Occupational Safety and Health Authority - OSHA

Occupational Safety and Health Authority - OSHA OSHA ni Wakala wa serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu).

Taasisi hii ina wajibu wa kuwalinda wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vilivyopo katika sehemu za kazi ambavyo vinaweza kusabisha magonjwa na ajali. Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa kazi ( OSHA) ilianzishwa inchini mwaka 2001 chini ya Sheria Na. 30 ya Wakala wa Serikali ya mwaka 1997 k**a sehemu ya Mpango wa Maboresho katika utoaji wa Huduma za Serikali kwa wananchi. Makusudi ya kuanzishwa kwa OS

HA ni kupata chombo cha serikali kwa ajili ya kusimamia Usalama na Afya mahali pa kazi. OSHA ina jukumu la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanafanya kazi katika mazingira ambayo ni salama na yenye kulinda afya zao kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa katika kuzuia ajali na magonjwa yatokanayo na kazi. Taasisi hii ina majukumu makuu manne;
-Kusimamia Utekelezaji wa Sheria Namba 5 ya mwaka 2003 ya Usalama na Afya na Mahali pa Kazi.
-Kushauri serikali kuhusu masuala ya usalama na afya mahali pa kazi, kuhusiana na sera, kanuni na miongozo mbalimbali ya usimamizi wa Usalama na Afya Nchini ikiwemo kushauri namna ya kuridhia mikataba ya kimataifa kuhusu masuala ya Usalama na Afya.
-Kuongeza uelewa miongioni mwa wadau kususiana na masuala ya Usalama na Afya kwa kutoa mafunzo mbalimbali ikiwemo kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wadau
-Kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na masuala ya usalama na afya katika sehemu za kazi ili kuweza kushauri serikali namna bora ya kutekeleza sheria tajwa.

Mtendaji mkuu wa OSHA Bi. Khadija Mwenda alikuwa ni miongoni mwa wakuu wa taasisi waliohudhuria halfa ya Uzinduzi wa Kit...
23/08/2026

Mtendaji mkuu wa OSHA Bi. Khadija Mwenda alikuwa ni miongoni mwa wakuu wa taasisi waliohudhuria halfa ya Uzinduzi wa Kituo cha kufua umeme cha Mwalimu Julius Nyerere, uzinduzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan. OSHA ni miongoni mwa wadau wakubwa waliofanikisha ukamilishajishi kwa wakati na ufanisi wa kituo hiko, kupitia kaguzi mbalimbali zilizofanyika kwenye mradi huo kuhakikisha suala usalama na afya linakuwa nguzo muhimu kwa wafanyakazi kwenye mradi huo wakati wote wa utekelezaji wa mradi na baada ya mradi. Huu ni uwekezaji mkubwa kwa taifa kwani zaidi ya fedha za Kitanzania Trion 7 zimewekezwa kwenye kituo hicho ambacho kinazalisha Umeme megawati 2115 na kufanya nnchi kujitosheleza kwa umeme wakati wote na hivyo kuchochea ukuaji wa Uchumi nchini

Mkufunzi kutoka OSHA, Bwn Simon Lwaho akitoa mada kwenye mkutano wa Maafisa Utumishi na Utawala kutoka nchi mbalimbali b...
21/08/2026

Mkufunzi kutoka OSHA, Bwn Simon Lwaho akitoa mada kwenye mkutano wa Maafisa Utumishi na Utawala kutoka nchi mbalimbali barani Afrika, mkutano wao wa mwaka ambao umeanza tarehe 18 Agosti, 2026 Jijini Arusha Tanzania, OSHA inashiriki kikamilifu katika Mkutano huo, kwa kutambua mchango mkubwa wa Maafisa Utumishi katika kusimamia watumishi, na usimamizi wa masuala ya Usalama na Afya katika maeneo yao kazi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akifanya majumuisho ya micha...
15/08/2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akifanya majumuisho ya michango ya Wajumbe wa Kamati katika kikao cha Kamati hiyo kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi. Khadija Mwenda, akitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizoibuliwa na Wajumbe wa Kamati ya Bung...
15/08/2026

Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi. Khadija Mwenda, akitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizoibuliwa na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kufuatia taarifa kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwaka wa fedha 2025/2026 iliyowasilishwa katika kikao cha Kamati hiyo.

