COSTECH

COSTECH page of Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) | Get update of whats Happening in Tanzania Research,Technology and Innovation.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Abdulla Rashid Abdulla wame...
21/08/2026

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Abdulla Rashid Abdulla wametembelea jengo la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STI Complex) jijini Dodoma tarehe 21 Agosti, 2026 na kupongeza hatua ya ujenzi ilipofikia.

Aidha k**ati hiyo imeiasa menejimenti ya COSTECH kuhakikisha inafuatilia kwa ukaribu ili kuhakikisha ujenzi unakamilika k**a ulivyopangwa.

DKT. NUNGU: VIJANA BUNIFU ZISIISHIE KWENYE MAKABRASHA NA MAONESHO PEKEE, ZIZALISHE AJIRA NA KUONGEZA KIPATO.Tanga.Raj hi...
20/08/2026

DKT. NUNGU: VIJANA BUNIFU ZISIISHIE KWENYE MAKABRASHA NA MAONESHO PEKEE, ZIZALISHE AJIRA NA KUONGEZA KIPATO.

Tanga.

Raj hiyo imetolewa na
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, kwa ametoa kwa vijana wabunifu wa Tanzania kuhakikisha bunifu zinabiasharishwa na kufika Sokoni ili Zizalishe kipato , Ajira na kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania. Kauli hiyo ameitoa tarehe 19 Agosti, 2026, wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu - iliyozinduliwa rasmi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof Adolf Mkenda, kuanzia tarehe 15 - 24 Agosyi inayoendelea, Viwanja vya Usagara- Jijini Tanga.

Wiki hii ya kitaifa ilitangazwa imewakutanisha wadau kutoka wizara mbalimbali, Vyuo vya elimu ya juu, Vyuo vya ufundi na ufundi stadi, mashirika ya utafiti na sekta binafsi, huku zaidi ya taasisi 300 zikishiriki chini ya kauli mbiu "_Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050_," jukwaa linalolenga kufikia uchumi wa dola trilioni 1 ifikapo mwaka 2050, na kuwezesha kipato cha wastani cha mtu mmoja kati ya Dola za Marekani 7,000–12,000, na ajira zenye staha kwa angalau asilimia 50 ya Watanzania.

Aidha, Dkt. Nungu amesisitiza kuwa ubunifu si zoezi la kitaaluma pekee, bali unapaswa kutumika kujiajiri na kutatua matatizo halisi ya jamii, akieleza kwamba maelfu ya vijana wanahitimu vyuo kila mwaka bila ajira wakati bunifu nyingi nzuri za Kitanzania zinakwama katika hatua ya wazo tu bila kuwahi kufika sokoni — hali inayogeuza ubunifu kutoka kitu kinachoonekana k**a shughuli ya vijana wenye vipaji peke yao kuwa chombo cha sera ya ajira kwa jamii nzima ya vijana.

Pia, Ameongeza kuwa maandalizi ya wabunifu hayapaswi kuanzia chuoni au baada ya kuhitimu bali tangu ngazi ya shule, huku akiwataka vijana kujifunza na kushirikiana na wadau wengine ili kutafsiri mawazo yao kuwa bunifu zinazoweza kutumika na Watanzania wa kawaida.
Tofauti na matamko ya kawaida ya kihamasisho, msimamo huu unaungwa mkono na mfumo halisi wa uwezeshaji: kupitia Mfuko wa Taifa wa Uendelezaji Sayansi na Teknolojia (NFAST, maarufu k**a MTUSATE).

" COSTECH imeshatoa dhamana za mikopo na seed funding zenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni TZS. 129 kufadhili tafiti na bunifu za vijana, kati ya hizo zaidi ya Shilingi bilioni TZS. 85 zikitoka moja kwa moja Serikalini. Aidha, madawati 90 ya sayansi na ubunifu yameanzishwa katika halmashauri mbalimbali nchini k**a njia ya kuwafikia vijana wa vijijini na si wale walio karibu na miji mikuu pekee, huku mpango wa MAKISATU ukishazalisha wabunifu 268 na kusaidia kusajili rasmi kampuni changa 23 za vijana — yote haya yakija wakati COSTECH ikitimiza miaka 40 tangu kuanzishwa kwake" amesisitiza Dkt. Nungu.

