TPDC Tanzania

TPDC Tanzania natural gas,tpdc,Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania,wizara ya nishati na madini,gas,oil,mafuta,gesi,Tanzania Petroleum Development

Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) is the National Oil Company of Tanzania through which the Ministry of Energy and Minerals implements its petroleum exploration and development policies. TPDC has a manpower strength of about 400 and is organized into seven directorates and three Units, namely: Directorate of Upstream, Directorate of Downstream, Directorate of Finance, Directorate o

f Legal Services, Directorate of Cooperate Strategy and Planning, Directorate of Corporate Management, Directorate of Internal Audit, Communication Unit, Procurement Unit and Risk Management Unit. TPDC was established through the Government NoticeNo.140 of 30th May 1969 under the Public Corporations Act No.17 of 1969. The Corporation began operations in 1973. TPDC is a wholly owned Government parastatal, with all its shares held by the Treasurer Registrar.

08/09/2026

TPDC 2026 ||
"TPDC Marathon 2026 inalenga kujenga daraja kati ya nguvu ya michezo, dhamira ya kijamii na uwezo wa wadau mbalimbali kuchangia katika kuboresha huduma na kuokoa maisha," Bw. Derick Moshi akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC katika Uzinduzi wa TPDC Marathon 2026.

TPDC 2026 ||  Sehemu ya Nukuu ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge wakati...
08/09/2026

TPDC 2026 ||
Sehemu ya Nukuu ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari kwenye Uzinduzi wa TPDC Marathon 2026.

TPDC 2026 ||  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)...
07/09/2026

TPDC 2026 ||
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), limezindua rasmi TPDC Marathon 2026, kampeni inayolenga kukusanya zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuchangia matibabu na upasuaji wa moyo kwa watoto 100 wanaozaliwa na ugonjwa wa moyo nchini.
Uzinduzi huo umefanyika leo katika mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Johari Rotana, Dar es Salaam, ambapo Kaimu Mtendaji Mkuu wa TPDC, Ndugu Derick Moshi, na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Richard Kisenge, wameeleza umuhimu wa kampeni hiyo katika kusaidia watoto wenye changamoto za moyo na kupunguza mzigo wa gharama za matibabu kwa familia zenye uwezo mdogo wa kiuchumi.
TPDC Marathon 2026 yenye kaulimbiu “Hatua Yako, Okoa Maisha” inatarajiwa kufanyika tarehe 21 Novemba 2026, ikijumuisha mbio za kilomita 5, 10 na 21. Kupitia mbio hizo, TPDC na JKCI zinawalenga wadau mbalimbali, wakiwemo wananchi, sekta ya nishati na uchumi, taasisi za afya, wadau wa maendeleo na jumuiya za kidiplomasia, kushiriki katika kampeni hiyo ya kuokoa maisha.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Ndugu Derick Moshi amesema kampeni hiyo ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuhakikisha watoto wenye changamoto za moyo wanapata huduma muhimu za afya, huku akisisitiza kuwa kila hatua na kila mchango ni sehemu ya juhudi za kuokoa maisha na kuwapatia watoto hao matumaini ya kuendelea na maisha yao.

TPDC 2026 ||   Tunatoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, familia, ndugu na...
07/09/2026

TPDC 2026 ||

Tunatoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, familia, ndugu na Watanzania wote kwa ujumla.

07/09/2026

TPDC 2026 ||

Rasmi tumezindua TPDC MARATHON 2026 yenye kauli mbiu, 'Hatua yako - Okoa Maisha'.

TPDC 2026 ||  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo y...
04/09/2026

TPDC 2026 ||
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi limeendelea na zoezi la uhakiki wa taarifa za wananchi na mali zao zinazoguswa na Mradi wa Bomba la Gesi Asilia Kinyerezi–Chalinze, hatua inayolenga kuweka msingi sahihi katika maandalizi ya mchakato wa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi huo.
Zoezi hilo linafanyika katika maeneo yanayopitiwa na mradi, likiwa sehemu ya hatua muhimu za maandalizi ya upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa bomba hilo lenye urefu wa takribani kilomita 89, kutoka Kinyerezi, Dar es Salaam hadi Chalinze, Pwani. Mradi huo unalenga kuongeza upatikanaji wa gesi asilia kwa matumizi ya viwandani katika maeneo ya Kibaha Mji, Kibaha Wilaya na Chalinze, hivyo kuchochea shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.
Ili kuhakikisha usahihi na uhalali wa taarifa za waguswa na mali zao, TPDC inahakikisha kila Mwananchi anaepitiwa na mradi huu anapata fursa ya kuhakiki taarifa zake ili kuhakikisha usahihi na uhalali wa Majedwali ya uthamini Wakati wa ulipaji fidia. Hatua hii pia inalenga kuimarisha uwazi, ushirikishwaji na uelewa wa wananchi kuhusu mchakato wa utwaaji wa ardhi unaohusishwa na mradi.
Mradi wa Kinyerezi–Chalinze ni miongoni mwa hatua za TPDC katika kuendeleza matumizi ya gesi asilia nchini, huku utekelezaji wake ukitarajiwa kufungua fursa zaidi za ajira, uwekezaji na shughuli za kiuchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

TPDC 2026 ||   Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), CPA M***a Makame, amesema ushirik...
03/09/2026

TPDC 2026 ||

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), CPA M***a Makame, amesema ushirikishwaji wa jamii ni sehemu muhimu katika utekelezaji wa miradi, kwa kuwa jamii inayozunguka miradi ina nafasi ya kutoa ushirikiano na ridhaa inayowezesha shughuli za miradi kuendelea.

