Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila

Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila A Place Of The Word, Power, Holiness, Greatness And Impactful Teachings

UNAPOPATA NAFASI YA KUKUTANA NA MTU ANAYEFANYA JAMBO K**A LAKO NA ANAKUZIDI UZOEFU AU MATOKEO1. Usiende kumuona bila seh...
21/08/2026

UNAPOPATA NAFASI YA KUKUTANA NA MTU ANAYEFANYA JAMBO K**A LAKO NA ANAKUZIDI UZOEFU AU MATOKEO

1. Usiende kumuona bila sehemu ya kuandika hekima kadhaa utakazopata kwake za kukupa hatua kwenye unachofanya au unachotaka kuwa

2. Ukifika muoneshe adabu, shuka, hata k**a atakusifia au kueleza unavyofanya vizuri, ili kuepuka kujiweka daraja moja na kumfanya asiseme mengi k**a mkubwa kwa mdogo

3. Sikiliza zaidi na ikiwezekana ongea tu mahali pa kushukuru, au kuuliza au kutaka ufafanuzi tu, Wewe sio mshirika mwenza wa hilo daraja, wewe ni mpokeaji wa hekima

4. Hakikisha umeandaa orodha ya maswali unayotaka kuuliza kabisa, na usiulize maswali ili uchangie unachojua, uliza ili yeye akupe siri na hekima

5. Uliza maswali yale tu ambayo akiyajibu kwa ufasaha ukapata nuru yatakupa hatua zaidi kwenye unachofanya

6. Usiongelee kabisa habari zako au mambo yako labda endapo amekuuliza, umekwenda kujifunza na si kuonesha mafanikio yako

7. Hata k**a huyu mtu ni mnyenyekevu, yuko simple mno, usilete mazoea k**a vile ni mtu wa daraja lako, mazoea yanakata flow ya moyo wa mtu mkuu kusema na kufunua mengi bali heshima na adabu ya waziwazi itakufungulia milango mikubwa kwa mhusika

8. Unapokwenda kwa mtu mkuu, usiende mikono mitupu, beba sadaka au zawadi iliyo kwenye ngazi au daraja lake, inaweza kuwa fedha ambayo hujawahi kuitoa kokote, kinaweza kuwa kitu ambacho kwako ni ghali (expensive, valuable)
Mioyo ya wakuu hufunguliwa na zawadi ya mtu!

9. Mruhusu akuambie mambo yapi kwako uyaondoe au uyaache ili uwe mtu bora
Usijitetee au kujieleza sana anapokuambia kuhusu makosa, madhaifu na yale ambayo hufanyi vizuri, maana kila mtu anapenda zaidi kuambiwa upande wake wa nguvu na hataki kuguswa upande wa marekebisho!

10. Uyazingatie hayo mambo tisa juu na yatakufanya uwe bora katika uyatendayo

Askofu Dickson Cornel Kabigumila
ABC GLOBAL DUNIANI

15/08/2026

NINI MAANA YA KAZI
NINI TOFAUTI YA KAZI NA AJIRA?
MUNGU HUBARIKI KAZI LAKINI SI KILA KAZI,
SIKILIZA HII NA UAMKE SASA KUELEKEA KAZI ULIYOUMBIWA,

Askofu Dickson Cornel Kabigumila
ABC GLOBAL DUNIANI

MARA HATUKUONI TENA ONLINETUNAAMBIWA UMESHAKUFA MUDA MBONA...SIKU moja tunatazama HATUKUONI TENA ONLINE! Hatuoni tena ST...
15/08/2026

MARA HATUKUONI TENA ONLINE

TUNAAMBIWA UMESHAKUFA MUDA MBONA...

SIKU moja tunatazama HATUKUONI TENA ONLINE! Hatuoni tena STATUS ZAKO wala POST ZAKO Facebook au Instagram! Timu yako ya Simba au Yanga imebeba ubingwa wewe haupo tena kupost kwa sababu MUDA WAKO WA KUISHI UMEISHA, UMEKUFA, HAUKO TENA DUNIANI...

Kitakachokuwa na maana muda huo si UMEOA, NI MCHUNGAJI, NABII, MFANYABIASHARA, AU CHEO CHOCHOTE.

Kitakachokuwa na maana wakati huo ni k**a UMEMPOKEA YESU K**A BWANA NA MWOKOZI WAKO (Yohana 3:16-18, Yohana 1:12, Yohana 14:6), na SI KUMPOKEA TU YESU, BALI UNAISHI MAISHA MATAKATIFU NDANI YA WOKOVU (Waebrania 12:14, Zaburi 16:3)!
SIKU HIYO HAIKO MBALI MNO, KILA UKIONA SIKU MPYA, UMEIKARIBIA MNO!

K**a kweli wewe ni muwazi,
K**a kweli wewe ni mkweli kwako na Mungu,
Na huu ujumbe unasema na moyo wako,
Na umegundua umekwama DHAMBINI na aina hii ya ujumbe inautisha moyo wako,
Naomba uje inbox WhatsApp 0655 466 675,
Nitakusaidia kwa upendo, kwa usiri, kimya kimya, na utavuka na kushinda jumla!