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI SERIKALI KUIONGEZA WATAALAM OSHAKamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imei...
15/08/2026

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI SERIKALI KUIONGEZA WATAALAM OSHA
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imeishauri Serikali kuiongezea wataalam Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ili Taasisi hiyo iweze kuimarisha afya, usalama na ustawi wa wafanyakazi nchini.

Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hawa Chakoma, Bungeni Jijini Dodoma (Agosti 12, 2026), alipokuwa akifungua kikao cha Kamati kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 ikiangazia mwenendo wa usajili wa maeneo ya kazi pamoja na utoaji wa elimu ya usalama na afya mahali pa kazi kwa umma kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Taarifa hiyo iliwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu ambaye aliambatana na wataalam katika Ofisi yake akiwemo Katibu Mkuu, Bi. Mary Maganga na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Waziri Sangu mbele ya Kamati hiyo, kwa mwaka fedha 2025/2026, OSHA imesajili maeneo ya kazi 16,813 na kutoa mafunzo ya usalama na afya kwa wadau wapatao 45,089 idadi ambayo ni zaidi ya lengo ya kuwafikia wadau 40,000.

Akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja za wajumbe wa Kamati, Mtendaji Mkuu wa OSHA amesema maeneo ya kazi yanayosajiliwa na OSHA yanapaswa kukidhi vigezo vilivyowekwa kikiwemo kigezo cha uwepo wa pande mbili zinazotegemeana ambazo ni mwajiri na mwajiriwa.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Hawa Chakoma, alipokuwa akifanya majumuisho ya michango ya Wajumbe wa Kamati, ameishauri Serikali kuiongezea Taasisi ya OSHA watumishi ili kuiwezesha kutekelezaja majukumu yake ipasavyo kutokana na watumishi 376 waliopo kutokidhi mahitaji ya watendaji wa shughuli za msingi za Taasisi hiyo.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, amesema serikali imejipanga kuendelea kuhamasisha uzingatiaji wa taratibu zote muhimu za usalama na afya kwa waajiri na wafanyakazi katika sekta ya umma na binafsi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, akifafanua masuala mbalimbali yaliyopo...
15/08/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, akifafanua masuala mbalimbali yaliyopo katika taarifa yake aliyoiwasilisha katika kikao cha Kamati kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, wakifuatilia mjadala baada ya taarifa ya utekeleza...
15/08/2026

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, wakifuatilia mjadala baada ya taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwaka wa fedha 2025/2026 iliyowasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu Bungeni Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Bi. Mary Maganga (kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Nchi...
15/08/2026

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Bi. Mary Maganga (kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Dkt. Aveline Munisi katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (wakwanza kulia) na Naibu wake, Dkt. Av...
15/08/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (wakwanza kulia) na Naibu wake, Dkt. Aveline Munisi (Katikati) wakiwa na Katibu Mkuu Wizara hiyo, Bi. Mary Maganga (kushoto) katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Bi. Mary Maganga, akiwahutubia watumishi wapya wa OSHA k...
15/08/2026

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Bi. Mary Maganga, akiwahutubia watumishi wapya wa OSHA katika mafunzo ya awali (induction training) yaliyofanyika Jijini Dodoma kwa muda wiki moja (Agosti 10-15, 2026).

Address

Ikungi Street
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 15:30
Tuesday 09:00 - 15:30
Wednesday 08:00 - 15:30
Thursday 08:00 - 15:30
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255222760548

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Occupational Safety and Health Authority - OSHA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Occupational Safety and Health Authority - OSHA:

Shortcuts

Share