Tanzania Forest Services Agency

Tanzania Forest Services Agency We conserve and sustainably supply quality forest and bee products and services in Tanzania.

TFS has been given the mandate for the management of national forest reserves (natural and plantations), bee reserves and forest and bee resources on general lands. TFS as an Executive Agency will enhance the management and conservation of forest and bee resources for sustainable supply of quality forest and bee products and services. The Forest and Beekeeping Division will remain with the respons

ibilities of development of the forest policy, laws and regulations and overseeing their implementation in the sector. Tanzania Forest Service takes over some of the core functions of the Forestry and Beekeeping Division which are;

Establishing and managing central government natural forest and bee reserves;
Establishing and managing central government forest plantations and apiaries;
Managing forest and bee resources in general land;
Enforcing Forest and Beekeeping legislation in areas of TFS jurisdiction;
Providing forest and beekeeping extension services in areas of TFS jurisdiction;
Developing TFS Human resources;
Collecting Forestry and Beekeeping revenue;
Safeguarding TFS Assets;
Marketing forest and bee products and services. The TFS has been established to achieve the following objectives:

Improve the quality and value for money of the delivery of public services;
Ensure efficient and effective management of forest and bee resources; and
Promote the potential for the continuous improvement of its services

Vision

The vision of TFS is “A center of excellence in the conservation of forest and bee resources and sustainable supply of quality forest and bee products and services in Tanzania.”

Mission

The Mission of TFS is “To sustainably manage the National forest and bee resources in order to contribute to the social, economic, ecological, cultural and needs of present and future generations”. Objectives

The TFS will work on the following five objectives;

HIV/AIDS infections reduced and supportive services to people living with HIV/AIDS improved;
Sustainable supply of quality forest and bee products enhanced;
Stable ecosystem and biological diversity maintained;
Institutional capacity to deliver services strengthened and;
Gender balance and good governance enhanced. Strategies;

To achieve the stated objectives, the following strategies must be implemented:

Improve the existing HIV/AIDS preventive services;
Establish care and supportive services for identified TFS staff living with HIV/AIDS;
To develop and operationalize the HIV/AIDS Strategy ;
Build capacity on preparation of forest and bee resource management plans and quality control;
Improve forest and bee resources information and management planning;
Expand forest plantations and gazette new forest and bee reserves;
Enhance stakeholders’ participation in forest and bee resources development and management in identified areas;
Diversify forest and bee products and services;
Enforce and monitor quality assurance of forest and bee products;
Strengthen forest protection and management;
Maintain adequate information on ecosystem;
Adopt mitigation measures on addressing climate change;
Rehabilitate degraded areas and poorly stocked forest reserves;
Establish and operationalize sustainable financing mechanism for TFS;
Strengthen human resources capacity;
Develop and improve working facilities and infrastructure;
Develop and implement effective Monitoring & Evaluation system;
Improve staff remuneration and develop incentive scheme;
Mainstream gender in TFS programme;
Strengthen and enforce compliance to laws, rules, regulation on forest and bee resource management; and
Improve customer care service delivery.

TFS YAONESHA FURSA ZA MABILIONI KWENYE MISITU, NYUKI NANENANENa Mwandishi Wetu, DodomaDODOMA — Wakala wa Huduma za Misit...
03/08/2026

TFS YAONESHA FURSA ZA MABILIONI KWENYE MISITU, NYUKI NANENANE

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

DODOMA — Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeonesha namna sekta ya misitu na nyuki inavyoweza kuwa chanzo kikubwa cha ajira, kipato na ukuaji wa uchumi kupitia mnyororo wa thamani wa mazao yake.

Hayo yamebainika katika Maonesho ya Nane Nane 2026 yanayoendelea Dodoma, baada ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi, kutembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii na kujionea ubunifu unaofanywa na TFS katika kuibua fursa hizo.

Brigedia Jenerali Lupi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Nane Nane Kitaifa upande wa JKT, alielezwa kuhusu safari ya mazao ya misitu na nyuki kutoka uzalishaji, uchakataji, uongezaji thamani hadi kufikia masoko ya ndani na nje.