NILIZALIWA KUWA SABABU YA WENGI KWENDA MBINGUNI, NA KUISHI MAISHA YA USHINDI DHIDI YA DHAMBI BILA KUJIKAZA, BALI K**A MATOKEO YA KUTEMBEA NA MUNGU KIBINAFSI!

Pastor Dickson Cornel Kabigumila,
Rafiki wa mwenye DHAMBI anayependa kubadilika,
Niliye tayari kusimama nawe!

14/08/2026

Kizazi cha wacha Mungu,
Kizazi cha wazalendo.

SABABU 5 KWANINI HUWEZI KUMBADILI MWANAUME AMBAYE HAJAOKOKA UNAYETAKA AKUOE NA UMBADILISHE1. Umeanzisha kitu kipya nje y...
14/08/2026

SABABU 5 KWANINI HUWEZI KUMBADILI MWANAUME AMBAYE HAJAOKOKA UNAYETAKA AKUOE NA UMBADILISHE

1. Umeanzisha kitu kipya nje ya NENO LA MUNGU
-Hatuwahubirii watu habari za Yesu kwa ajili ya KUSUDI la kuwaoa au kutuoa bali ili wasipotee bali WAWE NA UZIMA WA MILELE (Yohana 3:16-18)!
-Msingi wa wanaotaka kuoa au kuolewa kwenye mwili wa Kristo tayari umewekwa ya kwamba "usifungiwe nira na asiyeamini kwa jinsi isiyo sawasawa" ikiwemo kwa mfumo huo wa nitaoelewa naye nimgeuze (2Wakorintho 6:14)!

2. Jiambie ukweli, tangu mwaka umeanza nje ya huyo "asiyeokoka" unayetaka uolewe naye umbadilishe, NI WANAUME WANGAPI UMEWAHUBIRIA HABARI ZA YESU NA WAMEOKOKA, WAKASIMAMA NA WANAENDELEA MBELE NA MOTO WA MUNGU KANISANI?

-K**a huna wanaume ambao ni MAVUNO yako kwa Yesu kwa njia ya INJILI, kinachokupa UHAKIKA kwamba utamuokoa na kumgeuza "asiyeamini" ukiolewa naye ni kipi? Mbona unapima kina cha maji kwa miguu yote miwili, si kichaa hiki kimekupata? Jiambie ukweli, hutaweza, unachezea shilingi kwenye tundu la choo, ni MCHEZO HATARI huo!

-Unafikiri MWANAUME ambaye anajua tayari moyo wako haumchukulii k**a "mavuno kwa Yesu" bali "darling" au "babe" atakubali umuamulie misingi ya anayoyaamini?
Endelea kucheza k**ari hiyo halafu utakuja kuwasimulia wanao na wajukuu namna ULIVYOLIWA KEKUNDU!

3. Hadi unakutana naye, k**a hajaokoka, na k**a hajafika kanisani, na INJILI inavyohibiriwa kila mahali, si kwenye TV, si kwenye redio, si mitandaoni, si kwenye magari nakadhalika, UNAHISI WEWE MPENZI WAKE NDIYE UNA INJILI AMBAYO INACHOMA MOYO WA MTU NA KUMFANYA ASEME NIFANYE NINI NIPATE KUOKOKA? Acha utani mrembo, kichwa chako kina shida!
-Hapo ulipo hauhusiki na injili kokote, si mtandaoni, si ushuhudiaji mitaani, na unataka uugeuze moyo wa MWANAUME sio? Una utani wewe mdada!

4. Hivi unafahamu, kuna watu ambao piga ua garagaza, hawatakuja KUOKOKA na hawakuja kuingia uzimani ingawa Bwana Yesu keshawafanyia kila kitu... Unaweza kukuta mmoja wa hao watu walioshindikana ni huyo baharia unayetaka AKUOE UMBADILISHE...

Ikitokea ikawa hivyo, utaweza KUISHI KWENYE NDOA ya namna hiyo hadi KIFO au utatafuta vifungu kwamba ni mzinzi ili uachike na kuweka rekodi ya kuolewa zaidi ya mara moja?
Unajua nini? Pressure yako ya kuolewa si kubwa KULIKO hatari ya kuangukia kwenye mikono ya mnyang'anyi k**a mtu yule aliyekuwa akielekea Yerusalemu!

5. Anayewaokoa watu na dhambi zao ni Yesu Kristo tu na si NDOA (Mathayo 1:21)!

-Hakuna kokote maandiko yanasema uoe au uolewe na asiyeamini halafu utambadilisha wewe, bali kuna maelekezo kwamba IKITOKEA KATI YA WANANDOA WAWILI WALIOOANA KABLA YA KUMPOKEA YESU, NA MMOJA AKAIPATA NEEMA YA WOKOVU, HALAFU KULE KUOKOKA KWAKE KUSIMKERE WALA KUMKWAZA YULE MWENZA ASIYEOKOKA, BASI ASIMWACHE, AKOMAE NAYE NA MUNGU ATAFANYA MUUJIZA NAYE AIPATE NEEMA YA WOKOVU, hii si ya walio nje ya NDOA, ni ya waliokuwa tayari kwenye NDOA (1Wakorintho 7:12-15)!