PROF CAROLINE NOMBO : UENDELEZAJIRASILIMALI WATU, NJIA SAHIHI KUFIKIA DIRA 2050. Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wi...
19/08/2026

PROF CAROLINE NOMBO : UENDELEZAJIRASILIMALI WATU, NJIA SAHIHI KUFIKIA DIRA 2050.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara. Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo wakati wa Ufunguzi wa Kilele cha Maadhimishoya Wiki ya Kitaifa, Elimu , Ujuzi na Ubunifu, wakati akitoa Salamu za Ukaribisho wa mgeni rasmi aliyekuwa Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, mhe. Prof. Adolf Mkenda (mb) , tarehe 18 Agosti 2026 - Viwanja vya Usagara- Jijini Tanga.

Prof Nombo amewashukuru viongozi Mawaziri, naibu Waziri, wakuu wa Taasisi na Bodi zao na wanachi kutenga muda kushiriki pamoja na Taasisi za wizara hiyo ikiwemo NACTVET , COSTECH na wadau wote waliokuja kuadhimisha Wiki hiyo kitaifa

Aidha, Prof Nombo kufanyika kwa maonesho hayo kila mwaka kuna lengo la kukutanisha wadau ili kutoa taarifa , kujadili , kubadilishana uzoefu na kupeana taarifa kwa maendeleo ya Taifa letu. Huku kauli mbiu ya maonoesho hayo ikilenga kufikia maendeleo ya dira 2050 na Serikali inatambua elimu, utafiti na maendeleo ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu k**a nyenzo muhimu ya maendeleo

Mashindano ya Ujuzi na Bunifu kwa Washindi watapewa tuzo siku ya kuhitimisha maadhmimisho hayo " world skills Tanzania " ukilenga kuimarisha ujuzi kwa vitendo kwa wanafunzi na ufundishaji katika shule mbalimbali kwa kuzingatia sifa na vigezo huku mshindi wa kwanza atashiriki karina mashindano haya

Pamoja na hayo amefafanua, Wiki hii inafungamanisha wadau wa kisekta na kuongeza mnyororo wa thamani na matumizi ya uchumi-maarifa unachagizwa na utekelezaji wa mabadiliko ya mitaala ya elimu msingi, elimu ya juu, msingi na Sekondari na pamoja na elimu ya ufundi . Nakutoa Rai kwa Wadau kuendelea kujitokeza katika Warsha ya majadiliano ya pamoja ya mamlaka za Udhibiti Ubora (regulatory authority) k**a BRELA, PPRA , TRA na TISEZA kuwezesha utoaji wa elimu na hakimiliki kwa watafiti na wabunifu , ugawaji wa tuzo kwa watafiti washindi walioachapisha katika majarida ya hadhi ya juu ya kimataifa

MHESHIMIWA MHANDISI MUNDE , APONGEZA JITAHADA ZA WIZARA YA ELIMU KUTEKELEZA AHADI YA TRILIONI 2.8 KWA ASILIMIA 100,% Tan...
19/08/2026

MHESHIMIWA MHANDISI MUNDE , APONGEZA JITAHADA ZA WIZARA YA ELIMU KUTEKELEZA AHADI YA TRILIONI 2.8 KWA ASILIMIA 100,%

Tanga.

Kongole hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde alipomwakilisha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis M***a Omar, wakati wa ufunguzi wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu , tarehe 18 Agosti 2026 na kueleza kuwa Serikali kupitia wizara hiyo itahakikisha inatekeleza kikamilifu mipango ya maendeleo inayolenga kufanikisha Dira ya 2050.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika Tanga wiki hii — ile ile iliyohudhuriwa na viongozi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Elimu — Mhe. Munde alieleza kuwa amekuja kuwaelekeza wananchi wa Tanga jinsi serikali inavyotekeleza maendeleo chini ya Dira 2050 na hatua iliyofikiwa hadi sasa.