Amesema ubunifu huo unaonesha kuwa rasilimali za misitu zinaweza kutumika zaidi ya uhifadhi, bali pia kuwa kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.

“Nimeona mnyororo mzima wa thamani unaoonesha namna mazao ya misitu na nyuki yanavyoweza kuongeza ajira, kipato na kuchangia uhifadhi wa mazingira,” amesema.

Katika banda hilo, Brigedia Jenerali Lupi pia alishuhudia huduma ya tiba nyuki (Apitherapy), inayotumia bidhaa za nyuki pamoja na kudungishwa na nyuki chini ya uangalizi wa wataalamu.

Alielezwa kuwa tiba hiyo imekuwa ikitumika kusaidia kupunguza baadhi ya maumivu ya viungo na changamoto nyingine zinazohusishwa na afya, huku wataalamu wakisisitiza matumizi sahihi na salama ya huduma hiyo.

03/08/2026

TFS YAPONGEZWA KUBORESHA BARABARA PUGU KAZIMZUMBWI, YAFUNGUA NJIA UTALII WA MICHEZO

Na Mwandishi Wetu, Kisarawe

KISARAWE — Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mheshimiwa Petro Magoti, amepongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kuboresha barabara inayopita katika Hifadhi ya Mazingira Asilia Pugu Kazimzumbwi, akisema hatua hiyo imeongeza usalama na kufungua fursa za kukuza utalii wa michezo na shughuli za kiuchumi wilayani humo.

Akizungumza mapema hivi leo, Mh. Magoti amesema uboreshaji wa miundombinu hiyo umewezesha kufanyika kwa mashindano ya mbio za magari katika mazingira salama, huku ukiimarisha nafasi ya Kisarawe kuwa miongoni mwa maeneo yanayoweza kuandaa matukio makubwa ya michezo nchini.

Amesema mafanikio ya mashindano hayo yameongeza ushawishi wa kuandaa mashindano mengine makubwa, ikiwemo mbio za kitaifa za pikipiki, ambazo zinaweza kuongeza idadi ya wageni na kuchochea shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa wilaya hiyo.

“Ushirikiano huu unaonesha namna uhifadhi unaweza kwenda sambamba na maendeleo ya jamii. Kuboresha miundombinu katika maeneo ya hifadhi kunatoa fursa kwa wananchi kunufaika kupitia utalii na shughuli nyingine za kiuchumi,” amesema Mh. Magoti.

Kwa upande wa TFS, Kaimu Mhifadhi wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Pugu Kazimzumbwi, Mbaruku Sinon, amesema mafanikio ya mashindano hayo yameonesha uwezo wa maeneo yanayosimamiwa na wakala huo kuwa kitovu cha matukio mbalimbali ya michezo na utalii.

Sinon amewahimiza wadau wa michezo na utalii kuendelea kutumia maeneo ya TFS kuandaa matukio mbalimbali k**a marathon, mbio za pikipiki na baiskeli, akisema hatua hiyo itasaidia kuhamasisha utalii, kukuza uchumi na kuimarisha uelewa wa umuhimu wa uhifadhi wa mazingira.

“Maeneo haya yana thamani kubwa siyo tu kwa uhifadhi wa misitu na viumbe hai, bali pia yanaweza kutumika k**a majukwaa ya kukuza michezo na kuleta manufaa kwa jamii,” amesema.

Naye Mkurugenzi wa Mashindano, Ifan Aladin amesema ushirikiano wa TFS katika kuboresha barabara hiyo umeongeza ubora wa mashindano na kuvutia washiriki kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Amesema maandalizi bora ya miundombinu yamekuwa chachu ya mafanikio ya mashindano hayo na kuahidi kuendelea kushirikiana na TFS katika kuandaa matukio makubwa zaidi yatakayochangia maendeleo ya wilaya hiyo na sekta ya utalii.

Mmoja wa madereva walioshiriki mashindano hayo ameishukuru TFS kwa kuboresha barabara hiyo, akisema hatua hiyo imeongeza usalama kwa washiriki, kuboresha ubora wa mashindano na kuwapa hamasa madereva wengi zaidi kushiriki katika matukio yanayofanyika Kisarawe.