SASA WEWE RUKARUKA UYAKANYAGE,
MBONA UTAIMBA HALLELUJAH PEKE YAKO,
TUTAKUWA TUMEKAA PALEEEE TUNAKUCHORA,
HATUINGILII MAJANGA YASIYOTUHUSU,
TUKIJIKAZA TUTAKUSENG'ENYA KWAMBA ULIACHA WOKOVU ILI UKAOLEWE NA UTAUMIA ZAIDI,
BINTI YANGU SUMU HAIJARIBIWI KWA KUIONJA!

Bishop Dickson Dickson Cornel Kabigumila
ABC GLOBAL DUNIANI

KILA UKITAKA KUKATA TAMAA JIKUMBUSHE HAYA1. Mungu ana wewe mmoja tu tangu dunia ianze hadi itakapoisha●Kabla yako hakuku...
13/08/2026

KILA UKITAKA KUKATA TAMAA JIKUMBUSHE HAYA

1. Mungu ana wewe mmoja tu tangu dunia ianze hadi itakapoisha

●Kabla yako hakukuwa na wewe mwingine
●Wakati huu unapoishi, dunia nzima ya watu zaidi ya bilioni 8, upo wewe mmoja dunia nzima, hivyo kokote utakapokwenda wana uhitaji na mtu aina yako
●Baada ya wewe kuondoka duniani, hakutakuwa na wewe mwingine milele
JIKUBALI, JIAMBIE UKWELI HUU AMBAO SHETANI HATAKI UUJUE NA KUUSHIKA MAANA UTAKUPA THAMANI, KUJIAMINI NA KUJIPENDA!

2. Jiambie ukweli kwamba KUNA MTU AU KUNDI LA WATU linasubiri uvuke au ushinde ili kupitia wewe na wao WAJIPATE NA KUPIGA HATUA!
Yaani, kila mmoja wetu, maisha yako yameungwa na ya mtu mwingine ambaye huenda hata sasa humjui, UKIFANYA VIZURI, huyo mtu atafanikiwa kuwa yeye au kupiga hatua zake kupitia wewe!
KUKATA TAMAA NI KUWADHULUMU WENGINE MEMA YAO ULIYOBEBA NDANI YAKO!

3. Nyakati ngumu hazidumu bali watu wagumu udumu,
Iko wapi Covid 19?
Iko wapi gharika ya Nuhu?
Iko wapi miaka 430 ya utumwa Misri?
KILA HALI NA KILA KITU KWENYE MAISHA HATA KIWE KIGUMU KIASI GANI, KINA EXPIRED DATE, SI CHA KUDUMU, WALE WANAOKAZA MIKANDA NYAKATI ZA MITIKISIKO NDIO HUBAKI KULA MEMA MABAYA YAKISHAPITA, DON'T GIVE UP!

4. Hivi unajua unaweza kuwa umetumwa kugeuza aibu, vilio na historia mbaya za familia, ukoo au ulipotoka, na bahati mbaya unataka kukata tamaa kizembe?
WAGEUZA HISTORIA WOTE HAWAJAWAHI KUWA NA NJIA RAHISI,
WAANDIKA HISTORIA MPYA WAMEZIANDIKA KWA MACHOZI, JASHO NA HATA DAMU,
SASA WEWE KATA TAMAA KIJINGA UISHIE NJIANI, SISI TUTAENDELEA BILA WEWE!

Askofu Dickson Kabigumila
ABC GLOBAL DUNIANI

12/08/2026

How DIVINE IDEA can change your economical status,

The story of A PRODIGAL SON

LUKE 15:11-32

12/08/2026

KAZI NI NINI??!

MAFANIKIO NI NINI??!

JIFUNZE MAANA HALISI YA KAZI NA MAFANIKIO KUTOKA KWA MTUMISHI WA MUNGU

Bishop Dickson Cornel Kabigumila

ABC GLOBAL FILMSPresenting...CHOZI LA BINTI MLOKOLE || OFFICIAL MOVIE TRAILLERTO BE OUT  THIS WEDNESDAY> 🗓️ July 29, 202...
27/07/2026

ABC GLOBAL FILMS
Presenting...

CHOZI LA BINTI MLOKOLE || OFFICIAL MOVIE TRAILLER

TO BE OUT THIS WEDNESDAY

> 🗓️ July 29, 2026
> 🕕 6:00 PM

SUBSCRIBE now! 🚀
Don't just watch, join the movement. Hit the subscribe button 👇

https://youtube.com/?si=Bb9-26jnQpF45Ju5

Address

Kinzudi
Dar Es Salaam
14123

Opening Hours

Saturday 08:00 - 17:00
Sunday 08:00 - 17:00

Telephone

+255655466675

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Mwalimu Dickson Cornel Kabigumila:

Shortcuts

Share