Aidha, Mhe. Munde ameeleza kuwa utekelezaji wa mipango yote ya maendeleo ni matokeo ya moja kwa moja ya maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mipango, dira na utekekelezaji wa bajeti za Serikali hususani elimu iliyotengewa kiasi cha TZS Trilioni 2.8 kwa mwaka wa fedha ulioisha ili kuhakikisha inatekeleza kikamilifu mageuzi ya sekta ya Elimu kwa ujumla.

Amefafanua kuwa Serikali kupitia Wizara hiyo inaahidi kuendeleza sekta ya elimu ili iweze kuzalisha nguvu kazi ya rasilimali yenye maarifa yakutisha kutafsiri kwa vitendo maono ya dira 2050.

"Wizara ya Fedha haitamuangusha" Rais katika kutekeleza kiasi cha shilingi trilioni 2.8, akisisitiza utekelezaji huo utafikiwa kwa asilimia 100%.
Fedha hizo zinalenga kuwezesha mipango ya maendeleo ikiwemo: ujenzi wa mashule, utoaji wa mikopo, na kuwezesha Baraza la Mitihani." Aliongeza mhe. Munde.

Aidha, Mhe. Munde ameongeza kuwa Wizara itaendelea kutekeleza maelekezo ya mgeni rasmi kuelekea uchumi wa viwanda unaochagizwa na ujuzi, na kufanya hilo kuwa kipaumbele chake ili kurahisisha utekelezaji wa malengo ya Dira 2050 kwa kurejesha Hadhi ya Tanga k**a kitovu cha kiuchumi — nafasi mkoa huo uliyokuwa nayo miaka ya 1970 na 1980 — ikichochea Mkoa huo kukua kwa kasi kubwa. Ameahidi kuwa Wizara ya Fedha itahakikisha jambo hilo linafanikiwa mwaka huu.

MHE. SEKIBOKO : UBUNIFU SI MAPISHI YA CHAI YA N**I NA NANASI PEKEE, VIJANA TUMIENI FURSA YA MAONESHO KUENDELEZA UJASIRIA...
19/08/2026

MHE. SEKIBOKO : UBUNIFU SI MAPISHI YA CHAI YA N**I NA NANASI PEKEE, VIJANA TUMIENI FURSA YA MAONESHO KUENDELEZA UJASIRIAMALI KUKUZA MATUMIZI YA UCHUMI MAARIFA.

Tanga.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni, Mhe. Husna Sekiboko (mb) amepongeza jitihada zinazofanywa na Wizara hiyo kuboresha ya mitaala inayochochea ujuzi na bunifu zaidi ili kutatua changamoto zinazoikabili jamii na huduma za kudumu za jamii

" Mgeni rasmi nimepewa fursa ya kutoa salamu kwa mfupi sana,tumeshaanza utekelezaji wa dira ya 2050 na kazi kubwa inayofanywa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia iliyobeba maono na pia ninampongeza Waziri wa Elimu na Timu nzima ya Wizara kwa kutafsiri kwa vitendo maono haya" alisema Mhe. Sekiboko.

Alizungumza katika ufunguzi wa Wiki hiyo, Mhe Sekibo akimwakilisha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azan Zungu (mb) ametoa salamu za Spika huyo na kuelekeza kuwa Mhe. Spika anatambua uwepo wa Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu na pia Kamati na Bunge kwa pamoja tumeshirikiana vizuri na tunaahidi kuwa tutaendelea kuwa mabalozi wazuri katika kuzungumza mema ya sekta ya elimu, akirejea kuwa Mnamo mwaka 2022 Serikali ilielekeza Maonesho ya MAKISATU kufanyika Kitaifa ilikubaliwa kuwa matamasha na mashindano hayo kufanyika Tanga kwa mwaka 2023 na kupokelewa Mwenyeji wako aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dkt Batilda Buriani pamoja na kufanyika kwa miaka 3 mfululizo

" Kwa niaba ya wananchi wa Tanga - tunaishukuru Wizara kuleta Maoneosho haya hapa na tumeona miaka 3 yakipiga hatua mwaka hadi mwaka na kuimarisha mwamko wa wananchi wengi kushiriki zaidi na kunufaisha mikoa ya jirani ikiwemo, Bunifu zinazotatua Changamto na zitaongezewa wigo wa ushirikiano kati Sekta ya Elimu na Sekta binafsi ili kuwawezesha wabunifu wachanga wasiishie kwenye maonesho pekee na hatimae kusaidia jamii inayoizunguka" aliongeza.