Mashindano hayo ni sehemu ya jitihada za kuunganisha uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya maeneo ya asili kwa ajili ya kukuza utalii na maendeleo ya kiuchumi.

TEKNOLOJIA YAIBUA VIVUTIO VYA ASILI, TFS YAWAKARIBISHA WATANZANIA UTALII WA KIDIJITALINa Mwandishi Wetu, DodomaDODOMA — ...
03/08/2026

TEKNOLOJIA YAIBUA VIVUTIO VYA ASILI, TFS YAWAKARIBISHA WATANZANIA UTALII WA KIDIJITALI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

DODOMA — Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umetumia teknolojia ya kisasa kuwapa wananchi fursa ya kutembelea na kufahamu vivutio vya utalii wa mazingira asilia kwa njia ya kidijitali kabla ya kuvifikia moja kwa moja.

Akizungumza katika Maonesho ya Nane Nane 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma, Meneja wa Kituo cha TFS cha Michoro ya Kondoa Irangi, Zuberi Mabie, amesema teknolojia hiyo imekuwa nyenzo muhimu katika kutangaza vivutio vya asili vinavyosimamiwa na TFS na kuhamasisha utalii wa ndani.

Amesema kupitia huduma ya virtual tour, wananchi wanaweza kupata taswira halisi ya maeneo mbalimbali ya utalii ikiwemo misitu ya asili, mapango, maporomoko ya maji, maeneo ya ikolojia ya kipekee na michoro ya miambani kabla ya kupanga safari ya kuyatembelea.

“Teknolojia hii inasaidia kuwafikisha watu karibu na vivutio ambavyo huenda hawajawahi kuvifahamu. Wananchi wanaweza kuona uzuri wa maeneo haya kidijitali na kupata taarifa sahihi za namna ya kuyafikia,” amesema Mabie.

Amesema Kituo cha Michoro ya Kondoa Irangi kinaendelea kutumia mbinu za kisasa katika kutangaza urithi wa asili, ikiwemo kuwafahamisha wananchi kuhusu thamani ya michoro hiyo ya kihistoria na umuhimu wa kuihifadhi kwa vizazi vijavyo.

Mabie amewataka wananchi kutumia fursa ya Maonesho ya Nane Nane kutembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupata elimu kuhusu vivutio mbalimbali vinavyosimamiwa na TFS pamoja na kupanga safari za utalii wa ndani.

Ameongeza kuwa tarehe 9 Agosti 2026 kutakuwa na safari maalumu ya utalii wa ndani kuelekea eneo la Michoro ya Miambani Kolo, Kondoa, kwa ajili ya wananchi kupata uzoefu wa moja kwa moja wa urithi huo wa asili.

Amesema utalii wa ndani una mchango mkubwa katika kukuza uchumi, kuongeza uelewa wa uhifadhi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika kulinda rasilimali za mazingira.

“Tunawahimiza Watanzania kujifunza na kutembelea vivutio vilivyopo nchini. Kila safari ya utalii ni sehemu ya kuunga mkono uhifadhi na maendeleo endelevu,” amesema Mabie.

RC MALIMA: TUSHIRIKIANE KUREJESHA UOTO WA ASILINa Mwandishi Wetu, MorogoroMOROGORO — Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mheshimiw...
03/08/2026

RC MALIMA: TUSHIRIKIANE KUREJESHA UOTO WA ASILI

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

MOROGORO — Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima, ameitaka TFS, Halmashauri na wadau wa mazingira kuimarisha ushirikiano katika kurejesha uoto wa asili na kulinda vyanzo vya maji.

Mhe. Malima ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika Maonesho ya Nane Nane 2026 Kanda ya Mashariki yanayofanyika mkoani Morogoro.

Amesema elimu kwa wananchi kuhusu uhifadhi wa mazingira inapaswa kuendelea kutolewa ili kupunguza vitendo vya ukataji holela wa miti na uharibifu wa mazingira.

