hiyo, Madiwani wote waliafiki pendekezo hilo na kuruhusu timu ya menejimenti ya Halmashauri kuendelea na mchakato huo.

Ikumbukwe hivi karibuni Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa kuapisha baadhi ya viongozi aliowateua, pamoja na mambo mengine alionesha kuchukizwa na hali ya uchafu katika maeneo mengi ndani ya mkoa wa Dar es salaam na kuagiza viongozi kusimamia suala la usafi kwenye maeneo yao.

02/09/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Wakuu wa Mikoa kusimamia usafi katika maeneo yao, akizungumzia Miji mikubwa ikiwemo Dar es salaam, ambayo amesema baadhi ya maeneo yake bado hayaridhishi kwa usafi.

Akizungumza leo Septemba 2, 2026 baada ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala katika Ikulu ya Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema, “Dar es salaam, huko vichochoroni Mji ni mchafu mtupu.”

“Dar es salaam ni usoni tu, City Center nenda mpaka Ferry, angalia huko kunavyotazamika, lakini huko vichochoroni ni mchafu mtupu, na kwa kweli haipendezi, Miji mikubwa haipendezi kuwa michafu.”

“Mji ukiwa mchafu inamaanisha na wewe mwenyewe ni mchafu, kwa sababu anayejua uchafu ni nini haruhusu uchafu ukae kwenye maeneo yake.”

UHUSIANO KATI YA HALMASHAURI YA JIJI NA WADAU WAMVUTIA DC MPOGOLO.Na: Shalua MpandaUhusiano mzuri uliopo kati ya uongozi...
01/09/2026

UHUSIANO KATI YA HALMASHAURI YA JIJI NA WADAU WAMVUTIA DC MPOGOLO.

Na: Shalua Mpanda

Uhusiano mzuri uliopo kati ya uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na wadau mbalimbali wa maendeleo umemfurahisha Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mheshimiwa Edward Mpogolo na kuwataka wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hasa katika utunzaji wa Mazingira.

Akizungumza wakati wa kupokea msaada wa mapipa (Dustbin) 100 ya kuhifadhia taka kutoka Jumuiya ya Singasinga katika ofisi za Halmashauri ya Jiji, Mpogolo amesema uhusiano mzuri uliopo kati ya Uongozi huo na wadau ndio unasababisha wadau hao kujitoa kwa hali na mali.

Mkuu huyo wa Wilaya amewahakikishia kuwapa ushirikiano wadau wote wa maendeo katika wilaya ya Ilala ili kutimiza dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuleta tabasamu kwa wananachi.

"Sisi k**a Serikali tunataka kutumia dhamira ya Mhe. Rais wetu kuhakikisha Mazingira yanatunzwa na kwa kuwa yeye ni kinara kwenye Mazingira basi tuna imani tutafanikkwa”. Alisema Mpogolo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ya Singh ndugu Jasdeep Babhra amesema wamekuwa wakishirikiana mara kwa mara na Serikali hasa katika ujenzi wa visima vya maji na utunzaji wa mazigira.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ndugu Elihuruma Mabelya.

DC MPOGOLO:UCHAKATAJI TAKA NI FURSA YA AJIRA NA KIPATO KWA WANANCHI. Na:Samira RamadhanMkuu wa Wilaya ya Ilala Mheshimiw...
30/08/2026

DC MPOGOLO:UCHAKATAJI TAKA NI FURSA YA AJIRA NA KIPATO KWA WANANCHI.

Na:Samira Ramadhan

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mheshimiwa Edward Mpogolo ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya
Jiji la Dar es Salaam kwa kuunga mkono mabadiliko chanya katika sekta ya
usafi kwa kushirikiana na wadau wa usafi kampuni ya "Nipe Fagio" katika utekelezaji wa mfumo wa uchakataji
taka( Zero Waste) katika Kata ya Bonyokwa.

Ameyazungumza hayo Agosti 29,2026 katika hafla ya makabidhiano ya kituo hicho cha mfumo wa uchakataji taka kati ya
Kampuni ya Nipe Fagio na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhe.
Mpogolo amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa jitihada za Serikali katika
kuboresha usafi na utunzaji wa mazingira.

Mkuu huyo wa Wilaya amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ndugu
Ellihuruma Mabelya pamoja na timu yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa
sekta binafsi kwa kupokea maagizo ya Serikali kwa kuendelea kutumia vifaa vya kisasa,
akisema hatua hiyo itasaidia kuboresha zaidi usafi wa Jiji la Dar es Salaam.

“Nitumie nafasi hii kumpongeza Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kwa kupokea
mabadiliko chanya katika Jiji letu kupitia kushirikiana na Nipe Fagio katika mradi huu,”Alisema Mpogolo.

Aidha amewataka wadau kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali
katika sekta ya usafi na kuwataka wananchi kushirikiana katika kutunza mazingira na kupitia
mradi huu wa uchakatajii taka unaoenda sambamba na Dira ya Taifa ya
maendeleo 2050.

Kituo hicho cha uchakataji taka sifuri ( Zero Waste)
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kimefungua njia kwa vitendo, utekelezaji wa maelekezo ya
Serikali katika kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika utunzaji wa Mazingira.

30/08/2026
TUNA WAJIBU KUSHUGHULIKA NA  SHIDA ZA WATU-DC MPOGOLONa:Shalua MpandaWatendaji wa Serikali kuanzia ngazi za mtaa hadi wi...
29/08/2026

TUNA WAJIBU KUSHUGHULIKA NA SHIDA ZA WATU-DC MPOGOLO

Na:Shalua Mpanda

Watendaji wa Serikali kuanzia ngazi za mtaa hadi wilaya wametakiwa kushughulika na kutatua shida na changamoto za wananchi katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa leo hii na Mkuu wa wilaya ya Ilala Mheshimiwa Edward Mpogolo wakati wa zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira katika kata za Chanika na Zingiziwa.

Mhe. Mpogolo amesema viongozi hao wameaminiwa na Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa leongo la kumsaidia katika maeneo yao hivyo hawana budi kuhakikisha wanazichukua changamoto za wananchi k**a zao.

"Mheshimiwa Rais anajitahidi sana kuleta fedha za miradi ya maendeleo katika maeneo yetu, yeye hawezi kuja kutatua shida ndogondogo za watu, shida hizi ni zetu sisi". Alisema

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kwa kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha na kuwataka viongozi wa Halmshauri hiyo kuendelea kusimamia uadilifu.

Zoezi hilo la upandaji miti lililoongozwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mhe. Bakari Shingo limefanyika Zahanati ya Nzasa kata ya Zingiziwa likihusisha wadau mbalimbali wa Mazingia wakiwemo Chama cha Skauti Tanzania.

28/08/2026

DAR CITY YATWAA UBINGWA MPIRA WA WAVU WANAWAKE 2026.

28/08/2026

Address

1, Mission Street
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam:

Shortcuts

Share