Ametoa rai kwa vijana kubadilika na kuachana na Utamaduni wa kuona bunifu pekee ni mapishi ya chai ya n**i na nanasi pekee hivyo Wiki hii ya Maeonesho itumike kunufaisha wajasiriamali wadogo ikiwemo mama na baba lishe kuona maonesho haya ni fursa na tuendelee kuonesha uhodari wa Tanga kupokea maonesho haya kila mwaka.

" Maonesho haya yamedumu kwa miaka 5 sasa na bunifu zinye tija zitapewa kipaumbele zaidi ili ziweze kubiasharishwa na kutumia ujuzi kuongeza tija ya uzalishaji kutoka kwenye kifaa cha mfano ' Prototype' na kuwezesha uzalishaji wa bidhaa halisi ili zichangie upatikanaji wa ajira, kuinua kipato na kulipa kodi hatimae kuchangia ukuaji wa uchumi maarifa" ameongeza.

DKT. AKWILAPO : NAIONA TANZANIA YA KESHO ILIYO BORA ZAIDI,  IKIIMARISHA UJUZI NA BUNIFU KWA VITENDO. Tanga. Hayo yamebai...
19/08/2026

DKT. AKWILAPO : NAIONA TANZANIA YA KESHO ILIYO BORA ZAIDI, IKIIMARISHA UJUZI NA BUNIFU KWA VITENDO.

Tanga.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo wakati wa ufunguzi rasmi wa Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, tarehe 18 Agosti 2026 , Viwanja vya Usagara - Jijini Tanga.

Dkt Akwilapo ameeleza kuwa anajisikia furaha kuwa sehemu ya maadhimisho ya Wiki hiyo na kuungana na timu ya Wizara hiyo kukuatana pamoja Tanga kujadili pamoja msingi wa kuendelea kumtoa mtoto maskini na kumaundaa kuwa kiongozi bora na mkubwa katika nchi.

" Tunawapongeza ndugu zetu kwa kutualika nasi kushiriki nanyi katika tukio hili la kitaifa na kwa Maeonesho haya yamefana sana na kuongezeka sana kwa washiriki. Wizara ya Ardhi ipo tayari kuendelea kushirikiana na wizara hiyo muda wowote itakapohotajika kufanya hivyo " alisisitiza Dkt Akwlilapo.

" Hongereni sana mimi nilikuwa wizara hii takribani miaka 4 iliyopita na nilivyoiacha sivyo hivyo ilivyo kwasasa na imekamilisha mageuzi ya mitaala mpya wa elimu kupitia na Sera ya Elimu na Mafunzo 2014, Toleo la 2023 iliyozinduliwa Rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan siku ya tarehe 2 Februari 2025 pale JKCC- Dodoma na sasa inatoa matunda kupitia Wiki hii " aliongeza Dkt. Akwilapo.

PROF. MKENDA :  TANGA YANG'AA KWA ELIMU, UJUZI NA UBUNIFU.  📍Tanga. WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Mhe. Prof. ...
19/08/2026

PROF. MKENDA : TANGA YANG'AA KWA ELIMU, UJUZI NA UBUNIFU.

📍Tanga.

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda (mb) amesema hayo wakati wa Maonesho ya Wiki ya Kitaifa inayoadhinishwa mjini Tanga, tarehe 18 Agosti 2026 - Jijini Tanga. Ameeleza mafanikio, ubunifu na mipango mipya ya Serikali inalenga kuunganisha elimu na ujuzi ili kuchochea maendeleo ya viwanda na uchumi wa kisasa kuelekea Dira 2050.

Aidha, Prof. Mkenda mageuzi ya Elimu ni historia na muktadha wa Wiki ya Elimu Kitaifa umefanyika kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo ikishirikiana na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi - NACTVET ili kukuza ujuzi ikiwa ni Utekelezaŕji wa Agizo la Serikali kupitia Waziri Mkuu lilioelekeza tukio hili lifanyike kwa ngazi ya kitaifa.