“Ni muhimu wananchi wahamasishwe kupanda miti kwa wingi, ikiwemo miti ya matunda na mazao ya viungo k**a karafuu, ambayo yataongeza kipato huku yakisaidia kulinda mazingira,” amesema.

Amesisitiza kuwa ushirikiano wa taasisi za serikali na wadau wa mazingira ni nguzo muhimu katika kuhakikisha rasilimali za misitu zinahifadhiwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake, Kamanda wa TFS Kanda ya Mashariki, SACC Matthew Ntilicha, amesema wakala huo unaendelea na majukumu ya kulinda misitu ya hifadhi, kudhibiti uvunaji haramu wa mazao ya misitu, kuhamasisha upandaji miti na kurejesha maeneo yaliyoharibiwa.

Amesema TFS itaendelea kushirikiana na Halmashauri na wadau mbalimbali kuhakikisha juhudi za kurejesha uoto wa asili na matumizi endelevu ya rasilimali za misitu zinaimarishwa.

*TFS YAONESHA TEKNOLOJIA ZA UHIFADHI NANE NANE KANDA YA MAGHARIBI*Na Mwandishi Wetu, TaboraWakala wa Huduma za Misitu Ta...
03/08/2026

*TFS YAONESHA TEKNOLOJIA ZA UHIFADHI NANE NANE KANDA YA MAGHARIBI*

Na Mwandishi Wetu, Tabora

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unashiriki Maonesho ya Wakulima (Nanenane) Kanda ya Magharibi yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane Ipuli, Manispaa ya Tabora, ukiendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uhifadhi wa misitu na nyuki pamoja na kuonesha teknolojia mbalimbali zinazochangia maendeleo ya sekta ya misitu.

Maonesho hayo yalizinduliwa rasmi Agosti 1, 2026 chini ya kaulimbiu isemayo, “Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa 2050,” yakilenga kuhamasisha matumizi ya teknolojia na ubunifu katika kuongeza uzalishaji na kuchochea maendeleo ya uchumi.

Akizindua maonesho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Simon Sirro, aliwataka wadau wa sekta za kilimo, misitu, mifugo na taasisi mbalimbali za Serikali na sekta binafsi kuongeza ubunifu na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza tija katika uzalishaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema matumizi ya teknolojia ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku akisisitiza kuwa taasisi zinapaswa kuendelea kubuni na kusambaza teknolojia zinazowagusa wananchi moja kwa moja na kuchochea maendeleo endelevu.

Kwa upande wake, Kaimu Kamanda wa TFS Kanda ya Magharibi, PCO Ali Maggid, alisema ushiriki wa TFS katika maonesho hayo unalenga kuwafikia wananchi kwa elimu kuhusu uhifadhi wa misitu na nyuki, matumizi endelevu ya rasilimali za misitu pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana katika sekta hiyo.

Alisema banda la TFS linaonesha huduma na teknolojia mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa mbegu na miche bora ya miti, ufugaji nyuki, uhifadhi wa misitu na elimu kuhusu upandaji wa miti kwa ajili ya kurejesha uoto wa asili, kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuongeza kipato cha wananchi.

Aliwataka wananchi kutumia fursa ya Maonesho ya Nanenane kutembelea banda la TFS ili kujifunza teknolojia mbalimbali za uhifadhi, kupata ushauri wa kitaalamu na kufahamu huduma zinazotolewa na wakala huo ambazo zinachangia maendeleo ya sekta ya misitu na ustawi wa jamii.

Maonesho ya Nanenane yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wadau wa sekta za kilimo, misitu, mifugo na uvuvi, huku yakitoa fursa kwa wananchi kujifunza teknolojia bunifu, kubadilishana uzoefu na kupata elimu itakayowawezesha kuongeza uzalishaji na kushiriki katika uhifadhi wa mazingira kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

MLELE YAENDELEA KUTOA ELIMU YA UHIFADHI WA MISITU NA WANYAMAPORINa Mwandishi Wetu, KataviOfisi ya Mhifadhi wa Misitu Wil...
03/08/2026

