02/09/2026
📍KUSINI UNGUJA
K**ati ya Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Mkoa wa Kusini Unguja imeendesha mkutano wa elimu na uhamasishaji kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano kwa lengo la kuimarisha ulinzi wa watoto dhidi ya athari za matumizi mabaya ya huduma za mawasiliano.
K**ati imetoa elimu kwa wanafunzi wa Madrasa iliyopo katika Kijiji cha Bambi, Shehia ya Mitakawani, Jimbo la uzini, Wilaya ya Kati.
Mafunzo hayo yalihusu usalama wa mtoto mitandaoni, matumizi sahihi ya mtandao kwa watoto, pamoja na njia za kutoa taarifa pindi wanapobaini changamoto katika matumizi ya huduma za mawasiliano.
Katika hatua nyingine K**ati hiyo ilikutana na wajane katika Kijiji cha Mgeni Haji, Shehia ya Mgeni Haji, Jimbo la uzini, Wilaya ya Kati.
Akizungumza na wazazi hao, Mjumbe wa K**ati hiyo ndugu Mohamed Said alisema "watoto walioondokewa na wazazi wao ni wahanga zaidi wa matumizi mabaya ya mitandao, hivyo ni muhimu wazazi au walezi kuwa makini na kuwaelimisha mapema kabla ya athari kutokea".
Wazazi hao walielimishwa kuhusu matumizi sahihi ya mawasiliano na jinsi ya kuwalinda watoto wao dhidi ya athari zinazoweza kutokea kutokana na matumizi yasiyo sahihi ya mawasiliano.
K**ati ya Watumiaji wa huduma za mawasiliano Mkoa wa Kusini Unguja inaendelea na jitihada za kuelimisha watumiaji ikiwa ni sehemu muhimu ya majukumu ya K**ati ya kuelimisha na kusambaza taarifa zenye maslahi ya watumiaji wa huduma za bidhaa za mawasiliano .
mtandaoni
wa mtoto mtandaoni
kwa uma