" Mwaka huu, Wiki hii inayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24, Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ikiwakutanisha wadau kutoka wizara mbalimbali, vyuo vikuu, vyuo vya ufundi, taasisi za utafiti na sekta binafsi. Huku Kilele cha maonesho kitaongozwa na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba — kiongozi aliyeteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri Mkuu tarehe 13 Novemba 2025, akichukua nafasi ya mtangulizi wake Mhe. Kassim Majaliwa, baada ya kuhudumu k**a Waziri wa Fedha tangu Machi 2021." Alisisitiza.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Bunifu na Teknolojia zinazooneshwa hapa zinavutia zaidi wanafunzi na watafiti wa vyuo mbalimbali k**a Tiba-asilia ya Chuo cha MUHAS kuonesha tafiti za afya shirikishi, ikiwemo matumizi za kukabiliana na tatizo la tezi dume. Vilevile, Chuo Kikuu cha Nelson Mandela - NM-AIST kimegundua teknolojia ya mabaki ya korosho kutengeneza dawa ya kutunza ngozi, jambo linalotarajiwa kuongeza kipato, ajira na fedha za kigeni. Pamoja na Elimu ya Ufundi kupitia Tanga Tech imekuwa kitovu cha kituo cha mafunzo ya ufundi wa vitendo kwa kuonesha maendeleo makubwa ya wanafunzi kupata umahiri wa kuzungumza Kiswahili na Kiingereza, jambo lililowavutia hata wawakilishi wa kidiplomasia kutoka China.

" Kwa ujumla, zaidi ya bunifu 70 zipo katika hatua mbalimbali za ubiasharishwaji ili kuchangia uchumi wa taifa, Serikali ikiwa imeanzisha mfuko maalum wa kuwasaidia wabunifu wachanga SAMIA INNOVATION COMMERCIALIZATION FUND ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuharakisha ukuaji wa biashara zao. Wizara imeendelea kuwekeza katika maendeleo ya Elimu kwa Mkoa wa Tanga na kufanikiwa kuanza ujenzi wa miundombinu ya Elimu ya Ufundi na VETA Kila Wilaya na Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa Wilaya ya Mkinga yote hayo ni kusimamia utekelezaji wa maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan " amesisitiza

Prof. Mkenda amesema Serikali kupitia Wizara ya Fedha iliyowakilishwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde na Wizara ya Fedha, inawezesha mageuzi makubwa ya sekta ya ufundi stadi na Wanafunzi kushiriki mashindano ya ujuzi (skills competition) na Wizara kwa mwaka huu itapeleka timu ya Tanzania jijini Shanghai, China, kushiriki mashindano ya kimataifa."

" Mageuzi yote hayo yatawezesha Mkoa wa Tanga kupata— tawi jipya la Chuo Kikuu cha Mzumbe hatua hiyo itakayowezesha Tanga kumiliki chuo kikuu chake yenyewe. Urithi wa Kihistoria wa mji huo unanikumbusha reli ya kwanza nchini Tanzania ilijengwa mwaka 1893 iliyojulikana k**a Usambara Line au Tanga Line, huku historia ikifungamana na maelekezo ya sasa ya Rais ya kuongeza tija na bunifu kwa wataalamu wa ndani na kujenga teknolojia wenyewe, badala ya kutegemea zaidi wataalamu wa nje.

Amesisitiza kuwa Ufadhili wa "Samia Scholarship" - STEM Sehemu kubwa umejikita kuwezesha wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita masomo ya sayansi na kufanikiwa kuwanufaisha wanafunzi 1,050 waliofanya vizuri zaid Mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2026, wanafunzi 50 bora zaidi watapelekwa kusomea fani za Akili Unde (AI), Data Science na teknolojia nyingine za kisasa, huku waliosalia kusomea vyuo vikuu vya ndani kwa ufadhili wa asilimia 100 kutoka Serikalini. Wanufaika hao hupitia kambi maalum ya maandalizi katika Chuo Kikuu cha NM-AIST jijini Arusha kabla ya kuanza masomo yao ya elimu ya juu"

Vilevile, amerejea kuwa,Mhe. Rais amewahi kuahidi bungeni kupeleka wanafunzi kusoma nje ya nchi — akiwa tayari amepeleka baadhi Afrika Kusini na Moscow, huku juhudi zikiendelea za kupeleka wengine China. Uzalishaji wa Ndani na Uhandisi Rejeshi " Reverse Engeeeing " utapunguza utegemezi wa bidhaa za nje: wahandisi wa ndani wameanza kutengeneza vipuli vya bajaji na baadhi ya vipuli vikubwa vya magari ya FUSO ndani ya nchi, jitihada zinazoimarisha kujifunza kutengeneza bidhaa kwa kuchambua zilizopo, badala ya kuagiza kila kitu kutoka nje.