MLELE YAENDELEA KUTOA ELIMU YA UHIFADHI WA MISITU NA WANYAMAPORI

Na Mwandishi Wetu, Katavi

Ofisi ya Mhifadhi wa Misitu Wilaya ya Mlele kwa kushirikiana na Kamati ya Usalama ya Wilaya, Ofisi ya Pori la Akiba Nyonga na Mbunge wa Jimbo la Katavi, Thomas Kampala Maganga, imeendelea kuimarisha kampeni ya utoaji elimu kuhusu uhifadhi wa rasilimali za misitu na wanyamapori kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Ziara hiyo ya uelimishaji iliyofanyika leo, Agosti 3, 2026, imelenga kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi misitu na wanyamapori kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, ikiwa ni sehemu ya mpango endelevu wa kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii kwa elimu ya uhifadhi.

Makundi yaliyofikiwa ni pamoja na viongozi wa kisiasa, wadau wa uhifadhi, viongozi wa serikali za vijiji na wananchi, ambapo walihamasishwa kushiriki kikamilifu katika kulinda rasilimali za asili na kuzuia vitendo vinavyohatarisha bioanuwai.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mbunge wa Jimbo la Katavi, Thomas Kampala Maganga, alisema shughuli za uhifadhi wa misitu, nyuki na wanyamapori zina mchango mkubwa katika kulinda mazingira, kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha ustawi wa jamii kupitia maendeleo endelevu.

Alisema uhifadhi wa rasilimali za asili ni jukumu la kila mwananchi, akisisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi za uhifadhi na wananchi ni msingi wa kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Mbunge huyo pia aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Wilaya ya Mlele, wahifadhi na wadau wengine kuendeleza kampeni za utoaji elimu ya uhifadhi kwa makundi mbalimbali ya kijamii ili kuongeza ushiriki wa wananchi katika kulinda misitu na wanyamapori.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake za uhifadhi za kuhakikisha jamii inakuwa mshirika mkuu katika usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu na wanyamapori kwa maendeleo ya Taifa.

WAZIRI KIJAJI AIPONGEZA TFS, AAGIZA KUONGEZA UZALISHAJI WA MITI YA MALISHO KUPUNGUZA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJINa ...
03/08/2026

WAZIRI KIJAJI AIPONGEZA TFS, AAGIZA KUONGEZA UZALISHAJI WA MITI YA MALISHO KUPUNGUZA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji, ameipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kazi kubwa ya kusimamia na kuhifadhi rasilimali za misitu na nyuki pamoja na kuhamasisha wananchi kushiriki katika upandaji wa miti nchini.

Akitembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma leo Agosti 3, 2026, Waziri alipokea maelezo kuhusu shughuli za TFS, ikiwemo uzalishaji wa mbegu na miche bora ya miti kupitia vituo vya Morogoro, Lushoto na Iringa, ambavyo vinaendelea kuhudumia mahitaji ya wananchi na wadau mbalimbali.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Dkt. Kijaji alisema juhudi za TFS zimechangia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kuhifadhi misitu na mazingira. Hata hivyo, aliuagiza wakala huo kuongeza uzalishaji wa miche na mbegu za miti ya malisho ili kuwafikia wakulima wengi zaidi na kuwawezesha kuipanda katika mipaka ya mashamba yao, hatua itakayosaidia kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Aidha, aliwataka watumishi wa TFS kuendelea kuhamasisha wananchi kupanda miti kwa wingi pamoja na kuanzisha mashamba ya nyasi na miti ya malisho, akieleza kuwa hatua hiyo itaongeza upatikanaji wa malisho ya mifugo, kuimarisha uzalishaji na matumizi bora ya ardhi.

Alisema upandaji wa miti una mchango mkubwa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kuhifadhi vyanzo vya maji, kuzuia mmomonyoko wa ardhi na kuboresha mazingira, huku upatikanaji wa malisho ya kutosha ukiimarisha sekta ya mifugo na kudumisha amani katika jamii.