CPA Makame amesema hayo leo Septemba 3, 2026 jijini Dodoma wakati akizungumza katika Kongamano la Tano la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na Uwekezaji, lenye kauli mbiu “Ushiriki wa Watanzania ni Nguzo ya Uchumi Shindani na Jumuishi kuelekea Dira 2050.”

Amesema TPDC inatambua umuhimu wa kujenga uhusiano mzuri na jamii katika maeneo ambayo miradi inatekelezwa, hivyo Shirika limekuwa likitoa kipaumbele katika kushirikisha jamii na wadau wengine.

“Katika miradi yote tunahitaji jamii itupe leseni yake. Hivyo suala la kushirikisha jamii tunalichukulia jukumu hili kwa uzito na ndiyo maana leo tupo hapa tukiwa ni washiriki na wadhamini wa kongamano hili muhimu ambalo limehusisha washiriki zaidi ya 600,” amesema CPA Makame.

Ameongeza kuwa ushiriki wa TPDC katika kongamano hilo ni sehemu ya juhudi za kuendeleza mjadala kuhusu namna Watanzania wanavyoweza kushiriki na kunufaika na miradi ya kimkakati na uwekezaji nchini.

Kongamano hilo lilifanyika jijini Dodoma kwa siku mbili kuanzia tarehe 2-3 Septemba 2026 na kuhitimishwa na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, likiwakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi kujadili fursa za ushiriki wa Watanzania katika miradi ya kimkakati na uwekezaji.

TPDC 2026 ||  Jitihada za Serikali za kuwawezesha Watanzania kushiriki katika shughuli za kiuchumi zimeendelea kuzaa mat...
02/09/2026

TPDC 2026 ||

Jitihada za Serikali za kuwawezesha Watanzania kushiriki katika shughuli za kiuchumi zimeendelea kuzaa matunda katika sekta ya gesi asilia, huku viwanda vya kuchakata gesi asilia vya Madimba na Songosongo vikiendeshwa na wazawa kwa asilimia 100.

Akizungumza katika Kongamano la Tano la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati (Local Content) Mwaka 2026 jijini Dodoma Bw Eugene Isaya-Afisa kutoka TPDC anayeratibu Ushiriki wa Wazawa katika miradi ya Kimkakati ya Mafuta na gesi asilia nchini, amesema mafanikio hayo yanaonesha hatua zilizopigwa katika kuwawezesha wazawa kushiriki katika sekta ya mafuta na gesi.

“Jitihada za Serikali za kuwezesha ushiriki wa Watanzania zimezaa matunda katika sekta ya gesi asilia, kwani viwanda vya kuchakata gesi asilia vya Madimba na Songosongo vinaendeshwa na wazawa kwa asilimia 100,” amesema Eugene.

Ameongeza kuwa ajenda ya ushiriki wa Watanzania inalenga kuongeza thamani inayobaki nchini kupitia ajira, matumizi ya malighafi za ndani, ununuzi wa bidhaa na huduma za ndani, ushiriki wa taasisi za Kitanzania pamoja na uhawilishaji wa teknolojia.

Katika kuunga mkono ajenda hiyo, TPDC imeshiriki na kudhamini kongamano hilo kwa kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni Mia Moja (100).

Eugene ameongeza kuwa kuendelea kuimarisha ushiriki wa wazawa kutasaidia kuongeza fursa kwa Watanzania katika sekta ya mafuta na gesi, kukuza uwezo wa wazawa pamoja na kuhakikisha manufaa yanayotokana na rasilimali zilizopo yanaendelea kuwafikia Watanzania.

TPDC 2026 ||   JAMBO KUBWA LINAKUJA NOVEMBA 2026!
02/09/2026

TPDC 2026 ||

JAMBO KUBWA LINAKUJA NOVEMBA 2026!

01/09/2026

TPDC 2026 ||
TPDC Bonanza Kisemvule limekuwa zaidi ya michezo - limekuwa jukwaa la kujenga mshikamano, kuhamasisha ulinzi wa miundombinu ya gesi asilia, pamoja na kuchangia afya na ustawi wa jamii.
Kisemvule, asanteni kwa mapokezi, ushirikiano na mshikamano wenu.

Address

Azikiwe/Jamhuri Street
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TPDC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to TPDC Tanzania:

Shortcuts

Share