" Tuzo za Watafiti waliochapisha matokeo-tafiti katika majarida ya kimataifa yenye hadhi walitunukiwa tuzo kuanzia mwaka 2022 na kutolewa rasmi mwaka 2024; ili kuhakikisha watafiti wanaofikia vigezo hupokea kiasi cha shilingi milioni 50 ili kuchochea utafiti na uchumi wa taifa kupitia mpango wa Serikali wa kuimarisha elimu, ujuzi na ubunifu — k**a msingi wa kukuza uchumi wa maarifa, viwanda na unaotegemea na kugatua fursa za elimu ya juu na ufundi na kujenga rasilimali watu inayokidhi mahitaji ya nchi na kitaaluma kwenye sekta za kimkakati k**a AI na Data Science, na matunda yake yataendelea kuonekana zaidi miaka ijayo"

DKT. MUNISI : VIJANA JIFUNZENI KWA VITENDO , BIDII NA MAADILI MEMA ILI KUFIKIA DIRA2050 📍Tanga Rai hiyo imetolewa na Nai...
19/08/2026

DKT. MUNISI : VIJANA JIFUNZENI KWA VITENDO , BIDII NA MAADILI MEMA ILI KUFIKIA DIRA2050

📍Tanga

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, anaeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano , Mhe. Dkt. Eveline Munisi (mb) wakati Akihutubia katika Ufunguzi wa Wiki ya Kitaifa : Elimu, Ujuzi na Ubunifu, Tarehe 18 Agosti 2026 , Viwanja vya Usagara - Jijini Tanga.

Dkt. Munisi ameeleza kuwa Mkoa wa Tanga ni lango kuu la kiuchumi linalounganisha Tanzania na Masoko ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), huku akipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuandaa Wiki hiyo , warsha na Makongamano kwa lengo la kuendeleza ujuzi na maarifa ili kuwezesha ushindani wa soko la ndani na kimataifa.

Aidha, Mhe. Dkt. Munisi ametumia fursa hiyo kumpongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda (mb) pamoja na Taasisi zilizopo chini yake ikiwemo Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kuendeleza sekta hiyo ya elimu ikiwemo kukuza ujuzi na elimu kwa vitendo jambo linachochea ukuaji wa. Matumizi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu.

" Serikali inaunga mkono jitihada hizo za Sekta ya Elimu ya uandaaji wa nguvukazi kwaajili ya kufikia maono ya Dira 2050. Pia, Serikali inatoa ufadhili wa Asilimia 100% wa masomo, bima ya afya na kuchangia nauli kwa vijana kujiendeleza kielimu na kufanya mafunzo kwa vitendo" alisisitiza Mhe. Munisi.

Amehitimisha kwa kuendelea kutoa rai kwa vijana kuendelea kujifunza kwa vitendo, bidii na maadili mema ili kufanikisha maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na hatimae kulifikisha Taifa katika Uchumi wa Juu wa Kati na kufikia Dolla Trillioni moja (1) ifakapo 2050.

MAKBEL: MABADILIKO YA MITAALA YA AMALI KUZALISHA MABILIONEA WADOGO WA KESHO.📍TangaRai hiyo imetolewa na Mbunge wa Tanga,...
19/08/2026

MAKBEL: MABADILIKO YA MITAALA YA AMALI KUZALISHA MABILIONEA WADOGO WA KESHO.