“Ninawahamasisha wananchi kutumia fursa ya Maonesho ya Nanenane kujifunza teknolojia na mbinu bora zinazotolewa na TFS kuhusu uzalishaji wa miche bora ya miti, upandaji wake pamoja na uanzishaji wa mashamba ya nyasi na miti ya malisho,” alisema Dkt. Kijaji.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa TFS, Frida Kundy, alisema TFS itaendelea kutekeleza maelekezo ya Waziri kwa kuongeza uzalishaji wa miche ya miti na miti ya malisho kupitia vituo vyake vya Morogoro, Lushoto na Iringa, sambamba na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uhifadhi wa misitu, upandaji wa miti na matumizi endelevu ya rasilimali za misitu.

Alisema ushiriki wa TFS katika Maonesho ya Nanenane unaendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwaelimisha wananchi kuhusu huduma na fursa mbalimbali zinazotolewa na wakala huo, ikiwemo uzalishaji wa miche bora ya miti, mbegu za miti, uhifadhi wa misitu, ufugaji nyuki na teknolojia za kilimo cha nyasi na miti ya malisho kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

DODOMA: VIONGOZI WIZARA ZA KILIMO NA MIFUGO WATEMBELEA BANDA LA TFS, WAPONGEZA HUDUMA NA UHIFADHINa Mwandishi Wetu, Dodo...
03/08/2026

DODOMA: VIONGOZI WIZARA ZA KILIMO NA MIFUGO WATEMBELEA BANDA LA TFS, WAPONGEZA HUDUMA NA UHIFADHI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

DODOMA — Viongozi kutoka Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Mifugo wametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, wakipongeza juhudi za Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika uhifadhi wa misitu, upandaji miti na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akiwa katika banda hilo jana Agosti 2,2026, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Agness Meena, alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazoratibiwa na TFS, ikiwemo fursa za sekta ya misitu, ufugaji wa nyuki na vivutio vya utalii wa ikolojia vinavyosimamiwa na wakala huo.

Meena aliwataka wataalamu wanaohudumu katika banda hilo kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu bidhaa zitokanazo na mazao ya misitu, upatikanaji wa mbegu bora za miti na miche, pamoja na fursa zinazopatikana katika ufugaji wa nyuki kuanzia maandalizi ya mizinga, uvunaji, uchakataji wa mazao ya nyuki na matumizi ya bidhaa zake.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuhamasisha wananchi kutembelea vivutio vya utalii wa ikolojia vinavyosimamiwa na TFS, akieleza kuwa vina mchango mkubwa katika kukuza utalii na uchumi wa nchi.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo alipotembelea banda hilo alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Wizara ya Maliasili na Utalii ili kuongeza tija katika matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

Aidha, aliipongeza TFS kwa kazi kubwa ya upandaji miti na juhudi zake katika kuhifadhi misitu na rasilimali nyingine za asili.

Maonesho ya Nanenane yanaendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, ambapo Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii linaendelea kutoa elimu na kuonesha fursa mbalimbali za uwekezaji, uhifadhi na utalii kwa wananchi na wadau mbalimbali.

Maafisa 21 wa TFS wahitimu mafunzo ya kijeshi, watakiwa kuimarisha uzalendo na nidhamuKatavi. Wakala wa Huduma za Misitu...
01/08/2026

Maafisa 21 wa TFS wahitimu mafunzo ya kijeshi, watakiwa kuimarisha uzalendo na nidhamu

Katavi. Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewataka maafisa wake waliokamilisha mafunzo ya mfumo wa kijeshi (Paramilitary Transformation Course) kuyatumia maarifa, uzalendo, nidhamu na uadilifu walioupata katika kuimarisha usimamizi wa rasilimali za misitu na kutekeleza majukumu yao kwa weledi.

Wito huo umetolewa jana Julai 31, 2026 na Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Huduma Saidizi, DCC Emmanuel Wilfred Kiboko, wakati akifunga rasmi mafunzo ya Paramilitary Transformation Course Awamu ya 12 yaliyofanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Jeshi la Uhifadhi Mlele, mkoani Katavi, kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo.

DCC Kiboko aliwapongeza washiriki kwa kuonesha nidhamu na kujituma katika kipindi chote cha mafunzo huku akiwataka kuendeleza misingi hiyo wanaporejea katika vituo vyao vya kazi.

