Occupational Safety and Health Authority - OSHA

Occupational Safety and Health Authority - OSHA OSHA ni Wakala wa serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu).

Taasisi hii ina wajibu wa kuwalinda wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vilivyopo katika sehemu za kazi ambavyo vinaweza kusabisha magonjwa na ajali. Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa kazi ( OSHA) ilianzishwa inchini mwaka 2001 chini ya Sheria Na. 30 ya Wakala wa Serikali ya mwaka 1997 k**a sehemu ya Mpango wa Maboresho katika utoaji wa Huduma za Serikali kwa wananchi. Makusudi ya kuanzishwa kwa OS

HA ni kupata chombo cha serikali kwa ajili ya kusimamia Usalama na Afya mahali pa kazi. OSHA ina jukumu la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanafanya kazi katika mazingira ambayo ni salama na yenye kulinda afya zao kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa katika kuzuia ajali na magonjwa yatokanayo na kazi. Taasisi hii ina majukumu makuu manne;
-Kusimamia Utekelezaji wa Sheria Namba 5 ya mwaka 2003 ya Usalama na Afya na Mahali pa Kazi.
-Kushauri serikali kuhusu masuala ya usalama na afya mahali pa kazi, kuhusiana na sera, kanuni na miongozo mbalimbali ya usimamizi wa Usalama na Afya Nchini ikiwemo kushauri namna ya kuridhia mikataba ya kimataifa kuhusu masuala ya Usalama na Afya.
-Kuongeza uelewa miongioni mwa wadau kususiana na masuala ya Usalama na Afya kwa kutoa mafunzo mbalimbali ikiwemo kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wadau
-Kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na masuala ya usalama na afya katika sehemu za kazi ili kuweza kushauri serikali namna bora ya kutekeleza sheria tajwa.

Usikose kufuatilia Makala Maalum inayoangazia matukio yaliyojiri katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama na A...
29/05/2026

Usikose kufuatilia Makala Maalum inayoangazia matukio yaliyojiri katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Mkoani Njombe.

28/05/2026
Tunawatakia Sikukuu njema ya Eid Al Adha, wadau wetu.
26/05/2026

Tunawatakia Sikukuu njema ya Eid Al Adha, wadau wetu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya uzinduzi wa Bodi ...
26/05/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya uzinduzi wa Bodi ya 7 ya OSHA.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya 7 ya OSHA.
26/05/2026

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya 7 ya OSHA.

3Mwenyekiti wa Bodi ya OSHA, Bw. Makwaia Makani, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wenzake katika hafla ya uz...
26/05/2026

3
Mwenyekiti wa Bodi ya OSHA, Bw. Makwaia Makani, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wenzake katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika Ofisi za OSHA Jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Bi. Zuhura Yunus, akimkaribisha, Waziri wa Nchi, Ofisi...
26/05/2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Bi. Zuhura Yunus, akimkaribisha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya 7 ya OSHA.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akitoa ufafanuzi kuhusu aina ya vitendea kazi vilivyoandaliwa kwa ajili ya Wa...
26/05/2026

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akitoa ufafanuzi kuhusu aina ya vitendea kazi vilivyoandaliwa kwa ajili ya Wajumbe Wapya wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya 7 ya OSHA. Miongoni mwa vitendea kazi hivyo ni pamoja na Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa Taasisi ya OSHA, Kitabu cha Sheria na Vifaa Kinga (PPEs).

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, meza kuu na Menejimenti ya OSHA wakiwa katika...
26/05/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, meza kuu na Menejimenti ya OSHA wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya 7 ya Ushauri ya OSHA.

Wajumbe wa Bodi ya 7 ya Ushauri ya OSHA wakikabidhiwa vitendea kazi na Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo...
26/05/2026

Wajumbe wa Bodi ya 7 ya Ushauri ya OSHA wakikabidhiwa vitendea kazi na Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika katika Ofisi za OSHA Jijini Dar es Salaam Mei 25, 2026.

Address

Ikungi Street
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 15:30
Tuesday 09:00 - 15:30
Wednesday 08:00 - 15:30
Thursday 08:00 - 15:30
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255222760548

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Occupational Safety and Health Authority - OSHA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Occupational Safety and Health Authority - OSHA:

Share