📍Tanga

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Tanga, Mhe. Kassim Mbaraka Makbel (mb) kwa Taasisi za Umma na Sekta binafsi kuendeleza ushirikiano wa karibu na Sekta ya Elimu na wananchi kwa ujumla ili kuhakikisha wabunifu wachanga hawaishii kwenye maonesho pekee, bali wanakuwa nguzo ya utatuzi wa changamoto na kusaidia jamii inayowazunguka. Ameyasema hayo wakati akiwasilisha salamu za Ukaribisho Mkoa wa Tanga, Ufunguzi wa Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, Tarehe 18 Agosti 2026 - Viwanja vya Usagara- Tanga.

Mhe. Makbel amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya elimu nchini, mitaala kuelekea mafunzo ya amali (vitendo) ili kuzalisha mabilionea wengi wenye umri mdogo ifakapo mwaka 2050. Pia ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia chini ya uongozi wa Waziri Prof. Adolf Mkenda (mb) na timu yake kutafsiri kwa vitendo maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kubadilisha masomo kutoka ya nadharia pekee kuelekea ujuzi na vitendo ili kuleta matokeo chanya kwenye jamii ya watanzania kupitia utekelezaji wa mfumo mpya unaomwezesha mwanafunzi kupata Cheti cha Elimu ya Jumla na Cheti cha Ujuzi wa vitendo - Amali ili kusaidia kuongeza ajira, kulipa kodi na kukuza uchumi wa kidijitali

" Kufufuliwa kwa viwanda vya ndani kunainua Uchumi wa Tanga na kukumbusha historia ya maono ya Tanga iliyosheheni Viwanda, na kubadilisha utamaduni na msemo wa zamani wa "Waja leo kuondoka majaliwa" bali chini ya usimamizi wa Dkt. Samia na utekelezaji wa maelekezo ya kurejesha na kufufua viwanda ndani, sekta ya Elimu sasa imeimarisha upatikanaji wa elimu ya vitendo ujuzi, na kuunganisha fursa za mafunzo kwa vitendo kwa Mkoa wa Tanga" alisisitiza.

"Kiwanda cha Sabuni cha Foma na Kiwanda cha Chuma vimefufuka na sasa vinazalisha. Tanga imeinuka kiuchumi, na sasa inasimama k**a lango kuu la uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki na Jumuia ya SADC kupitia Bandari yetu," amesisitiza Mhe. Makuberi.

Adha, Mhe. Makbel amekumbusha kuwa Serikali kupitia Waziri Mkuu mwaka 2022 ilielekeza Maonesho ya MAKISATU kufanyika Kitaifa yanaliyokuwa yakiratibiwa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilichukua hatua na kuridhia ombi lake, ilikubali maonesho hayo ya Wiki ya Elimu kufanyikia mkoani Tanga na viongozi hao wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa Maonesho hayo kufanyika kwa mafanikio makubwa kwa miaka mitatu mfululizo jijini Tanga.

Vilevile, Mhe. Makbel ameeleza kuwa kutokana n mwamko mkubwa wa wananchi wa Mkoa wa Tanga, amewasilisha ombi maalum kwa Wizara ya Elimu kutoacha kuyaleta maonesho hayo mkoani humo ili majirani zake waendelee kunufaika na utekelezaji wa mitaala mipya na kukuza ujuzi wa vitendo kwa vijana wa Kitanzania kupitia utekelezaji wa muongozo wa unaunganisha viwanda, Vyuo na Sekta binafsi kuchangia kukuza uchumi-maarifa nchini.

Amesema ubunifu haupaswi kutazamwa kwa kifaa cha mfano pekee 'Prototype' bali ni fursa ubiasharishwaji wa bidhaa za kibunifu za ndani zinazochochea ukuzaji wa matumzii ya bidhaa zitokanazo na uchumi-maarifa ili kuwezesha mabadiliko makubwa na kutanua wigo wa matimizi ya bidhaa za ndani na kutekeleza mwa vitendo maono ya Mhe. Rais kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Inaratibu Mfuko Maalum wa Samia Innovation Commercialization Fund - SICF uliopewa kiasi cha TZS bIllioni 4.6 mwaka 2024 ili kuendeleza wabunifu wachanga na kupunguza utegemezi kwa vijana kujiajiri na kuajiri wenzao kwa lengo la kuzalisha mabilionea wadogo ifakapo mwaka 2050.