"Mafunzo haya yatawajengea uwezo, yatawajengea uzalendo na yatawajengea uadilifu mtakapokwenda kutekeleza majukumu yenu katika maeneo yenu ya kazi," alisema Kiboko kabla ya kutangaza rasmi kufungwa kwa mafunzo hayo.

Awali, Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Mhasibu Mkuu wa TFS, Peter Mwakosya, aliwapongeza wakufunzi wakiongozwa na Mkuu wa Kituo cha Mafunzo ya Kijeshi Mlele, SCO Samuel Msuva, kwa ubunifu na kiwango cha juu cha mafunzo waliokitoa, akisema yameendelea kuboreshwa kila mwaka.

Aliwataka wahitimu kuendeleza nidhamu waliyoijenga kambini akisisitiza kuwa msingi mkuu wa mfumo wa kijeshi ni utii na kwamba mafunzo hayo yataisaidia TFS kujenga taasisi yenye viongozi wenye uwezo mkubwa wa kusimamia rasilimali za taifa.

"Msingi mkuu wa mfumo wa kijeshi ni utii. Tunaamini utii huu pamoja na ukak**avu mliojengewa hapa mtauendeleza mnaporejea kwenye maeneo yenu ya kazi ili kuendelea kuijenga TFS imara," alisema Mwakosya.

Akitoa taarifa ya mafunzo, Mkuu wa Kituo cha Mafunzo ya Kijeshi Mlele, Mhifadhi Mwandamizi Samuel Msuva, alisema jumla ya maafisa 21 walihitimu mafunzo hayo, wakiwemo makamishna wanne na maafisa 17, ambapo wanawake walikuwa 12 na wanaume tisa.

Alisema washiriki walipatiwa mafunzo ya nadharia na vitendo yaliyohusisha uongozi, parade, mazoezi ya viungo, afya, matumizi ya silaha ndogo, mafunzo ya kurusha risasi pamoja na sheria na nyaraka zinazoongoza utendaji wa Jeshi la Uhifadhi.

Kwa mujibu wa Msuva, lengo la mafunzo hayo lilikuwa kuwaandaa viongozi wenye uwezo wa kusimamia askari na watumishi chini yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za mfumo wa kijeshi unaotekelezwa katika taasisi za Jeshi la Uhifadhi.

Aliwataka wahitimu kuwa viongozi wa mfano kwa kuonesha nidhamu, uaminifu, kulinda siri za taasisi na kujenga mshik**ano kazini.

"Panapokuwa na upendo kuna umoja, panapokuwa na umoja kuna nguvu, na penye nguvu hakuna changamoto isiyoweza kushindwa," alisema.

Kwa niaba ya wahitimu, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Meneja Uhusiano wa TFS, Johari Kachambwa, alisema mafunzo hayo yamewaongezea maarifa, stadi na maadili ya kijeshi yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Alisema washiriki wamejengewa uwezo katika nidhamu, itifaki za kijeshi, matumizi salama ya silaha, usimamizi wa watumishi pamoja na utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi kwa kuzingatia sheria na amri za jumla za Jeshi la Uhifadhi.
Kachambwa aliwashukuru viongozi wa TFS kwa kuwezesha watumishi walioajiriwa kabla ya mabadiliko ya mfumo wa taasisi pamoja na wale waliohamia kutoka taasisi zisizo za kijeshi kupata mafunzo hayo maalumu ili kuendana na mfumo wa sasa wa utendaji.

"Tunawaahidi viongozi wetu kuwa tutatumia maarifa, ujuzi na maadili tuliyojifunza kutekeleza majukumu yetu kwa uadilifu, nidhamu, weledi na kujituma kwa maslahi ya taasisi na taifa," alisema.

Picha zaidi link: https://drive.google.com/drive/folders/1XL1hf1eHYmd46vjo-nAVSq9t13NAlTqX?usp=sharing

31/07/2026

Address

P. O. Box, Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
40832

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Forest Services Agency posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tanzania Forest Services Agency:

Shortcuts

Share