DKT. BATILDA : WIKI YA ELIMU YAING'ARISHA TANGA, LANGO LA UCHUMI AFRIKA MASHARIKITanga. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mk...
19/08/2026

DKT. BATILDA : WIKI YA ELIMU YAING'ARISHA TANGA, LANGO LA UCHUMI AFRIKA MASHARIKI

Tanga.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dkt. Batilda Buriani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, iliyobeba Kauli mbiu " Elimu , Ujuzi na Ubunifu, njia ya kufikia Dira 2050" , Tarehe 18 Agosti 2026 - Uwanja wa Usagara - Jijini Tanga.

Amesema kuwa Uwekezaji unaofanywa na Serikali kwa Sekta ya Elimu - Tanga ni utekelezaji wa maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuboresho mitaala, Ujenzi wa miundombinu ya elimu na utekelezaji wavsera ya elimu ni nyenzo ya kuimarisha ujuzi, sayansi, teknolojia na bunifu kutumia rasilimali adhimu za Mkoa huo ili kutumia uchumi-maarifa kwa lengo la kuongeza tija ya uzalishaji wa viwanda vya ndani, biashara, kilimo, utalii na uwekezaji mkao wa Tanga.

" Tunajenga refinery na viwanda, hivyo tunahitaji kuwaandaa zaidi vijana wetu ili wawe tayari kutumia fursa hizi, Tanga imekuwa Kitovu cha viwanda, madini na uwekezaji wa kiuchumi hivyo kuimarisha utaoji huduma kwa sekta za viwanda, ujenzi, madini, nishati, biashara na gesi miongoni mwa maeneo yenye fursa kubwa " alisisitiza

Dkt. Batilda amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa uwekezaji huo mkubwa na kuendelea kuchagua kuadhimisha Wiki hiyo mkoani humo kwa mara ya tatu mfululizo, na kutambua mchango wa viongozi wa dini kudumisha amani, mshik**ano na utulivu nchini Tanzania.

Aidha, Uwekezaji wa Elimu umeanza kuonekana kupitia ujenzi wa shule, madarasa, mabweni kutoka shule 46 mpaka shule 94 na ongezeko la ufaulu kutoka Asilimia 84% mpaka kufikia Asilimia 90% vikienda sambamba na ongezeko la ajira za walimu na upanuzi wa upatikanaji wa huduma ya elimu ya amali na ufundi Jijini Tanga. Ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo, Elimu bila ada, kuimarika kwa ongezeko la fedha hivyo kusaidia Serikali kukabiliana na changamoto za miundombinu na mazingira ya kujifunzia.

" Kwa Mwaka wa Fedha wa 2026/27, Mkoa wa Tanga imekuwa mwenyeji wa Ujenzi wa Chuo Kikuu Mzumbe ikiwa ni fursa ya uwekezaji wa elimu ya juu, tafiti, ubunifu na uzalishaji wa wataalamu ili kuongeza mwingiliano kati ya vyuo, viwanda, sekta binafsi na jamii, na kutumika kwa uchumi maarifa kutatua changamoto za jamii na kuzalisha ajira." Amelisema.

Aidha, amebainisha kuwa Mkoa huo umekuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa kwa kutumia rasilimali za ndani k**a vile madini ya graphite, saruji (cement), vifaa vya ujenzi na gesi zinazoongeza thamani ya mkoa, mazingira ya vijana kujifunza elimu ya vitendo, badala ya kubaki watazamaji wa maendeleo pekee bali kuchangia matumzi ya uchumi maarifa.

Dkt. Burian alisema kufanyika kwa Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu mkoani Tanga kumetoa faraja na umuhimu wa kipekee kuonesha mafanikio, kubaini changamoto na kujadili namna bora amali inavyoweza kutatua changamoto za jamii na kuchochea ujenzi wa uchumi maarifa sayansi, teknolojia na ubunifu. Pia, Utalii na uchumi wa buluu nao wachangia fursa za ukuzaji na mazingira ya ujifunzi wa vitendo kupitia viwanda vya Tanga vilivyo na utajiri mkubwa wa vivutio vya utalii k**a Mapango ya Amboni na Magoroto vinavyochangia uchumi wa mkoa na Taifa.

Address

Bagamoyo Road
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Telephone

+255222771358

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when COSTECH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share